JIJI LA DODOMA LATUMIA MIL. 23 KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetumia zaidi ya shilingi milioni 23 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo fedha kutoka serikali kuu, mapato ya ndani na wahisani pamoja na bakaa.



Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akiwasilisha taarifa fupi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Alisema kuwa katika kipindi cha kuanzia Julai, 2025 hadi kufikia Machi, 2026 halmashauri imetumia jumla ya shilingi 23,815,713,415.02 sawa na asilimia 91.19 ya fedha zilizopokelewa kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo. “Kati ya fedha hizo, shilingi 6,406,582,002.56 ni fedha kutoka serikali kuu, shilingi 16,807,859,627.46 mapato ya ndani, shilingi 601,771,785.00 fedha za wahisani na shilingi 5,279,467,344.52 ni fedha za bakaa. Kwa kipindi cha kuanzia Julai, 2025 hadi kufikia Machi, 2026, halmashauri imepokea jumla ya shilingi 25,314,611,746.31 sawa na asilimia 55.99 ya makisio yote ya fedha za miradi ya maendeleo, kiasi cha shilingi 7,139,598,162.00 ni fedha za serikali kuu, shilingi 814,771,785.00 ni fedha za wahisani na shilingi 17,360,241,799.31 ni fedha kutoka mapato ya ndani” alisema Fungo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya TAMISEMI, Florian Kyombo aliipongeza serikali ya awamu ya sita kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo katika halmashauri. Vilevile, alilipongeza Jiji la Dodoma kwa kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayogusa maisha ya wananchi.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Mwaka wa Fedha 2025/26, katika Mpango na Bajeti ilikadiria kutumia jumla ya shilingi 45,209,805,500.00 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo kupitia vyanzo mbalimbali vya fedha. Kati ya fedha hizo, shilingi 4,303,552,000.00 ni fedha za wahisani, shilingi 10,074,637,000.00 ni fedha kutoka serikali kuu na shilingi 30,951,616,500.00 ni fedha kutoka mapato ya ndani ambazo ni sawa na asilimia 68.46 ya bajeti ya miradi ya maendeleo.

MWISHO

 

 

Comments

Popular Posts

JIJI LA DODOMA LATOA VIWANJA 1,900 KWA WAFANYAKAZI

Ofisi ya Kata Zuzu yaboreshwa kwaajili ya utoaji huduma bora