Posts

Showing posts from 2026

Watumishi wa Kanda Namba Tatu watembelea Zahanati ya Soweto

Image
  Watumishi wa Kanda Namba Tatu watembelea Zahanati ya Soweto jijini Dodoma ambayo imekamilika na imeanza kufanya kazi. Zahanati hiyo inajumuisha jengo la huduma ya wagonjwa wa nje (OPD), chumba cha daktari, chumba cha kujifungulia wanawake, maabara na huduma ya mama, baba na mtoto. Uwepo wa zahanati hiyo ni kusogeza huduma karibu na wananchi ambao walikuwa wanatembea umbali mrefu kufuata huduma za afya katika Kituo cha Afya Zuzu au kwenda Hospitali ya Mkoa General  

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipanda mti wa Muembe (Mangifera indica) katika eneo la Bungi Kilimo, Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 27 Januari, 2026, wakati wa kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa. Rais Mhe. Dkt. Samia alizaliwa tarehe 27 Januari, 1960 katika Kijiji cha Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipanda mti wa Muembe (Mangifera indica) katika eneo la Bungi Kilimo, Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 27 Januari, 2026, wakati wa kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa. Rais Mhe. Dkt. Samia alizaliwa tarehe 27 Januari, 1960 katika Kijiji cha Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Kikao cha wazazi Shule ya Sekondari Mtumba katika uhamasishaji wa upatikanaji chakula shuleni

Image
Afisa Lishe wa Jiji la Dodoma, Frida Mollel alitoa wito kwa wazazi ya juu ya faida ya chakula shuleni na jinsi kinavyoweza kusaidia kuongeza ufaulu na kupunguza ukatili wa kijinsia kwa watoto huku akisema kuwa shule zinazotoa chakula watoto hufanya vizuri kwenye masomo na ufaulu wao upo juu.  

DKT. MWIGULU ASHIRIKI ZOEZI LA UPANDAJI MITI, DODOMA

Image
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 27, 2026 ameshiriki zoezi la upandaji miti, mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu Mlimwa Jijini Dodoma. Zoezi hilo ni sehemu ya hatua ya kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa kizalendo wa kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa vitendo vya kulinda mazingira. Akizungumza baada ya zoezi hilo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu akiwa ameambatana na mwenza wake Mama Neema Mwigulu, amempongeza Rais Dkt. Samia kwa uongozi wake kwa kuendelea kudhihirisha namna alivyo kiongozi mwenye maono, mbunifu na anayejali maslahi mapana ya Taifa. “Shughuli hii imekuwa na utofauti kwa kusababisha miti ipandwe kila kona ya nchi, kwenye vitabu vyetu vitukufu, kupanda mti ni moja ya ibada kwasababu wanufaika wa miti ni wengi” Kadhalika, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa wito kwa Watanzania kuadhimisha siku zao za kuzaliwa kwa kupanda miti. “Tunapokuwa na jambo la kukumbuka la aina hii, tufanye kitu ambacho kinaweka alam...

Kampeni ya upandaji miti Jiji la Dodoma yafanikiwa S/M Mbwanga

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Jiji la Dodoma limeendelea kutekeleza kampeni ya upandaji miti ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhifadhi mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Zoezi hilo limefanyika katika maeneo mbalimbali ya jiji ikiwemo shule, taasisi za umma, barabara na maeneo ya makazi. Akizungumza katika Shule ya Msingi Mbwanga, Katibu Tawala wa Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alisema kuwa zoezi la upandaji miti ni muendelezo wa kulifanya Jiji la Dodoma kuwa la kijani na pia kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika siku yake ya kuzaliwa. Aliwataka wanafunzi, walimu na wananchi kwa ujumla kujenga utamaduni wa kupanda na kutunza miti ili kulinda mazingira na kuhakikisha ustawi wa vizazi vijavyo. Alisisitiza kuwa upandaji wa miti shuleni una mchango mkubwa katika kuelimisha watoto kuhusu umuhimu wa mazingira tangu wakiwa wadogo. "Tunapanda miti hii kwasababu ya kuungana na Mhe. Rais, Dkt. Samia kumpongeza katik...

