Posts

Showing posts from 2025

Dodoma Jiji FC, Fiti Kuwavaa Wajelajela

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, imejiandaa kuwakabili Klabu ya soka ya Tanzania Prisons katika muendelezo wa mbilinge mbilinge za duru ya pili ya Ligi kuu ya NBC Tanzania bara hapo kesho katika dimba la Jamhuri Dodoma. Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa Tanzania Prisons, Kocha Mkuu wa Dodoma Jiji FC,   Meck Mekisime alisema “Timu ipo tayari na tumejiandaa vizuri tukijua kuwa mchezo utakua mgumu kwasababu wapinzani wetu wametoka kupoteza michezo miwili mfululizo. Kwahiyo, sisi kama klabu tupo tayari kupambana na kuhakikisha alama tatu zinabaki Dodoma na niwaombe mashabiki na wanadodoma kwa ujumla kesho waje kwa wingi uwanjani kuja kuwaunga mkono wachezaji na kuwafariji kutokana na kile kilichotokea siku kadhaa zilizopita, jambo ambalo litawaongezea nguvu wachezaji kuipambania timu huku wakijua kuna namba kubwa ya watu jukwaani inawaunga mkono”. Nae, Augustin Nsata, Nahodha wa klabu ya Dodoma Jiji FC, akaelezea hali y...

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Na. Halima Majidi, DODOMA Wananchi wa Kata ya Makutupora, jijini Dodoma, wameeleza kilio chao juu ya changamoto kubwa zinazowakabili, zikiwemo ukosefu wa maji safi, matatizo ya umeme, pamoja na shule kuwa mbali, hali inayowakwamisha katika shughuli za kila siku. Wakizungumza katika mkutano wa mkuu wa mkoa uliofanyika katika Kata ya Makutupora, baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamesema wamekuwa wakikumbana na shida ya maji kwa muda mrefu, huku wakilazimika kutembea umbali mrefu kutafuta huduma hiyo muhimu. Akitoa kero hiyo, mkazi wa Mtaa wa Sekondari, Pasisi James, alisema kuwa, tangu kuhamia katika mtaa huo ni miaka mingi hivyo ameiomba serikali kuwasogezea huduma ya maji kwa sababu imekuwa ni changamoto kubwa na hivyo kushindwa kuendelea na kazi zao za kila siku. “Maji ni tatizo hapa kwetu, tunamiaka mingi tangu kuhamia hapa, nimekuja hata kusoma sijui mpaka leo bado tunahangaikia maji, tunachukua maji kwa wachina dumu moja hilo hilo ufulie pamoja na kunywa, hapo naomba mtusaidie” ...

Senyamule awasisitiza wanufaika wa TASAF kutumia pesa kujiletea maendeleo

Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amewataka wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kutumia vizuri pesa wanayopewa na mfuko huo katika kufanyia shughuli mbalimbali za kuingiza kipato ili kujikwamua kiuchumi na kuondokana na dhana ya kuwa tegemezi katika jamii na taifa kwa ujumla. Aliyasema hayo wakati akiwa kwenye ziara fupi ya kutembelea wanufaika wa Mfuko wa TASAF katika mtaa wa Mchemwa, Kata ya Makutupora, jijini Dodoma iliyokwenda na Kaulimbiu isemayo ‘TASAF, kwa pamoja tuondoe umaskini’. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, alisema kuwa miongoni mwa malengo ya TASAF ni kuhakikisha wanajamii wenye kipato cha chini wanainuka kiuchumi na kuwa na kipato cha juu ili kusaidia kuinua vipato vyao na familia zao kwa ujumla. “Mfuko wa TASAF umekuja ili kuwafanya wale wenye kipato cha chini kuongezeka na kuanza kupata kipato cha juu” alisema Senyamule. Katika hatua nyingine, aliwahimiza wanufaika wa mfuko huo kuipa thamani pesa hiyo kwa kufan...

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma

Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Greyson Msigwa, amesema mradi wa ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu Dodoma, utakaoweza kubeba watu 32,000 ambao utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 352 fedha za kitanzania, unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 24, chini ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aliyasema hayo katika hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu Dodoma, uliohusisha wizara hiyo na Kampuni ya Lemonta SPA, iliofanyika kiwanja cha Changamani, Kata ya Nzuguni, jijini Dodoma. Akizungumza kuhusu lengo la ujenzi wa uwanja huo, Msigwa alisema, mradi huo ni fursa kwa maendeleo ya michezo kwa wakazi wa Jiji la Dodoma kwasababu uwanja huo utatumika katika mashindano mbalimbali kitaifa na kimataifa ili kuhakikisha sekta ya michezo inazidi kukua. “Mradi huu ni fursa kwa maendeleo ya wakazi wa Dodoma lakini ni fursa kubwa kwa wanamichezo katika kukuza vipaji vyao, na sisi kama wizara tumejip...

Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo Dodoma watarajia makubwa Mradi wa TACTIC

Image
Na. Halima Majidi, DODOMA Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo Jiji la Dodoma,   wameishukuru serikali kwa kuona umuhimu wa kukarabati miundombinu ya Soko hilo na kuomba   kuharakishwa uboreshaji wa soko ili waweze kuendelea na majukumu yao,   kwa sababu soko hilo ndio soko mama la chakula. Akizungumza katika hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Ujenzi wa Miradi ya TACTIC uliofanyika katika Bustani ya Chinangali Park, Mfanyabiashara wa   Soko Kuu   la Majengo, Rhoda Boyi, alipongeza juhudi za   Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuwashirikisha   katika hatua zote za mradi "Tunatarajia kuwa sauti zetu zitasikilizwa na kuzingatiwa ili kuhakikisha kuwa maboresho haya yanakidhi mahitaji yetu na kuboresha mazingira ya biashara" alisema Boyi. Kwa upande wake   Mohammedi,   alifafanua changamoto watakazokumbana nazo   katika kipindi chote cha ukarabati wa jengo hilo, ni pamoja na; kupoteza wateja, kuharibika kwa bidhaa kutokana na kuhamishw...

Wakandarasi Wasiomaliza Miradi Mashakani

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA TARURA imeagizwa kuwasimamisha wakandarasi wasiokamilisha miradi kwa wakati na wasipewe tena miradi hiyo kwasababu wanakwamisha juhudi za Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati na ya kimaendeleo nchini. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa (Mb) Hayo yalisemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa (Mb) alipokuwa akizungumza na wataalam kutoka taasisi mbalimbali za kiserikali pamoja na wananchi wa Jiji la Dodoma katika Hafla ya utiaji saini mkataba wa uboreshaji Soko Kuu la Majengo pamoja na ujenzi wa Kituo cha Daladala eneo la Mshikamano, Kizota na Nzuguni, uliofanyika tarehe 06 Februari, 2025 katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. “Maelekezo yangu kwa TARURA, mkandarasi huyu asiruhusiwe kufanya kazi yoyote chini ya TARURA kuanzia sasa mpaka akamilishe mradi huu tunaoukusudia. Nenden...

Miundombinu ni nyenzo ya maendeleo ya Jiji la Dodoma

Image
Na. Shahanazi Subeti, DODOMA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) pamoja na   Halmashauri ya Jiji la Dodoma zilisaini mkataba wa TACTIC   wenye thamani ya shilingi Bilioni 14.2 kwa lengo la kuboresha miundombinu, kuimarisha usimamizi wa uendelezaji miji na kuboresha mazingira ya uwekezaji ili kukuza uchumi wa halmashauri ya jiji. Hafla hiyo ya Utiaji saini ilifanyika bustani ya Chinangali Park jijini Dodoma katika hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa soko kuu la majengo pamoja na ujenzi wa kituo cha daladala eneo la Mshikamano, Kizota na Nzuguni. Akielezea tukio hilo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa alisema, mikataba hii itakwenda kuleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi kwa watanzania wanaoishi Dodoma na aliwaomba wakandarasi kutekeleza majukumu yao kwa wakati. "Tunapoboresha miundombinu hii itawafanya watanzania na wafanyabiashara, kuweza kusogeza biashara zao karibu, kuweza kutum...

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Image
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa (Mb), aliwapongeza watumishi wa umma kwa kusimamia miradi mbalimbali jijini Dodoma ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Aliyasema hayo katika Hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa Soko Kuu la Majengo pamoja ujenzi wa kituo cha daladala eneo la Mshikamano, Kizota na Nzuguni, iliyofanyika kiwanja cha Chinangali Park, Jijini Dodoma. Akizungumzia kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali Mohamed Mchengerwa, alitaka wakandarasi wote ambao hawajatekeleza majukumu yao katika miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa ujenzi wa barabara, kutopewa   fursa ya kufanya kazi yoyote   ikiwa ni onyo kwa wale wote wanaofanya kazi kwa uzembe na kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa wakati. "Maelekezo yangu kwa mtendaji mkuu na katibu mkuu wa TARURA, Mkandarasi huyu asiruhusiwe kufanya kazi yoyote chini ya TA...

Wananchi washuhudia utiaji saini mkataba wa mradi wa TACTIC

Image
Na. Coletha Charles, DODOMA Wananchi wa Jiji la Dodoma wamejitokeza kwa wingi kushuhudia hafla ya utiaji saini mkataba wa Mradi wa “Tanzania Cities Transforming Infrastructure and Competitiveness” (TACTIC), unaolenga kuboresha na kujenga miundombinu muhimu katika jiji hilo ikiwa ni pamoja na Uboreshaji wa Ujenzi wa Soko, Vituo vya daladala pamoja na vivuko. Hafla hiyo, iliyofanyika katika viwanja vya Chinangali, inahusisha uboreshaji wa Soko Kuu la Majengo, Kituo cha Daladala Mshikamano, Stendi ya mabasi madogo eneo la Kizota, ujenzi wa stendi ya mabasi madogo eneo la Nzuguni, pamoja na ujenzi wa vivuko katika maeneo ya Chadulu, Mailimbili, na Ntyuka. Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mgeni Rasmi ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa (Mb), aliwaomba watanzania kuitunza miradi hiyo inayotekelezwa kwenye majiji na miji zaidi ya 45 kwasababu ina thamani kubwa zaidi ya Trilioni 1.1. Alisema kuwa mkataba huo wa bilioni 14.2 wa kuboresha na kujenga m...

Miaka 48 ya CCM Uwanja wa Jamhuri, Dodoma

Image