Posts

Showing posts from 2025

Mikopo ya asilimia 10 yawang’arisha wajasiriamali Makutupora

Image
Na. Nancy Kivuyo, MAKUTUPORA Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupitia utoaji wa mikopo ya asilimia 10 yanufaisha makundi ya wanawake katika kujikwamua kiuchumi katika Kata ya Makutupora ikitajwa kuwa chachu ya kuinua maendeleo katika sekta ya kilimo, ufugaji na ujasiriamali. Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na makundi ya wanawake waliopata mikopo ya asilimia 10 katika Kata ya Makutupora, Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Makutupora, Andrew Boma alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kusimamia vema uwezeshaji wa wananchi kupata haki zao hasa kwa makundi maalum ambayo yamewezeshwa kupitia mikopo hiyo. “Sisi Kata ya Makutupora vikundi 20 vimepatiwa mkopo wa jumla ya shilingi 230,000,000. Vikundi vya wanawake ni 10, vijana saba na watu wenye ulemavu vitatu. Mpaka sasa wameweza kurejesha shilingi 159, 980,000 na bakaa inaendelea kulipwa na vikundi hivyo” alisema Boma. Aliongeza kuwa vikundi hivyo vinajishughulisha na shughuli mbalimbali kama...

Kata ya Makutupora, kinara wa timu za michezo na ngoma za asili

Image
Na. Nancy Kivuyo, MAKUTUPORA Kata ya Makutupora yapongeza juhudi za serikali ya awamu ya sita za kuboresha miundombinu ya michezo jambo iliyopelekea hamasa kwa wananchi kupenda kushiriki katika michezo kwaajili ya kuibua vipaji na kuboresha afya zao. Pongezi hizo zilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Matukupora Hamis Jigwa mbele ya waandishi wa habari waliofanya mazungumzo nae baada ya kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Alisema kuwa kwenye sekta ya michezo Kata ya Makutupora ina vikundi vya ngoma za asili ambavyo vimekuwa vikishiriki kwenye upokeaji wa Mwenge wa Uhuru na kushiriki mikutano ya kitaifa pamoja na timu za mpira wa miguu. “Hapa katani kwetu tupo vizuri, wananchi wa kata hii wanapenda michezo sana. Hata hii leo kuna mashindano yanaendelea, kama mtapata muda mtaona jinsi wananchi wa hapa wanavyojitokeza kwa wingi kushiriki katika michezo” alisema Jigwa. Akiongelea chachu ya hamasa ya michezo, alimtaja Rais, Dkt. Samia ...

Zabibu Hoteli Dodoma yajikita matumizi ya Nishati safi

Image
Na. Mussa Richard, TAMBUKARELI Kampeni ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhakikisha taasisi na sehemu zenye mkusanyiko wa watu zaidi ya 100 kutumia nishati safi ya kupikia, imepokelewa na kufanyiwa kazi ipasavyo na uongozi wa Zabibu Hoteli, iliyopo Kata ya Tambukareli jijini Dodoma. Hayo yamebainishwa na Meneja Mkuu wa Zabibu Hoteli, Mathew Gabriel, wakati akizungumza na vyombo vya Habari baada ya kutembelea hoteli hiyo ili kujionea matumizi ya nishati safi katika hoteli hiyo. “Zabibu Hoteli ni miongoni mwa taasisi ambayo imejizatiti kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia kwenye kila nyanja inayohusu mapishi. Nishati safi ya kupikia ni nzuri na ina faida nyingi kulinganisha na nishati zingine zinazochangia kwenye uchafuzi wa mazingira. Kwahiyo, niziombe sekta zote na watu binafsi wajikite katika matumizi ya nishati safi za kupikia kwasababu ni rahisi na salama” alisema Gabriel. Nae, Focus Mwenda, Mpishi Mkuu wa Zabibu Hoteli, alimshukur...

