Posts

Showing posts from 2025

Jiji lataka mpango kazi kukamilisha ujenzi shule ya Mil. 299,200,000 utekelezwe

Image
Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imemuagiza Mkuu wa Shule ya Sekondari Nzuguni kusimamia mpango kazi wa ujenzi wa shule mpya ya msingi ya mkondo mmoja yenye gharama ya shilingi 299,200,000 fedha kutoka mradi wa BOOST ili ikamilike kwa wakati kwa mujibu wa mkataba. Agizo hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoongoza timu hiyo kutembelea na kukagua hatua ya ujenzi wa shule hiyo katika Kata ya Nzuguni, jijini Dodoma. Alisema kuwa mpango kazi wa ujenzi wa shule hiyo unatakiwa kufahamika na kila anayehusika na kusimamia utekelezaji wake ili ujenzi ukamilika kwa wakati. Idadi ya mafundi anatakiwa kuongezeka ili kuhakikisha mradi unakamilika haraka, aliongeza. Pia, ilishauriwa manunuzi yote ya vifaa pamoja na madawati yatangazwe kwenye mfumo wa NeST mapema ili kusiwe na ucheleweshaji katika utekelezaji wa mradi. Akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa shule mpya ya msingi mkondo mmoja kwa Ti...

Mwalimu Mkuu S/M Mazengo apongezwa usimamizi ukarabati wa shule

Image
Na. Dennis Gondwe, KIKUYU KASKAZINI Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imempongeza Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mazengo kwa kusimamia vizuri ukarabati wa shule kupitia fedha za mradi wa BOOST na kumtaka kuongeza kasi kukamilisha kabla ya shule kufunguliwa ili wanafunzi wasiwe na upungufu wa madarasa ya kusomea. Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoongoza timu hiyo kukagua ukarabati wa shule hiyo jijini Dodoma. Baada ya kupokea taarifa ya ukarabati wa shule hiyo iliyowasilishwa kwa ustadi na mwalimu mkuu na kukagua mradi huo, Mwenyekiti wa Timu ya Menejimenti alisema kuwa mwalimu mkuu (Mwl. Rehema Nkungu) anafanya kazi kubwa na nzuri ya kusimamia ukarabati wa mradi huo. “Hapa kuna ushirikiano mzuri, ninataarifa ya utendaji mzuri wa (Mkaguzi Majengo, Jacob Stephen) anayesimamia mradi huu tangu nikiwa ofisini, hongera sana. Matamanio yetu, kasi iongezeke ya ukarabati huu ukamili...

Menejimenti ya Jiji la Dodoma yaelekeza ukarabati S/M Dodoma Mlimani kufanyika usiku na mchana

Image
Na. Dennis Gondwe, TAMBUKARELI Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Dodoma Mlimani ametakiwa kusimamia ukarabati wa madarasa 12 kufanyika hadi usiku ili ukamilike mapema kabla ya shule kufunguliwa kwa sababu fedha shilingi 150,000,000 zimeshatolewa. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoongoza Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kutembelea na kukagua maendeleo ya ukarabati wa madarasa 12 kwa shilingi 150,000,000 fedha kutoka mradi wa BOOST. Alisema kuwa kazi ya ukarabati inatakiwa kufanyika usiku na mchana ili kukamilisha madarasa hayo kwa wakati. Aliongeza kuwa fedha ipo, hivyo, hakuna sababu ya kufanya mradi uchelewe kukamilika, na kuwataka afisa mtendaji kata na mtaa kuweka kambi shuleni hapo kusimamia utekelezaji wa ukarabati wa shule hiyo.    Akiongelea mradi huo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Dodoma Mlimani, Mwl. Jenipher Mhavile alisema kuwa ukarabati ulianza 13 Oktoba, 2025. “Hatua ya ukara...

