Posts

Showing posts from 2025

Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini ni nyenzo ya utendaji kazi serikalini – Dkt. Biteko

Image
Na. Mwandishi Wetu, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, amehitimisha Kongamano la Nne la Kitaifa la Ufuatiliaji, Tathmini na Kujifunza lililofanyika jijini Mwanza akiweka mkazo kuwa mfumo wa ufuatiliaji na tathmini ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha kuwa kila taasisi inatimiza wajibu wake kwa ufanisi na hivyo kufikisha huduma bora kwa wananchi. Kutokana na hilo, Dkt. Biteko amewataka Wataalam wa Ufuatiliaji na Tathmini nchini kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu bila kuogopa kuchukiwa kwani taifa linawategemea ili kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi. “Hakuna mtu au taasisi inayoweza kufanikisha majukumu yake bila kufanya tathmini, ninyi ndio mnaoweza kutambua changamoto mapema na kuzitafutia suluhisho kabla hazijawa kubwa, taasisi yoyote inayokosa mfumo huu inafanana na timu inayoingia uwanjani bila refa..” alisema Dkt. Biteko. Alitoa mfano kuwa katika sekta ya umeme, kabla ya kupeleka huduma hiyo eneo lolote lazima tathmni ifanyike ili kuepuka kurudia...

OCPD yapongeza ushirikiano na Ofisi ya Mashitaka katika zoezi la Urekebu wa Sheria

Image
Na. Calvin Gwabara, DODOMA Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria (OCPD) imekabidhi Juzuu za toleo la Urekebu wa Sheria la Mwaka 2023 kwa Ofisi ya Taifa ya Mashitaka na kupongeza mchango mkubwa uliotolewa na Ofisi hiyo kupitia watumishi wake kwenye utekelezaji wa zoezi la Urekebu.  “Wakati tunaanza zoezi hili Ofisi yetu ilikuwa na changamoto kubwa ya uhaba wa watumishi hasa Mawakili wa kufanya kazi hii lakini tulikuwa tukibisha hodi kwenye Ofisi yako kuomba Mawakili kuja kushirikiana nasi katika kutekeleza zoezi hili, na hakika walitusaidia sana hadi tumekamilisha” alieleza Katuga. Aliongeza “Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria kwa kutambua mchango wenu imeona ni muhimu na Ofisi yako pia ipate nakala hizi ingawa tunatambua kuwa tumeleta chache kutokana na gharama lakini ziwasaidie kwa kuanzia na kuwa kama kumbukumbu kwenu, lakini mnaweza kupata nakala laini zote kupitia mfumo wa OAG MIS library” alieleza Katuga. Kaimu Mkurugenzi huyo wa Divisheni ya Urekebu, Tafiti na Mafunzo ameong...

Ruzuku ya Mil. 250 yatolewa kwa wabunifu wa matumizi ya bora ya Nishati

Image
*Kamishna wa Umeme asema Serikali itaendelea kuwawezesha vijana wabunifu katika teknolojia ya matumizi bora ya nishati  *Wabunifu wa kike wapongezwa kujitokeza kwa wingi matumizi bora ya nishati nchini   Serikali kupitia Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya (EU) na Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP), imetoa ruzuku ya jumla ya shilingi milioni 250 kwa wabunifu kumi waliofanya vizuri katika Mashindano ya Ubunifu na Ufanisi wa Matumizi Bora ya Nishati. Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Innocent Luoga amekabidhi ruzuku hiyo akimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mha. Felchesmi Mramba katika hafla iliyofanyika Septemba 12, 2025 jijini Dar es Salaam.  Hafla hiyo iliwakutanisha wabunifu mbalimbali waliobobea katika nyanja ya ufanisi wa matumizi bora ya nishati katika maeneo matatu ambayo ni ubunifu kwenye vifaa vinavyotumia umeme kidogo, ubunifu kwenye miundombinu ya majengo yanayotumia umeme kidogo pa...