Wananchi Tambukareli wafurahia barabara miaka minne ya Rais Samia

Image
Na. Mussa Richard, TAMBUKARELI Diwani wa Kata ya Tambukareli jijini Dodoma, Juma Michael, amesema kuwa ndani ya miaka minne ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amejenga barabara ya kiwango cha lami inayoanzia ‘ Shoppers’ hadi Kituo Kikuu cha Mabasi Dodoma kwa lengo la kupunguza msongamano na kurahisisha huduma ya usafiri. Diwani Michael, alisema hayo baada ya kutembelewa na waandishi wa habari ofisini kwake kwa lengo la kujionea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa kwenye Kata ya Tambukareli kwa kipindi cha miaka minne ya uongozi wa awamu ya sita chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan. “Kipindi cha nyuma tulikuwa na changamoto ya barabara, lakini tunaishukuru sana serikali imeweza kusikia kilio chetu na kuweza kutujengea barabara yenye kiwango cha lami. Barabara ambayo imekuja kuwa mkombozi kwa wafanyabiashara, wajasiriamali na wananchi kwa ujumla, kwasababu hapo awali wafanyabiashara walikuwa wana shindwa jinsi ya kufikisha bidhaa katika ...

Bado siku 18 Mwenge wa Uhuru uingie Jiji la Dodoma

Image
 

Kheri ya Kumbukizi ya Karume

Image
 

Zimebaki Siku 19 Kupokea Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma

Image
 

Global Affairs Canada yafurahishwa na utekelezaji wa Mradi wa AHADI katika Kata ya Chamwino

Image
  Kata ya Chamwino, imepokea ugeni kutoka Global Affairs Canada ukiongozwa na Mary Harasym aliyeambatana na Zahra Popatia ambao ni wafadhili wa mradi wa AHADI na kueleza kuridhishwa na utekelezaji wa mradi huo. Lengo la ziara hiyo ni kufanya tathimini na kujionea kwa macho namna mradi unavyotekelezwa hususan utoaji wa elimu kuhusu maswala ya Afya ya uzazi kwa vijana wa Kata ya Chamwino. Kwa upande ‘Promoter’ wa mradi, Khadija Ally alitoa maelezo ya kina kuhusu shughuli zinazofanyika na mafanikio yaliyopatikana kwa vijana kushiriki kwenye mafunzo yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kuhusu maswala Afya ya uzazi, kujikinga dhidi ya mimba zisizotarajiwa na kuwa na mipango bora ya maisha ya baadae pamoja na kuwajengea uwezo wa kuwa na shughuli za kuingiza kipato. Afisa Mtendaji wa Kata ya Chamwino, kwa niaba ya Diwani aliwashukuru wageni hao kwa kuitembelea Kata ya Chamwino na kusema kuwa mradi wa AHADI ni kielelezo kizuri cha ushirikiano baina ya kata yake...

Agenda ya Lishe yaongeza Ari ya usomaji S/M Dodoma Makulu

Image
Na. Abdul Iddi, DODOMA MAKULU Shule ya Msingi Dodoma Makulu imeshukuru agenda ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya lishe shuleni kwa sababu inawaongezea ari ya kusoma na kupata matokeo yanayokusudiwa. Shukrani hiyo ilitolewa na Mwalimu wa Lishe, Rehema Kalinga alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari waliotembelea shule ya msingi Dodoma makulu kujionea hali ya lishe kwa wanafunzi shuleni hapo. Alisema kuwa shule yake inazingatia ajenda ya Lishe kwa kuwapa wanafunzi wote kuanzi awali mpaka darasa la Saba uji. Darasa la Nne na la Saba kupata chakula cha mchana. “Toka ajenda hii kuanza kutekelezwa, tumeanza kuona matokeo Chanya. Kwanza kwakupunguza utoro, pia watoto darasani wanafundishika” alisema Mwl. Kalinga. Aidha, alitoa pongezi kwa wazazi kwa kusikiliza ajenda ya Lishe na kuitekeleza bila kusuasua kwasababu waliweza kutoa mchango kwa kiasi walicho kubaliana na kamati ya wazazi wa shule hiyo. “Muitikio ni mkubwa kwasababu watoto wote katika Shule ya Dodoma Makulu wanapata uji ...

Kata ya Ipala ipo mstari wa mbele katika Michezo

Image
Na. Nancy Kivuyo, IPALA Hamasa ya serikali katika michezo nchini ni kichocheo cha wananchi wa Kata ya Ipala kupenda kushiriki michezo ya aina mbalimbali kwa ajili ya kujenga na kuboresha afya zao ili waweze kushiriki katika shughuli za maendeleo. Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu nafasi ya michezo katika Kata ya Ipala walipotembelea kata hiyo. Diwani Magawa alisema kuwa serikali imekuwa inafanya hamasa kubwa katika michezo hali iliyopelekea kata yao kuwa na mwamko mkubwa katika kushiriki mashindano mbalimbali yanayoandaliwa katani hapo. “Kwakweli, mambo ya michezo tunaenda nayo vizuri, kila mwaka tunafanya mashindano yanayoitwa ‘Magawa Cup’ ambayo diwani ndiye mimi na kwa kushirikiana na mheshimiwa mbunge tuna ‘Mavunde Cup’, tunaandaa mashindano hayo ili kuwasogeza wananchi karibu zaidi na michezo. Wakati mwingine tunaunganisha michezo na kampeni za kijamii za serika...

Umeme wa REA chachu ya viwanda vidogo vidogo Kata ya Ipala

Image
Na. John Masanja, IPALA Awamu ya kwanza ya umeme wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umechochea shughuli za maendeleo na kuinua uchumi wa wananchi katika Kata ya Ipala, Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ‘media tour’ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika kata hiyo kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Alisema kuwa serikali ya awamu ya sita imepeleka huduma ya umeme katika Kata ya Ipala. “Kata yetu imefikiwa na awamu ya kwanza ambayo ina faida nyingi sana. Wananchi wanafanya shughuli mbalimbali zinazojumuisha matumizi ya umeme kwa kiwango kikubwa na naamini kwa siku za usoni hapa kwetu kutakuwa mtaa wa viwanda vya aina tofauti” alisema Magawa. Nae mkazi wa Kata ya Ipala, Mathias Masita aliishukuru serikali kwa kuwapelekea umeme kwasababu maisha yao yamebadilika na wanafanya shughuli zinazohusisha umeme kwa kiwango kikubwa. “Mradi wa REA umetunufaisha s...

Usipange kukosa kukimbia na Mbunge wako

Image
 

Serikali yatoa fedha kujenga Kituo cha Jemolojia ili kuongea thamani ya Madini

Image
Na. Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba amesema kuwa katika kuhakikisha Madini yanaongezewa thamani kabla ya kupelekwa nje ya nchi, Serikali imetoa fedha nyingi na kujenga Kituo kikubwa cha Jemolojia ili kuwa na kituo bora, chenye mashine bora na wataalam bora nchi nzima ili kuhakikisha Madini hasa ya vito yanaongezewa thamani hapa nchini kwa viwango vinavyohitajika kabla ya kusafirisha kwenda nje. Mhandisi Samamba aliyasema hayo jijini Dodoma katika hafla fupi ya utiaji saini wa makubaliano kati ya Kampuni Sun Set kutoka Tailand na Taasisi ya Jemolojia Tanzania iliyoko chini ya Wizara ya Madini. Alisema kuwa watahakikisha kwamba wanaweka utaratibu wa namna ambavyo makubaliano hayo yatatekelezwa ili pande zote mbili waweze kunufaika na makubaliano hayo. “Kupitia Kituo chetu chetu cha TGC, Mheshimiwa Rais ameweka fedha nyingi, tumejenga jengo kubwa kabisa ambacho ni kituo kikubwa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla ambapo lengo...

Waziri Mavunde asisitiza miradi mikubwa ya madini iliyopewa leseni kuanza kazi haraka

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, ameagiza miradi mikubwa na ya kati ya Madini ambayo tayari imekwishapewa leseni kuanza utekelezaji wake mara moja ili kuchochea ukuaji wa sekta na kuleta manufaa kwa taifa na kutimiza azma ya serikali kutoa leseni hizo. Waziri wa Madini, Anthony Mavunde Aliyasema jijini Dodoma wakati akizungumza katika mkutano maalum na Chemba ya Migodi Tanzania (TCM) kwa lengo kujadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya Madini ili kuboresha uendelezaji na usimamizi wa shughuli za uchimbaji na biashara ya Madini kwa manufaa ya sekta na taifa kwa ujumla. Waziri Mavunde alisema serikali inataka kuhakikisha kuwa miradi yote ya uchimbaji Madini iliyopangwa kuanza inaanza mara moja bila kucheleweshwa, na kuwa serikali kwa upande wake imejitahidi kurahisisha taratibu kwa wawekezaji na sasa ni wakati wa sekta binafsi kuchukua hatua kwa upande wao. “Serikali imefanya kazi yake, tumeondoa vikwazo vingi na kurahisisha utaratibu. Sasa ni juku...

Shule shikizi Ipala, mkombozi kwa wanafunzi wanaotembea umbali mrefu

Image
Na. John Masanja, IPALA Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa, aishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu ya elimu msingi katika kata hiyo kwa kujenga shule shikizi ili kutengeneza mazingira rafiki kwa wanafunzi wenye umri mdogo kupata elimu bora. Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa Aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ‘media tour’ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika Kata ya Ipala kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Diwani Magawa alisema kuwa katika miaka minne ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita, elimu katika Kata ya Ipala imekuwa kwa kasi. “Serikali yetu tukufu imetuletea elimu hadi kwenye kata yetu. Tuna shule shiziki mbili zimeanzishwa kwa lengo la kusaidia wanafunzi wadogo wanaotembea umbali mrefu karibu kilomita tano kufuata elimu. Sasa hivi uwepo wa madarasa haya matatu nafuu imekuwa kubwa sana kwa kuwapunguzia watoto wadogo kutembea umbari mrefu” ...

Nyumba ya mtumishi kuchangia huduma masaa 24 Zahanati ya Ipala

Image
Na. Nancy Kivuyo, IPALA Mradi wa ujenzi wa nyumba ya mtumishi katika Zahanati ya Ipala uliogharimu kiasi cha shilingi 55,000,000, umeleta maboresho katika utoaji wa huduma ya afya katika kata hiyo. Nyumba ya Mtumishi Zahanati ya Ipala Hayo yalielezwa na Muuguzi kutoka Zahanati ya Ipala, Tumain Sanga alipokuwa akiwaelezea waandishi wa habari waliofanya ‘media tour’ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika kata hiyo kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Alisema kuwa anatoa pongezi kwa serikali kuwajengea nyumba hiyo ili kurahisisha utoaji wa huduma za afya katika kata hiyo. “Tunaipongeza serikali kutujengea nyumba ya mtumishi, uwepo wa nyumba hii imeturahisishia kutendaji wa kazi mzuri. Laiti tungekuwa mbali tungeshindwa kuwahudumia wananchi vizuri na kwa wakati, lakini sasa wagonjwa wanaweza kuja muda wowote na wakatukuta na tukawahudumia kwa masaa 24. Tunaishukuru sana serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tuna...

Wananchi wa Mtaa wa Mwaja, Jiji la Dodoma washiriki kufanya usafi wa mazingira wa Jumamosi ya mwisho wa Mwezi, Machi, 2025

Image
Leo tarehe 29.03.2025, wananchi wa Mtaa wa Mwaja, Kata ya Chamwino, Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshiriki zoezi la usafi wa Mazingira wa kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kwa lengo la kuweza mazingira safi kwa ajili ya afya zao. Usafi huo uliongozwa na Mwenyekiti wa Mtaa wa Mwaja, Athumani Makuka ambaye aliambatana na Afisa Mtendaji wa Mtaa, Mwanaasha Mani. Zoezi hilo la usafi lilifanyika katika mtaro unaopita pembezoni mwa Shule ya Msingi Chinangali ambao umehusisha kuzibua mtaro wenye urefu wa mita 100 sambamba na kutoa taka ngumu kama makopo na mifuko kwenye mtaro huo ili kuruhusu maji yaliyotuwama kwa sababu ya mvua kutiririka pasina kizuizi chochote.

Ukarabati tanki la Maji Kata ya Ipala waleta neema kwa wananchi

Image
Na. John Masanja, IPALA Ukarabati mradi wa tanki la maji la Lita 90,000 katika Kata ya Ipala, waleta ahueni kwa wananchi na kuwapunguzia adha ya kutembea umbali mrefu kufuata maji kwa matumizi mbalimbali. Akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ‘media tour’ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika Kata ya Ipala kuanzia mwaka 2021 hadi 2025, Diwani George Magawa aliishukuru serikali kwa kutoa fedha shilingi 43,406,300 kwaajili ya ukarabati wa tanki la mradi mkubwa wa Maji Ipala. “Wananchi sasa wanapata maji safi na salama. Kwahiyo, tunaishukuru serikali, tunamshukuru sana mbunge wetu na wataalam mbalimbali. Kata imechimba visima vinne kwaajili ya kupata maji safi na kupunguzia wananchi adha ya kutumia maji yasiyo salama. Hivi visima vinapunguza adha ya kwenda umbali mrefu kufuata maji ambayo mara nyingi siyo salama. Hivyo, wananchi wa kata yetu tatizo hili la uhaba wa maji limepungua sana” alisema Magawa. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Maji Hombo...

Mikopo ya 10% yawanufaisha vijana wa Kata ya Ipala

Image
Na. John Masanja, IPALA Halmashauri ya Jiji la Dodoma yakipatia kikundi cha Kazi iendelee Ipala mkopo usio na riba wa shilingi 17,000,000 kwa ajili ya kuongeza mtaji kwa shughuli ya bodaboda na kutengeneza ajira kwa vijana ili waweze kujitegemea kimaisha. Hayo yalielezwa na Mhasibu wa Kikundi cha Kazi iendelee, Peter Mhaka mbele ya waandishi wa habari waliofanya ‘media tour’ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika kata hiyo kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. “Kikundi kilipata mkopo huu ili kujikwamua kiuchumi. Mwaka 2023 tulichukua mkopo wa shilingi 17,000,000 tukiwa watano, tukanunua bodaboda tano ambazo zimetunufaisha kwa kusomesha watoto, tumejiingiza kwenye kilimo na tumepunguza utegemezi yote hii ili kujikwamua zaidi kiuchumi” alisema Mhaka. Aidha, aliiomba serikali kuendelea kuhamasisha vijana ili wafahamu umuhimu wa mikopo hiyo. “Nawashauri vijana wenzangu wachangamkie fursa ya mikopo hii isiyoumiza, watembelee ofisi za kata ili kupata elimu ya mikopo h...

Shule shikizi Ipala, mkombozi kwa wanafunzi wanaotembea umbali mrefu

Image
Na. John Masanja, IPALA Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa, aishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu ya elimu msingi katika kata hiyo kwa kujenga shule shikizi ili kutengeneza mazingira rafiki kwa wanafunzi wenye umri mdogo kupata elimu bora. Aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ‘media tour’ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika Kata ya Ipala kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Diwani Magawa alisema kuwa katika miaka minne ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita, elimu katika Kata ya Ipala imekuwa kwa kasi. “Serikali yetu tukufu imetuletea elimu hadi kwenye kata yetu. Tuna shule shiziki mbili zimeanzishwa kwa lengo la kusaidia wanafunzi wadogo wanaotembea umbali mrefu karibu kilomita tano kufuata elimu. Sasa hivi uwepo wa madarasa haya matatu nafuu imekuwa kubwa sana kwa kuwapunguzia watoto wadogo kutembea umbari mrefu” alisema Magawa. Pia, aliongeza kuwa...

Zaidi ya Shilingi Bil 1 zaijenga Kata ya Matumbulu

Image
 

Shilingi Bil. 2.5 zaiboresha Kata ya Makole

Image