Chidachi S/M watakiwa kuboresha mpango kazi wa fundi kukamilisha ujenzi mradi wa BOOST

Image
Na. Dennis Gondwe, MKONZE Mhandisi wa halmashauri, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Chidachi wametakiwa kufanya mapitio ya mpango kazi wa mafundi na kuandaa mpango wa haraka unaotekelezeka ili kukamilisha mradi wa ujenzi wa miundombinu kwa gharama ya shilingi 182,100,000 fedha kutoka mradi wa BOOST shuleni hapo. Agizo hilo lilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoambatana na Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kukagua ujenzi wa mradi wa miundombinu katika Shule ya Msingi Chidachi kwa fedha za ufadhili wa BOOST. Timu ya Menejimenti ilipokagua mradi huo haikuridhika na kasi ya ujenzi na kuelekeza mhandisi wa halmashauri, mwalimu mkuu pamoja na fundi kupitia upya mpango kazi na kutengeneza mpango kazi wa haraka unaotekeleza ili kukamilisha mradi huo kwa wakati uliopangwa. Mkurugenzi alisema kuwa kila mmoja anatakiwa kuongeza umakini katika usimamizi ili mradi ukamilishwe kwa viwango, na kusema kuwa menejimenti haitachele...

Jiji la Dodoma lataka kasi ukarabati madarasa Kitelela Sec

Image
Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI TIMU ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeelekeza kuongeza kasi ya ukamilishaji wa ukarabati wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kitelela ili wanafunzi watakapofungua shule mwezi Januari, 2026 waweze kuyatumia. Agizo hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoongoza timu hiyo kutembelea na kukagua maendeleo ya ukamilishaji wa ukarabati wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kitelela iliyopo Kata ya Nzuguni, jijini Dodoma. Dkt. Sagamiko ambae ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema kuwa baada ya kukagua hali ya ukarabati inavyoendelea, kasi siyo ya kuridhisha. “Hivyo, maelekezo yetu ni kwamba, kasi iongezeke ili mradi ukamilike kwa wakati na shule zinapofunguliwa wanafunzi waanze kutumia madarasa hayo” alisema Dkt. Sagamiko. Wakati huohuo, alimuagiza Afisa Mtendaji wa Kata ya Nzuguni na Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Kitelela kuweka kambi katik...

Diwani Iyumbu apongezwa usimamizi miradi

Image
Na. Dennis Gondwe, IYUMBU DIWANI wa Kata ya Iyumbu amepongezwa kwa kusimamia miradi ya maendeleo na kutakiwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa wataalam wa kata hiyo ili kukamilisha miradi kwa wakati ili iweze kutoa huduma kwa wananchi. Pongezi hizo zilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoongoza Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji kutembelea na kukagua ukamilishaji wa madarasa mawili, maabara tatu, jengo la utawala na matundu nane ya vyoo katika Shule ya Sekondari Iyumbu. “Mheshimiwa Diwani ninakupongeza kwa kusimamia vizuri miradi katika Kata ya Iyumbu. Kwa umoja huu kata inakwenda kubadilika kimaendeleo, wape ushirikiano wataalam katika kata ili kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kwa nafasi yako upo katika wakati mzuri zaidi kuhamasisha wananchi kujitolea kushiriki shughuli za maendeleo na nguvu kazi” alisema Dkt. Sagamiko. Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Iyumbu, Sadick Mpondamali aliishukuru halmashauri kwa kut...

Mil. 838 zakopeshwa wanawake, vijana na wenye ulemavu Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imetoa mikopo ya shilingi 838,775,212 kwa vikundi 54 katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2024/2025 hadi kufikia Oktoba 2025/2026 kwa lengo la kuviongezea mtaji wa kutekeleza shughuli za kujikwamua kiuchumi. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Juni hadi Oktoba, 2025 katika mkutano wa kwanza wa halmashauri baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani. Alisema kuwa vikundi 17 vya wanawake vilikopeshwa shilingi 274,334,000, vikundi 26 vya vijana vilikopeshwa shilingi 460,041,212 na watu wenye ulemavu vikundi 11 vilikopeshwa shilingi 104,400,000. Akiongelea uchangiaji wa michango ya asilimia 10, alisema kuwa mwaka 2024/2025 halmashauri ilitenga shilingi 4,032,510,000, kwa mwezi Juni, 2024/2025, jumla ya shilingi 373,778,597.12 zimechangiwa katika mfuko. “Mwaka 2025/2026 halmashauri imetenga b...

Madiwani watakiwa kuifanya Dodoma kuwa kinara ukusanyaji mapato

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri amelitaka Baraza la Madiwani kuendelea kuifanya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuwa kinara katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kupitia mapato ya ndani ili kuwaletea wananchi maendeleo na kuboresha maisha yao. Kauli hiyo aliitoa alipokuwa akiwasalimia madiwani katika mkutano wa kwanza wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri jijini hapa. Alhaj Shekimweri alisema “katika mapato ya ndani mmekuwa vinara katika kutekeleza miradi mizuri   ya maendeleo. Tumeona miradi ya hoteli, mradi wa Soko la wazi la Machinga, miradi ya ujenzi wa barabara, mfano ile ya Nala kuelekea hospitali ya jiji na miradi mingine mingi. Nendeni mkawe vinara wa kutekeleza miradi ya maendeleo. Ninayasema haya kwa kumuenzi Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba mnapochukua madaraka yale mema yaliyoanzishwa na wenzenu msiyaweke kando, ambayo hayajakamilika mkayakamilishe, yanayoendelea mkayakalishe huku ...

Madiwani Jiji la Dodoma watakiwa kuwa walezi

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MADIWANI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kutumia nafasi yao na kuwa walezi kwa maafisa watendaji katika kata zao na kuwasimamia ili kuwaletea maendeleo wananchi. Rai hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipokuwa akiongea na madiwani katika mkutano wa kwanza wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani wa tarehe 29 Oktoba, 2025. “Waheshimiwa Madiwani, nataka niwaombe sana mkawalee maafisa watendaji wenu kwenye ngazi ya kata. Mstahiki Meya, ninasema hapa kwa kuwaangukia na kuwaomba, mkawe walezi, ninyi ndiyo wenyeviti wa kamati za maendeleo kwenye kata, mkono wako wa kulia ni katibu, ambae ni Afisa Mtendaji wa Kata. Watendaji hawa inawezekana wakawa na madhaifu ya hapa na pale, nenda ukawe mlezi, nenda ukawe mzazi, yeye pamoja na wataalam wengine ngazi ya kata. Wasaidieni wafanye majukumu yao sawasawa ili wewe upate matokeo na kuwaletea wananchi maendeleo. Mimi, nitakusifu san...

Madiwani Jiji la Dodoma watakiwa kutoa tamko la rasilimali na madeni

Image
                                              Na. Dennis Gondwe, DODOMA SEKRETARIETI ya Maadili ya Viongozi wa Umma imewataka madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kutoa tamko la rasilimali na madeni kwa mujibu wa sheria. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Msaidizi Kanda ya Kati, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jasmin Bakari wakati akiwaongoza kutoa tamko la kimaandishi la ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Niwapongeze kwa kufanikiwa kuchaguliwa kuwa madiwani, ni mategemeo yetu mtatekeleza majukumu yenu kwa viwango vya juu vya maadili, na mviishi viapo vyenu. Niwakumbushe madiwani na viongozi wote waliopo hapa kutoa tamko la rasilimali na madeni, tunawakumbusha kuingia kwenye mfumo kwa wale wapya kuna sehemu ya kujisajili. Kwa wale waliokuwa baraza lililopita wataingia kwa aka...

Jiji la Dodoma lakusanya 104% Mapato ya ndani 2024/2025

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma ilikusanya shilingi 65,042,215,034 sawa na asilimia 104 ya lengo la mwaka la mapato ya ndani kwa Mwaka wa Fedha 2024/ 2025. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Juni hadi Oktoba, 2025 katika mkutano wa kwanza wa halmashauri baada ya uchaguzi mkuu wa Rais, Watunge na Madiwani. Alisema kuwa baada ya kuvunjwa kwa Baraza la Madiwani Mwaka 2025/2026 Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliendelea na jukumu la kukamilisha ukusanyaji wa mapato kwa kipindi cha mwaka 2024/2025. “Kwa Mwaka huo wa fedha, halmashauri ilikusudia kukusanya shilingi 143,164,202,949.46 na hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2025, ukusanyaji wa mapato ya ndani ulikuwa shilingi 65,042,215,034 sawa na asilimia 104 ya lengo la mwaka na kufanya ukusanyaji wa mapato yote ya halmashauri kuwa shilingi 152,269,204,654 sawa na asilimi...

Diwani Alimwoni Chaula, achaguliwa Meya Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika mkutano wake wa kwanza limemchangua Alimwoni Simon Chaula, Diwani wa Kata ya Makutupora kuwa Mstahiki Meya wa Jiji hilo kwa kupata kura za ndiyo 57 sawa na asilimia 100 ya kura zote zilizopigwa. Akitangaza matokeo ya kura zilizopigwa, Mwenyekiti wa Mkutano wa Halmashauri, Sakina Mbugi alitangaza kuwa Diwani Alimwoni Chaula alipata kura 57 kati ya kura 57 zilizopigwa na wajumbe. “Niwapongeze wajumbe wote halali mlioshiriki kupiga kura kwa nafasi ya Mstahiki Meya na Naibu Meya. Naomba kutanga za matokeo kama ifuatavyo. Nafasi ya Mstahiki Meya, kura 57 zilipigwa, hakuna kura ambayo haikupigwa. Kura zote 57 ni kura za ndiyo. Kwa matokeo hayo, ninamtangaza rasmi Mheshimiwa Alimwoni Chaula kuwa Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma. Nafasi ya Naibu Meya, jumla kura zilizopigwa 55 kati ya kura 57. Wajumbe wawili hawakupiga kura. Kura za ndiyo ni zote 55. Hivyo, ninatangaza rasmi kuwa Mheshimiwa Bakari Fundikira a...

DC Shekimweri asisitiza semina elekezi kwa madiwani Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri amesema kuwa semina elekezi kwa madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni muhimu ili kuwapa maarifa na kufanya uendeshaji wa mikutano ya halmashauri kuwa ya viwango kwa mujibu wa kanuni zilizopo. Kauli hiyo aliitoa alipokuwa akiwasalimia madiwani katika mkutano wa kwanza wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma baada ya Uchanguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani wa tarehe 29 Oktoba, 2025. “Ninawapongeza kwa dhati Mstahiki Meya, Chaula na Naibu Meya, Fundikira kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi na baraza hili. Ninyi bado ni vijana, kwa hiyo baraza hili lina sura ya viongozi wa vijana. Ukiangalia waheshimiwa madiwani wengi pia ni vijana, hapo peke yake ni fursa lakini pia ni changamoto msipoangalia vizuri. Nami niungane na mtoa hoja wa kwanza, kwamba yakaandaliwa mafunzo na kupata semina elekezi ili msheheni maarifa, uelewa wa taratibu za vikao, lakini kanuni za kudumu za Baraza la Madiwani. Kwa sababu katika mkutano...

M/Kiti CCM apewa kongole kuchagua safu makini ya madiwani

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma amepongezwa kwa kupanga safu makini ya wagombea nafasi ya udiwani jambo lililowawezesha kushinda kwa kishindo katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025. Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipotoa salamu katika mkutano wa kwanza wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri. Alhaj Shekimweri alisema “nichukue nafasi hii kuwapongeza waheshimiwa madiwani kwa kuchaguliwa kwa kishindo kuwa madiwani kwa kata zenu, ninyi mnatokana na CCM. Mstahiki Meya, nichukue nafasi hii kumpongeza Mwenyekiti, Charles Mamba kwa kuteua madiwani wazuri waliofanya kampeni zao kistaarabu na kuchaguliwa kwa kishindo kuunda Baraza la Madiwani la Jiji la Dodoma”. Aidha, aliwapongeza wabunge wa Jimbo la Dodoma Mjini na Mtumba kwa kuchaguliwa kuwa wabunge. “Mstahiki Meya, ulikuwa ni Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, nichukue nafasi hii kuwapongeza wabunge wetu...

Waziri Mkuu amtaka Mkandarasi kukamilisha Soko Kuu la Majengo kwa wakati

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt. Mwigulu Nchemba atembelea Soko Kuu la Majengo jijini Dodoma leo kwa ajili ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa soko hilo na kutoa maagizo kwa m kandarasi anayekarabati soko hilo kuhakikisha kazi inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaostahili. Katika ziara hiyo, Waziri Mkuu aliambatana na viongozi wa Mkoa wa Dodoma pamoja na Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambapo alisomewa taarifa ya ukarabati wa miundombinu mbalimbali inayoboreshwa kama vile maeneo ya biashara, mitaro ya maji ya mvua, mifumo ya usalama na umeme. Baada ya taarifa hiyo , Waziri Mkuu alisema kuwa serikali imejipanga kuhakikisha soko linarejea katika matumizi haraka ili kuwezesha wananchi na wafanyabiashara kunufaika na miundombinu bora. “Mradi huu ni muhimu sana kwa wananchi wa Dodoma na lazima ukamilike kwa wakati na kwa kiwango bora. Mkandarasi hakikisha soko hili linakamilika kama ambavyo mkataba unasema. Nanyi jiji naelekeza kuwa soko l...

Kamati za kudumu zatakiwa kuchangia kasi utekelezaji miradi ya maendeleo

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alimtangaza Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Maadili ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuwa ni Omary Omary, Diwani wa Kata ya Makole, aliyepata kura zote tano kutoka kwa wajumbe wa kamati hiyo. Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Omary Omary (kushoto) ambae ni Diwani wa Kata ya Makole. Kulia ni Naibu Meya wa Jiji la Dodoma, Bakari Fundikira ambae pia ni Diwani wa Kata ya Chang'ombe Alisema kuwa kamati hiyo ina jumla ya wajumbe watano ambao ni Omary Omary (Diwani Kata ya Makole), Swalihina Athuman (Diwani Kata ya Viwandani), Charles Ngh’ambi (Diwani Kaya ya Mbalawala), Judith Mushi (Diwani Viti Maalum) na Mwamrisho Kasule (Diwani Viti Maalum). Mstahiki Meya aliwasoma wajumbe wa kamati nyingine kuwa ni Robert Njama, Diwani wa Kata ya Mkonze na Flora Liacho, Diwani wa Viti Maalum kuwa wajumbe wa Kamati ya Mfuko wa Jimbo la Dodoma Mjini. Wengine ni Elis Kitendya, ...

Kamati ya Kudumu Uchumi, Elimu na Afya yapata Jembe!

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA DIWANI wa Viti Maalum, Joan Mazanda aliibuka kidedea kwa kupata kura 15 na kuongoza Kamati ya kudumu ya Uchumi, Elimu na Afya katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Uchumi, Elimu na Afya, Joan Mazanda Akitangaza matokeo hayo, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alisema kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Uchumi, Elimu na Afya ni Joan Mazanda. “Kamati ya kudumu ya Uchumi, Elimu na Afya ilikuwa na wagombea watatu wa nafasi ya mwenyekiti. Matokeo yalikuwa ni kama ifuatavyo. Mheshimiwa Andrew Muholo, Diwani wa Ipala alipata kura tatu; Mheshimiwa Fatuma Zollo, Diwani wa Viti Maalum alipata kura nne na Mheshimiwa Joan Mazanda, Diwani wa Viti Maalum alipata kura 15. Hivyo, mshindi ni Mheshimiwa Joan Mazanda” alisema Chaula. Katika hatua nyingine, Diwani wa Kata ya Madukani, Prof. Davis Mwamfupe alitoa pongezi kwa Diwani Mazanda kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamat...

Diwani Gombo kuongoza Kamati ya Mipango Miji na Mazingira

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Diwani wa Kata ya Ipagala, Gombo Dotto apata ushindi mnono nafasi ya Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Mipango Miji na Mazingira kwa kuibuka na kura 20 akiwaacha kwa mbali wagombea wawili. Akitangaza matokeo ya nafasi ya Mwenyekiti, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula, alisema kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Mipango Miji na Mazingira ni Mheshimiwa Gombo Dotto. “Kamati ya kudumu ya Mipango Miji ilikuwa na wagombea watatu wa nafasi ya mwenyekiti. Mheshimiwa Leonard Ndama, Diwani wa Kata ya Nzuguni alipata kura moja, Mheshimiwa Theobalt Mahina, Diwani wa Kata ya Ntyuka alipata kura moja na Mheshimiwa Gombo Dotto alipata kura 20” alitangaza Mstahiki Meya Chaula. Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri aliwapongeza viongozi wote waliochaguliwa katika nafasi za kamati za kudumu na kuwaasa kutumia nafasi hizo kuhakikisha wanasimami...