DIWANI KATA YA MNADANI ASHIRIKI KIKAO CHA WAZAZI MIYUJI SEKONDARI

Image
Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge amepata wasaa wa kuzungumza na wazazi wa wanafunzi wa shule ya sekondari Miyuji. Katika kikao hicho Diwani Kerenge alisisitiza umuhimu wa wazazi kushirikiana na walimu katika kusimamia watoto ili kuongeza ufaulu shuleni hapo. Pia alisisitiza kuendeleza uwazi dhidi ya michango ya wazazi wanayotoa katika shule hiyo. Alitoa wito kwa wazazi na walimu kuhakikisha watoto wote wanapata chakula shuleni chenye virutubisho ili kuongeza uwezo wa kusoma vizuri wakati wote wanapokuwa shuleni. Diwani Kerenge aliwashauri wazazi kuhakikisha watoto wote wanakaa kambi hasa madarasa ya mitihani ili wapate muda wa kusoma vizuri.  

Baraza la Wafanyakazi Jiji la Dodoma lajadili rasimu ya mapendekezo ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka 2026/2027

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Baraza la Wafanyakazi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma limekutana kujadili taarifa ya utekelezaji wa shughuli za halmashauri pamoja na rasimu ya mapendekezo ya M pango na B ajeti kwa M waka wa F edha 2026/2027 ambapo uongozi huo ulieleza kiasi cha bajeti kinachotarajiwa kutekelezwa katika kipindi hicho. Akizungumza katika kikao hicho, Mchumi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Francis Kaunda alisema kuwa halmashauri imekasimia kukusanya shilingi bilioni 166 kutoka vyanzo vyake vya ndani, serikali kuu na wahisani mbalimbali kwaajili ya kutekeleza shughuli za maendeleo, utoaji huduma na kujiendesha. Kaunda alisema kuwa kutoka mapato ya ndani kiasi cha shilingi bilioni 73 kinatarajiwa kukusanywa ambapo kati ya fedha hizo shilingi bilioni 46 ni mapato yasiyolindwa na shilingi bilioni 27 ni mapato lindwa. Fedha hizo zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo na matumizi ya kawaida. Aliongeza kuwa kati ya fedha hizo, kiasi cha shilingi bilioni 32 kimepangwa kwa ...

Baraza la Biashara la Wilaya ya Dodoma lapongezwa kwa kuimarisha mazingira ya uwekezaji

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Sekta ya Biashara na Uwekezaji Wilaya ya Dodoma imepongezwa kwa kuboresha mazingira ya ufanyaji wa shughuli za kiuchumi, hatua iliyochochea ongezeko la wafanyabiashara na wawekezaji wanaotumia fursa zilizopo kukuza uchumi wa wilaya hiyo. Hayo yalielezwa na Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipokuwa akizungumza wakati wa Kikao cha Baraza la Biashara la Wilaya ya Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri jijini Dodoma. Alilipongeza baraza hilo kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya katika kuhamasisha uwekezaji na shughuli za kiuchumi. “Jiji letu limeendelea kusimamia mifumo inayotoa huduma kwa wananchi. Tunaelezwa kuwa pale SGR huduma ya ‘shuttle’ inapatikana ambapo zinapunguza kadhia kwa wageni ambao hawaujui usafiri wa bajaj na bodaboda. Pia Kanda zimeanzishwa na zinafanya vizuri sana kwa kusaidia wananchi kupata huduma zinazopatikana katika ofisi kuu, hali inayowasaidia kuepuka kupoteza muda...

Duka la Kuuza Viwanja kutoa huduma Jumamosi Tarehe 10 Januari, 2026

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Ofisi za Halmashauri ya Jiji la Dodoma zitakuwa wazi siku ya Jumamosi tarehe 10 Januari, 2026 kuanzia saa 2:30 hadi saa 9:30 alasiri kwa lengo la kuwahakikishia huduma bora hasa upatikanaji wa ‘control number’ za malipo ya viwanja ndani ya muda wa notisi ya halmashauri ya siku 21. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikali Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dennis Gondwe alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu maelekezo ya Mkurugenzi wa Jiji hilo juu ya ofisi hizo kufunguliwa siku ya Jumamosi, tarehe 10 Januari, 2026. “Ndugu waandishi wa habari, napenda kuwatangazia kuwa katika kufanikisha utekelezaji wa Notisi ya siku 21 ya kulipa madeni ya viwanja kwa wananchi waliochukua viwanja eneo la Mtumba Zone II, III na Kikombo kuanzia tarehe 30 Desemba, 2025 inayokamilika tarehe 19 Januari, 2026. Hivyo, mkurugenzi ameagiza ofisi za halmashauri iliyokuwa manispaa ya zamani duka la kuuza viwanja ziwe wazi kuanzia saa 2:30 asubuhi hadi sa...