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali yawaasa wahariri wa vyombo vya habari kutumia kalamu kulinda amani ya taifa

Image
Na. Noel Rukanuga, DODOMA Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imewataka wahariri wa vyombo vya habari nchini kutumia kalamu zao kwa uadilifu, kwa kuzingatia maadili ya taaluma na kuhakikisha wanahabarisha umma kwa namna inayolinda amani na usalama wa taifa. Akizungumza wakati akifunga kikao kazi cha siku mbili kati ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wahariri wa vyombo vya habari, kilichofanyika leo Septemba 12, 2025 katika Ukumbi wa Mkemia Mkuu wa Serikali, jijini Dodoma, Mkurugenzi Msaidizi wa Uratibu na Huduma za Ushauri wa Kisheria, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Ipyana Mlilo, amesema kuwa sekta ya habari ni mhimili muhimu katika maendeleo ya taifa, hivyo kikao kazi hicho kimetoa nafasi ya kuimarisha ushirikiano baina ya wahariri na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, ili kuendelea kutoa elimu ya kisheria kwa jamii kwa weledi. “Kikao hiki kimekuwa na manufaa makubwa katika kuhakikisha jamii inapata uelewa mpana kuhusu masuala ya kisheria. Tumejadiliana mambo mengi ...

Madereva wa Serikali wahimizwa kuendesha kwa ustadi, kulinda Usalama barabarani

Image
  Na. Sizah Kangalawe, DODOMA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amewahimiza madereva wa Serikali kutumia vyema mafunzo waliyopatiwa katika kuboresha utendaji kazi wao na kuleta tija zaidi. Alitoa maagizo hayo Septemba 04, 2025 jijini Dodoma wakati akifunga Kongamano la Nne la Chama cha Madereva wa Serikali Tanzania (CMST) lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete. "Naamini mada mlizofundishwa hapa zitakwenda kuboresha uwezo wenu katika utendaji kazi na kuleta tija zaidi katika kuhakikisha mwajiri mkuu ananufaika na mafunzo mliyopata kupitia kongamano hili, na ninaamini kuwa kushiriki kwenu kutapelekea kuendesha magari kwa ustadi na kupunguza matukio ya ajali. Tutajua thamani ya abiria mliowabeba na kuendesha tukiwa tunawakinga na madhara, lakini pia mtajua thamani ya vitu mnavyobeba kupitia magari hayo ambayo mnatakiwa mvisafirishe kwa usalama,” alisema Senyamule. Alifafanua kuwa madereva wa Serikali ni mhimili muhimu katika utekelezaji wa majukumu y...

ACC yatoa vifaa vya Mil. 62 kwa watoto wenye changamoto ya Afya

Image
Na. Sofia Remmi, DODOMA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amepokea na kukabidhi vifaa vya michezo, vya kujifunzia pamoja na vitendea kazi vya watoa huduma za afya ngazi ya Jamii ili viweze kuwafikia walengwa waliopo katika baadhi ya halmashauri za mkoa huu. Hafla hiyo ilifanyika katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jengo la Mkapa. Akizungumza na baadhi ya wadau na watoa huduma ngazi ya jamii amesema Mkoa unashirikiana na Shirika la Action for Community Care (ACC) katika kutekeleza miradi ya Imarisha Afya na ViiV Pediatric Breakthrough Partnership ambayo inalenga kusaidia watoto na vijana wanaoishi na Virusi vya UKIMWI wenye umri wa miaka 0-19. Miradi inawezesha kuwaibua na kuwaunganisha watoto na vijana kwenye matibabu, kuwasaidia kubaki katika huduma na matibabu na kuishi maisha yenye afya. “Vifaa vya  michezo na vya kujifunzia vinavyopokelewa leo vina umuhimu wa kipekee kwa kuwa  vitawezesha uchangamshi na ukuaji wa ubongo wa watoto na kuwa...

Halmashauri ya Jiji la Dodoma Yatoa Mafunzo ya Malisho ya Mifugo

Image
Na. Rehema Kiyumbi, DODOMA Afisa Mifugo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma Leonia Msuya ameendelea kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji namna ya kulisha na kutunza mifugo yao kwa maendeleo ya kiuchumi.   Aliyasema hayo wakati akiwa katika vipando vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika maadhimisho ya kimataifa Nanenane. ’’Tumejiandaa kutoa elimu na kuonesha maonesho ya malisho ambayo ni chakula cha mifugo kwa sababu yamepanuka sana wananchi na wahamiaji wamekuwa wengi ambapo kusababisha malisho kupungua. Kwa mwaka huu tumeandaa vipando vitatu ambavyo ni malisho ya mikunde, nyasi na magugu (sumu) ambapo huchanganywa ili ng’ombe kupata virutubisho ambavyo ni protini, mafuta na wanga kama sisi binadamu,” alisema Msuya. Alisema kuwa aina ya malisho ambayo ni sumu huchangia kutoa elimu kwa wakulima na ni moja ya kutunza mazingira. ’’Sumu ni aina ya malisho kama mihogo na nyanya tumefanya makusudi ili mkulima na mfugaji kuweza kuyaondoa kwenye shamba lake. Pia, mkulima na mfugaji ...

RC Dodoma apongeza wafugaji kwa ushiriki wa Paredi ya Mifugo

Image
Na. Veronica John, DODOMA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule awapongeza wafugaji kwa kujitokeza kwa wingi katika shindano la Paredi ya Mifugo Kitaifa 2025 ambalo hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 1-8 Agosti. Akizungumza na wafugaji, Senyamule alisema kuwa ameshuhudia mabadiliko na maboresho makubwa katika shughuli za mifugo ambapo hapo awali ilifanyika kikanda na sasa yameenda kimataifa. Alisema kuwa mashindano hayo kufanyika sehemu nyingi duniani yakiwa na lengo la kutambua mchango na juhudi za wafugaji katika kuchangia maendeleo ya taifa na ya mtu mmoja mmoja. “Maonesho haya huongeza ari kwa wananchi katika kuinua hadhi ya uzalishaji na tija kwa kutumia teknolojia mpya zilizoboreshwa katika shughuli za ufugaji ili kukidhi mahitaji ya soko. Na nimearifiwa kuwa maonesho na mashindano haya yaliasisiwa na Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2010 katika siku ya kilele cha sherehe za maonesho ya Nanenane Dodoma” a...

Elimu ya utunzaji zao la Zabibu yawafikia wananchi Jiji la Dodoma

Image
Na. Veronica, NANENANE DODOMA   Afisa Kilimo Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Emanuel Mayyo ametoa elimu juu ya utunzaji wa kilimo cha zabibu kuanzia upandaji hadi uvunaji ili kiwe na tija kwa wakulima. Hayo aliyasema katika viwanja vya maonesho ya Nanenane wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea vipando bustani vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa kuna umuhimu wa kulima zao la zabibu kwasababu ni zao lenye faida katika sekta ya biashara na kuwakwamua kiuchumi wananchi wa Jiji la Dodoma. “Zao la zabibu ni zao mama hapa Dodoma na ni zao ambalo linafaida kubwa kwa wakulima. Hivyo, kuna haja ya wale wakulima ambao wanahitaji kulima zao hili kujifunza na kutambua hatua zote za zao hili kuanzia upandaji hadi uvunaji ili kupata zao bora,” alisema Mayyo. Pia aliongeza kusema kuwa kuna mpango wa kuweka mkataba na baadhi ya makampuni ili wananchi wa Jiji la Dodoma waweze kupata soko la zao hilo. “Vilevile, tuna mpango madhubuti kwa wale wakulima ...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa Pamoja na viongozi mbalimbali kabla ya kuaga mwili wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Job Yustino Ndugai katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma tarehe 10 Agosti, 2025

Image
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha Maombolezo mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma kwa ajili ya kuongoza waombolezaji kuaga mwili wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Job Yustino Ndugai tarehe 10 Agosti, 2025

Image
 

Zao la Zukini na faida lukuki

Image
Na. Rehema Kiyumbi, DODOMA Afisa Kilimo Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Nkunde Kimweri amesema kuwa zao la zukini ni zao lenye vitamini ambalo hutumika kama kiungo cha mboga ili kuleta ladha na kiafya hutumika kupunguza shinikizo la damu. Alisema kuwa zao la zukini ni jepesi kupanda na lina matokeo mazuri. ’’Tulitumia mbolea na dawa kutoka Kampuni ya Fomi kuzia na baadae tukatumia Fomi nenepesha ilipoanza kutoa maua. Pia tulitumia dawa ya 40-44 kutoka Kampuni ya Jumbo kudhibiti wadudu na kuhakikisha usalama na ubora wa zao letu, lakini pia tunamshukuru Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa kutuletea vitu muhimu katika kukuza mazao yetu na hatujapata changamoto yoyote hadi hapa tulipofikia,” alisema Kimweri. Alimalizia kwa kuwashauri vijana walio jumbani wakati wakisubiri ajira wajikite katika kilimo ili kujipatia kipato. ’’Tunawashauri vijana wachukue mikopo inayotolewa na halmashauri ili wajikite katika kilimo na kujikwamua kiuchumi katika maisha yao na kama tunavyofahamu kilimo kinamto...

Zao la Nyanyachungu na Bilinganya linafaida kwa jamii

Image
Na. Rehema Kiyumbi, DODOMA Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Nkunde Kimweri    ametoa elimu kuhusiana na zao la nyanyachungu na bilinganya kwa kuanisha uandaaji, matumizi sahihi ya mbolea na matumizi ya dawa ya kudhibiti wadudu wanaoathiri zao hilo kwa lengo la kukuza uchumi kwa wafanyabiashara na matumizi ya nyumbani. Akizungumza na mwanahabari katika vipando vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa wa mazao hayo hasa kwa wafanyabiashara. “Tulianza kwa kuandaa shamba la zao la bilinganya aina ya ‘black beauty’ na nyanyachungu aina ya ‘tengeru white’ kwa umbali wa sentimita 60 kwa sentimita 60 ili kuwezesha mmea kuweza kujitanua na kukua kwa uhuru na tulitumia mbolea kutoka Kampuni ya Yara ambapo ni Yara oteshi, na Yara kuzia wakati wa kukuzia mmea wetu na tukatumia dawa viwatilifu kwa kuulia wadudu wanaoshambulia kwa kasi sana zao hili,” alisema Kimweri.   Naye, msimamizi wa bustani Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Milton Edwa...

IAA Tawi la Dodoma kuendelea kulea wataalam kwa vitendo

Image
Na. Alex Sonna, DODOMA CHUO cha Uhasibu Arusha (IAA) – Tawi la Dodoma, kimeendelea kuwa kinara katika kutoa elimu ya vitendo kwa vijana nchini, tangu kuanzishwa kwake mwaka 2021 kwa kuanza na programu tatu za diploma. Akizungumza katika banda la Chuo hicho katika Maonesho ya Kitaifa ya Wakulima (NaneNane) yanayoendelea katika Uwanja wa Nzuguni, jijini Dodoma, Meneja wa tawi hilo, Dkt. Grace Temba, alisema kuwa chuo hicho ni sehemu ya mtandao wa kitaaluma unaojumuisha kampasi mama iliyopo Dar es Salaam, pamoja na matawi mengine yaliyopo Babati, Songea, Bukombe, Arusha, na Dodoma yenyewe. “Tunapokea wanafunzi kuanzia ngazi ya kidato cha nne ambao husoma kwa miaka mitatu, wakijifunza kupitia mitalaa ya kisasa inayolenga kuwaandaa kwa soko la ajira la sasa na la baadaye,” alisema, Dkt. Temba. Kwa sasa, IAA inatoa jumla ya programu 38 katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na Uhasibu, Usimamizi wa Fedha, Uhasibu wa Kodi, Uongozi na Utawala wa Biashara, Masoko, na Usimamizi wa Ununuz...

Rais Samia: Tumieni kikamilifu Miundombinu, Teknolojia na mitaji iliyowekezwa katika Kilimo, Uvuvi na Mifugo

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi, Wizara na Taasisi zinazohusika na sekta za kilimo, mifugo na uvuvi kutumia kikamilifu miundombinu, teknolojia na mitaji iliyowekezwa na Serikali ili kuongeza tija na ushindani wa Taifa katika masoko ya ndani na nje. Akizungumza katika kilele cha Maonesho na Sherehe za wakulima, wafugaji na wavuvi (Nanenane) zilizofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nzuguni, Rais Dkt. Samia amesema miradi ya umwagiliaji iliyokamilika na inayoendelea kutekelezwa inapaswa kusimamiwa kwa viwango bora ili kuongeza eneo la kilimo cha umwagiliaji na kukuza tija ya mavuno. Alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeongeza bajeti ya kilimo ili kugharamia ujenzi na ukarabati wa skimu za umwagiliaji, mabwawa na visima, pamoja na kuanzisha mashamba makubwa ya pamoja, huku upatikanaji wa mbegu bora na mbolea ya kisasa ukiimarika kupitia ruzuku na kuanzishwa kwa viwanda vya uzalishaji, hatua iliyo...

Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Atembelea Maonesho ya Nanenane 2025 Jijini Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Salim Msangi, atembelea banda la TCAA pamoja na mabanda mengine kadhaa katika Maonesho ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma. Ziara hii ililenga kuonyesha huduma zinazotolewa na TCAA na kuhamasisha umma kuhusu masuala ya usafiri wa anga. Katika ziara hiyo, Msangi alionesha kuridhishwa na namna TCAA inavyotoa huduma na elimu kwa wananchi, hasa kuhusu usalama wa anga, matumizi salama ya ndege zisizo na rubani (ndege nyuki), na fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya usafiri wa anga. Alieleza kuwa huduma zinazotolewa na TCAA zinachangia pakubwa katika kuimarisha usalama na maendeleo ya sekta hiyo. Vilevile, alifurahishwa na ushirikiano wa watumishi wa TCAA katika kuelimisha umma, akiwapongeza kwa kujituma na kuendelea kutoa taarifa muhimu kwa wananchi kuhusu masuala ya usafiri wa anga. Alisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana na wadau wengine katik...

Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu yafungua Masoko ya Nje kwa Wafanyabiashara nchini

Image
Na. Calvin Gwabara, DODOMA Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) imewezesha Tanzania kuondolewa vikwazo vya kiubora iliyowekewa kwenye masoko mbalimbali duniani na hivyo kusaidia wakulima wa Tanzania kunufaika na uuzaji wa mazao nje ya nchi. Hayo yalibainishwa na mtaalamu wa afya ya mimea kutoka TPHPA, Dorah Amur wakati akimueleza Balozi wa Tanzania nchini Italia, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipotembela banda la TPHPA kwenye maonesho ya wakulima Nanenane kitaifa Jijini Dodoma kuhusu mafanikio na jitihada zinazofanywa na Taasisi hiyo katika kuhakikisha ubora wa mazao na kufungua masoko. “Wakulima wa wafanya biashara wa Tanzania wamekuwa wakiuza bidhaa zao kwenye masoko mbalimbali ya kimataifa duniani lakini kuna baadhi ya masoko yalizuia Tanzania kuingiza bidhaa zetu kutokana na sababu mbalimbali za kiubora lakini TPHPA ikaalifanyia kazi haraka kwa kufanya uchunguzi wa kina na kuwasilisha kwenye mamlaka za masoko hayo na kufanikiwa kuondolewa kwa zuio hilo ...

Manaibu Makatibu Wakuu OR TAMISEMI Watembelea Banda la TARURA

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Manaibu Makatibu Wakuu wa Ofisi ya Rais - TAMISEMI wakiongozwa na Mhandisi Rogatus Mativila Naibu Katibu Mkuu (Miundombinu), Sospeter Mtwale - Naibu Katibu Mkuu (TAMISEMI) na Prof. Tumaini Nagu - Naibu Katibu Mkuu (Afya) wametembea Banda la Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) katika kilele cha Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima NaneNane katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.   Makatibu Wakuu hao walipatiwa maelezo mbalimbali kutoka kwa wataalamu wa TARURA wakiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano, Catherine Sungura kuhusu majukumu, utekelezaji wa miradi mbalimbali pamoja na mipango ya TARURA inayohusu uboreshaji na ujenzi wa miundombinu ya barabara nchini.    Akizungumza kwa niaba ya wenzake Naibu Katibu Mkuu, Sospeter Mtwale amewapongeza TARURA kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kufungua barabara hususan maeneo ya wakulima, wavuvi na wafugaji na hivyo kuwarahisishia kusafirisha mazao yao.   Pia ...