Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aweka jiwe la msingi kiwanda cha kuunganisha Matrekta jijini Dodoma

 

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweka jiwe la msingi kiwanda cha kuunganisha matrekta na zana nyingine za kilimo kwa lengo la kusogeza matumizi ya matrekta karibu na wakulima nchini na kuwapunguzia gharama.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweka jiwe la msingi kiwanda cha kuunganisha matrekta


Jiwe hilo la msingi liliweka na Rais katika viwanja vya Nanenane, Nzuguni Jijini Dodoma.

Akitoa maelezo ya awali, Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe alisema kuwa kiwanda cha kuunganisha matrekta na zana nyingine za kilimo ni ushirikiano wa kampuni ya Agricom na Mahindra kutoka nchini India. Alisema kuwa makubaliano baina ya wizara yake na Mwenyekiti wa taasisi ya sekta binafsi nchini, Angelina Ngalula ni kuwa kampuni hizo kufikia mwezi Juni, 2025 kiwanda hicho kianze kutoa huduma.

Aidha, kiwanda cha kuunganisha matrekta kinajengwa katika viwanja vya Nanenane, Nzuguni Dodoma eneo lenye ukubwa wa mita za mraba takribani mita za mraba 20,000 kikiunganisha matrekta aina na Swaraj na kutarajiwa kuzalisha ajira za kudumu 400 na ajira zisizo za kudumu zaidi ya 2000.

Ikumbukwe kuwa uwekezaji wa kiwanda hicho ni matokeo ya ziara ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini India na kualika wawekezaji wa India kuwekeza nchini Tanzania pamoja na mambo mengine.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma