Popular Posts
VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA JIJI LA DODOMA WAPEWA MAFUNZO YA MAADILI KATIKA UONGOZI NA UMUHIMU WA MAWASILIANO KWA VIONGOZI
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DODOMA VIONGOZI wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma watakiwa kusimamia misingi ya maadili na mawasiliano ili kulinda imani ya wananchi katika huduma wanazopewa. Rai hiyo imetolewa wakati wa mafunzo maalumu ya uongozi yaliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, yakilenga kuwajengea uwezo viongozi hao katika kusimamia rasilimali na kuhudumia umma kwa uadilifu, huku wakionywa kuwa mmomonyoko wa maadili duniani sasa ni tishio linalohitaji udhibiti wa pamoja. Akiwasilisha mada kuhusu maadili na umuhimu wa mawasiliano katika uongozi, Mhadhiri kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa (Hombolo), Ng'omange Merkiad alisisitiza kuwa kuwepo kwa taratibu na kanuni madhubuti za kimaadili ni jambo la lazima ili kuwepo na tabia inayofanana na inayotabirika wakati wa kuwahudumia wananchi. "Maadili sio masimulizi tu ya maneno, bali ni maelekezo ya vitendo yanayomwongoza kiongozi kujua nini cha kufanya na kwa wakati gani katika utekelezaj...
Umeme wa REA chachu ya viwanda vidogo vidogo Kata ya Ipala
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. John Masanja, IPALA Awamu ya kwanza ya umeme wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umechochea shughuli za maendeleo na kuinua uchumi wa wananchi katika Kata ya Ipala, Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ‘media tour’ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika kata hiyo kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Alisema kuwa serikali ya awamu ya sita imepeleka huduma ya umeme katika Kata ya Ipala. “Kata yetu imefikiwa na awamu ya kwanza ambayo ina faida nyingi sana. Wananchi wanafanya shughuli mbalimbali zinazojumuisha matumizi ya umeme kwa kiwango kikubwa na naamini kwa siku za usoni hapa kwetu kutakuwa mtaa wa viwanda vya aina tofauti” alisema Magawa. Nae mkazi wa Kata ya Ipala, Mathias Masita aliishukuru serikali kwa kuwapelekea umeme kwasababu maisha yao yamebadilika na wanafanya shughuli zinazohusisha umeme kwa kiwango kikubwa. “Mradi wa REA umetunufaisha s...
Comments
Post a Comment