Posts

Showing posts from 2025

Halmashauri ya Jiji la Dodoma Yatoa Mafunzo ya Malisho ya Mifugo

Image
Na. Rehema Kiyumbi, DODOMA Afisa Mifugo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma Leonia Msuya ameendelea kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji namna ya kulisha na kutunza mifugo yao kwa maendeleo ya kiuchumi.   Aliyasema hayo wakati akiwa katika vipando vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika maadhimisho ya kimataifa Nanenane. ’’Tumejiandaa kutoa elimu na kuonesha maonesho ya malisho ambayo ni chakula cha mifugo kwa sababu yamepanuka sana wananchi na wahamiaji wamekuwa wengi ambapo kusababisha malisho kupungua. Kwa mwaka huu tumeandaa vipando vitatu ambavyo ni malisho ya mikunde, nyasi na magugu (sumu) ambapo huchanganywa ili ng’ombe kupata virutubisho ambavyo ni protini, mafuta na wanga kama sisi binadamu,” alisema Msuya. Alisema kuwa aina ya malisho ambayo ni sumu huchangia kutoa elimu kwa wakulima na ni moja ya kutunza mazingira. ’’Sumu ni aina ya malisho kama mihogo na nyanya tumefanya makusudi ili mkulima na mfugaji kuweza kuyaondoa kwenye shamba lake. Pia, mkulima na mfugaji ...

RC Dodoma apongeza wafugaji kwa ushiriki wa Paredi ya Mifugo

Image
Na. Veronica John, DODOMA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule awapongeza wafugaji kwa kujitokeza kwa wingi katika shindano la Paredi ya Mifugo Kitaifa 2025 ambalo hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 1-8 Agosti. Akizungumza na wafugaji, Senyamule alisema kuwa ameshuhudia mabadiliko na maboresho makubwa katika shughuli za mifugo ambapo hapo awali ilifanyika kikanda na sasa yameenda kimataifa. Alisema kuwa mashindano hayo kufanyika sehemu nyingi duniani yakiwa na lengo la kutambua mchango na juhudi za wafugaji katika kuchangia maendeleo ya taifa na ya mtu mmoja mmoja. “Maonesho haya huongeza ari kwa wananchi katika kuinua hadhi ya uzalishaji na tija kwa kutumia teknolojia mpya zilizoboreshwa katika shughuli za ufugaji ili kukidhi mahitaji ya soko. Na nimearifiwa kuwa maonesho na mashindano haya yaliasisiwa na Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2010 katika siku ya kilele cha sherehe za maonesho ya Nanenane Dodoma” a...

Elimu ya utunzaji zao la Zabibu yawafikia wananchi Jiji la Dodoma

Image
Na. Veronica, NANENANE DODOMA   Afisa Kilimo Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Emanuel Mayyo ametoa elimu juu ya utunzaji wa kilimo cha zabibu kuanzia upandaji hadi uvunaji ili kiwe na tija kwa wakulima. Hayo aliyasema katika viwanja vya maonesho ya Nanenane wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea vipando bustani vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa kuna umuhimu wa kulima zao la zabibu kwasababu ni zao lenye faida katika sekta ya biashara na kuwakwamua kiuchumi wananchi wa Jiji la Dodoma. “Zao la zabibu ni zao mama hapa Dodoma na ni zao ambalo linafaida kubwa kwa wakulima. Hivyo, kuna haja ya wale wakulima ambao wanahitaji kulima zao hili kujifunza na kutambua hatua zote za zao hili kuanzia upandaji hadi uvunaji ili kupata zao bora,” alisema Mayyo. Pia aliongeza kusema kuwa kuna mpango wa kuweka mkataba na baadhi ya makampuni ili wananchi wa Jiji la Dodoma waweze kupata soko la zao hilo. “Vilevile, tuna mpango madhubuti kwa wale wakulima ...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa Pamoja na viongozi mbalimbali kabla ya kuaga mwili wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Job Yustino Ndugai katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma tarehe 10 Agosti, 2025

Image
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha Maombolezo mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma kwa ajili ya kuongoza waombolezaji kuaga mwili wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Job Yustino Ndugai tarehe 10 Agosti, 2025

Image
 

Zao la Zukini na faida lukuki

Image
Na. Rehema Kiyumbi, DODOMA Afisa Kilimo Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Nkunde Kimweri amesema kuwa zao la zukini ni zao lenye vitamini ambalo hutumika kama kiungo cha mboga ili kuleta ladha na kiafya hutumika kupunguza shinikizo la damu. Alisema kuwa zao la zukini ni jepesi kupanda na lina matokeo mazuri. ’’Tulitumia mbolea na dawa kutoka Kampuni ya Fomi kuzia na baadae tukatumia Fomi nenepesha ilipoanza kutoa maua. Pia tulitumia dawa ya 40-44 kutoka Kampuni ya Jumbo kudhibiti wadudu na kuhakikisha usalama na ubora wa zao letu, lakini pia tunamshukuru Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa kutuletea vitu muhimu katika kukuza mazao yetu na hatujapata changamoto yoyote hadi hapa tulipofikia,” alisema Kimweri. Alimalizia kwa kuwashauri vijana walio jumbani wakati wakisubiri ajira wajikite katika kilimo ili kujipatia kipato. ’’Tunawashauri vijana wachukue mikopo inayotolewa na halmashauri ili wajikite katika kilimo na kujikwamua kiuchumi katika maisha yao na kama tunavyofahamu kilimo kinamto...

Zao la Nyanyachungu na Bilinganya linafaida kwa jamii

Image
Na. Rehema Kiyumbi, DODOMA Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Nkunde Kimweri    ametoa elimu kuhusiana na zao la nyanyachungu na bilinganya kwa kuanisha uandaaji, matumizi sahihi ya mbolea na matumizi ya dawa ya kudhibiti wadudu wanaoathiri zao hilo kwa lengo la kukuza uchumi kwa wafanyabiashara na matumizi ya nyumbani. Akizungumza na mwanahabari katika vipando vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa wa mazao hayo hasa kwa wafanyabiashara. “Tulianza kwa kuandaa shamba la zao la bilinganya aina ya ‘black beauty’ na nyanyachungu aina ya ‘tengeru white’ kwa umbali wa sentimita 60 kwa sentimita 60 ili kuwezesha mmea kuweza kujitanua na kukua kwa uhuru na tulitumia mbolea kutoka Kampuni ya Yara ambapo ni Yara oteshi, na Yara kuzia wakati wa kukuzia mmea wetu na tukatumia dawa viwatilifu kwa kuulia wadudu wanaoshambulia kwa kasi sana zao hili,” alisema Kimweri.   Naye, msimamizi wa bustani Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Milton Edwa...

IAA Tawi la Dodoma kuendelea kulea wataalam kwa vitendo

Image
Na. Alex Sonna, DODOMA CHUO cha Uhasibu Arusha (IAA) – Tawi la Dodoma, kimeendelea kuwa kinara katika kutoa elimu ya vitendo kwa vijana nchini, tangu kuanzishwa kwake mwaka 2021 kwa kuanza na programu tatu za diploma. Akizungumza katika banda la Chuo hicho katika Maonesho ya Kitaifa ya Wakulima (NaneNane) yanayoendelea katika Uwanja wa Nzuguni, jijini Dodoma, Meneja wa tawi hilo, Dkt. Grace Temba, alisema kuwa chuo hicho ni sehemu ya mtandao wa kitaaluma unaojumuisha kampasi mama iliyopo Dar es Salaam, pamoja na matawi mengine yaliyopo Babati, Songea, Bukombe, Arusha, na Dodoma yenyewe. “Tunapokea wanafunzi kuanzia ngazi ya kidato cha nne ambao husoma kwa miaka mitatu, wakijifunza kupitia mitalaa ya kisasa inayolenga kuwaandaa kwa soko la ajira la sasa na la baadaye,” alisema, Dkt. Temba. Kwa sasa, IAA inatoa jumla ya programu 38 katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na Uhasibu, Usimamizi wa Fedha, Uhasibu wa Kodi, Uongozi na Utawala wa Biashara, Masoko, na Usimamizi wa Ununuz...

