Vijana waalikwa kushiriki Kongamano S/M Mbwanga
Na. Mwandishi Wetu
Vijana
wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kujitokeza na kushiriki kongamano
la vijana la Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025 lenye lengo la kutoa elimu kuhusiana na
fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo nchini.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kongamano la Vijana katika mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025, Abeid Msangi
Kauli
hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kongamano la Vijana katika mbio za Mwenge
wa Uhuru Mwaka 2025, Abeid Msangi akiongelea maandalizi ya kongamano hilo
litakalofanyika katika Shule ya Msingi Mbwanga iliyopo Halmashauri ya Jiji la
Dodoma.
Alisema
kuwa kongamano hilo limeandaliwa kwa ajili ya vijana wa Halmashauri ya Jiji la
Dodoma. “Nichukue nafasi hii kuwahamasisha vijana wa Jiji la Dodoma kujitokeza kwa
wingi katika kushiriki kongamano hilo. Kongamano hilo linalenga kuwajenga
vijana kuwa wazalendo, kuifahamu historian a falsafa ya Mwenge wa Uhuru. Pia
tutatoa elimu kwa vijana kuhusiana na umuhimu wa kushiriki Uchaguzi Mkuu wa
Mwaka 2025 kwa amani na utulivu. Mada nyingine zitakazofundishwa ni fursa za kiuchumi
katika sekta ya madini pamoja na fursa zilizopo Halmashauri ya Jiji Dodoma. Vilevile,
vijana watahamasishwa katika masuala ya afya ili waweze kulitumikia taifa
wakiwa na afya njema” alisema Msangi.
Akiongelea
vijana wanaolengwa katika kongamano hilo, aliwataka kuwa ni vijana mchanganyiko
kutoka katika vyuo, sekta binafsi na wajasiriamali na kusisitiza kuwa hakuna
ubaguzi. “Nipende kuwataarifu vijana kukimbilia fursa za namna hii kwasababu
zinajitokeza kwa mara moja kila mwaka tunapokuwa katika mbio za Mwenge wa
Uhuru. Fursa hizi ni muhimu kwasababu kuna vitu vingi vya kujifunza kama vijana,
lakini pia mafunzo hayo yatawapatia faida kutokana na kitu mlichojifunza”
alisema Msangi.
Mwenge
wa Uhuru Mwaka 2025 ulianza rasmi mbio zake katika Mkoa wa Dodoma tarehe 20
Aprili, 2025 na katika Wilaya ya Dodoma utapokelewa na kukimbizwa tarehe 26
Aprili, 2025 chini ya kaulimbiu isemayo “Jitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka
2025 kwa Amani na Utulivu”.
MWISHO
Comments
Post a Comment