CCM yampongeza Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan utekelezaji Ilani
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
CHAMA
cha Mapinduzi (CCM) kimempongeza Rais, wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi katika sekta ya Kilimo,
Mifugo na Uvuvi.
Pongezi
hizo zilitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara, John Mongela
alipotoa salamu za CCM katika kilele cha maonesho ya Nanenane kitaifa, Nzuguni
Dodoma.
Mongela
alisema “Ilani ya CCM ina kurasa 308, kurasa 33-56 zinaelezea sekta ya Kilimo, Mifugo
na Uvuvi. Leo mimi ni shahidi kwamba utekelezaji wa Ilani unafanywa kwa kiwango
cha juu sana, tumpongeze Rais na serikali yake. Chini ya uongozi wako ni kazi
kubwa inatambulika kwenye sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi”.
Aidha,
aliahidi CCM kuendelea kufanya kazi karibu na serikali ili wananchi wapate
maendeleo zaidi.
Akitoa
salamu kutoka kwa mabalozi wa nchi za nje, Balozi wa Marekani nchini Tanzania,
Michael Battle alisema kuwa washirika wa maendeleo wanaunga mkono juhudi za
Tanzania katika kukuza sekta za Kilimo, Mifugo na Uvuvi hasa ushiriki wa
wanawake na vijana.
Alisema
kuwa Serikali ya Marekani itaendelea kuchangia katika Kilimo cha Tanzania
kupitia mpango wa Feed the Future unaofadhiliwa na USAID.
Aidha,
alimhakikishia Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Marekani na washirika wake
wapo tayari kuitangaza Tanzania kuwa imefunguka kibiashara. “Mungu akupe nguvu
na hekima ya kuongoza Tanzania” alimalizia Balozi Battle.
Maonesho
ya Nanenane mwaka 2024 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Chagua viongozi bora
wa serikali za mitaa kwa maendeleo endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi”.
MWISHO
Comments
Post a Comment