Rais Samia: Tumieni kikamilifu Miundombinu, Teknolojia na mitaji iliyowekezwa katika Kilimo, Uvuvi na Mifugo

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi, Wizara na Taasisi zinazohusika na sekta za kilimo, mifugo na uvuvi kutumia kikamilifu miundombinu, teknolojia na mitaji iliyowekezwa na Serikali ili kuongeza tija na ushindani wa Taifa katika masoko ya ndani na nje. Akizungumza katika kilele cha Maonesho na Sherehe za wakulima, wafugaji na wavuvi (Nanenane) zilizofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nzuguni, Rais Dkt. Samia amesema miradi ya umwagiliaji iliyokamilika na inayoendelea kutekelezwa inapaswa kusimamiwa kwa viwango bora ili kuongeza eneo la kilimo cha umwagiliaji na kukuza tija ya mavuno. Alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeongeza bajeti ya kilimo ili kugharamia ujenzi na ukarabati wa skimu za umwagiliaji, mabwawa na visima, pamoja na kuanzisha mashamba makubwa ya pamoja, huku upatikanaji wa mbegu bora na mbolea ya kisasa ukiimarika kupitia ruzuku na kuanzishwa kwa viwanda vya uzalishaji, hatua iliyo...

Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Atembelea Maonesho ya Nanenane 2025 Jijini Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Salim Msangi, atembelea banda la TCAA pamoja na mabanda mengine kadhaa katika Maonesho ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma. Ziara hii ililenga kuonyesha huduma zinazotolewa na TCAA na kuhamasisha umma kuhusu masuala ya usafiri wa anga. Katika ziara hiyo, Msangi alionesha kuridhishwa na namna TCAA inavyotoa huduma na elimu kwa wananchi, hasa kuhusu usalama wa anga, matumizi salama ya ndege zisizo na rubani (ndege nyuki), na fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya usafiri wa anga. Alieleza kuwa huduma zinazotolewa na TCAA zinachangia pakubwa katika kuimarisha usalama na maendeleo ya sekta hiyo. Vilevile, alifurahishwa na ushirikiano wa watumishi wa TCAA katika kuelimisha umma, akiwapongeza kwa kujituma na kuendelea kutoa taarifa muhimu kwa wananchi kuhusu masuala ya usafiri wa anga. Alisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana na wadau wengine katik...

Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu yafungua Masoko ya Nje kwa Wafanyabiashara nchini

Image
Na. Calvin Gwabara, DODOMA Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) imewezesha Tanzania kuondolewa vikwazo vya kiubora iliyowekewa kwenye masoko mbalimbali duniani na hivyo kusaidia wakulima wa Tanzania kunufaika na uuzaji wa mazao nje ya nchi. Hayo yalibainishwa na mtaalamu wa afya ya mimea kutoka TPHPA, Dorah Amur wakati akimueleza Balozi wa Tanzania nchini Italia, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipotembela banda la TPHPA kwenye maonesho ya wakulima Nanenane kitaifa Jijini Dodoma kuhusu mafanikio na jitihada zinazofanywa na Taasisi hiyo katika kuhakikisha ubora wa mazao na kufungua masoko. “Wakulima wa wafanya biashara wa Tanzania wamekuwa wakiuza bidhaa zao kwenye masoko mbalimbali ya kimataifa duniani lakini kuna baadhi ya masoko yalizuia Tanzania kuingiza bidhaa zetu kutokana na sababu mbalimbali za kiubora lakini TPHPA ikaalifanyia kazi haraka kwa kufanya uchunguzi wa kina na kuwasilisha kwenye mamlaka za masoko hayo na kufanikiwa kuondolewa kwa zuio hilo ...

Manaibu Makatibu Wakuu OR TAMISEMI Watembelea Banda la TARURA

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Manaibu Makatibu Wakuu wa Ofisi ya Rais - TAMISEMI wakiongozwa na Mhandisi Rogatus Mativila Naibu Katibu Mkuu (Miundombinu), Sospeter Mtwale - Naibu Katibu Mkuu (TAMISEMI) na Prof. Tumaini Nagu - Naibu Katibu Mkuu (Afya) wametembea Banda la Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) katika kilele cha Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima NaneNane katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.   Makatibu Wakuu hao walipatiwa maelezo mbalimbali kutoka kwa wataalamu wa TARURA wakiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano, Catherine Sungura kuhusu majukumu, utekelezaji wa miradi mbalimbali pamoja na mipango ya TARURA inayohusu uboreshaji na ujenzi wa miundombinu ya barabara nchini.    Akizungumza kwa niaba ya wenzake Naibu Katibu Mkuu, Sospeter Mtwale amewapongeza TARURA kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kufungua barabara hususan maeneo ya wakulima, wavuvi na wafugaji na hivyo kuwarahisishia kusafirisha mazao yao.   Pia ...

Pinda ataka matokeo ya Utafiti yazingatiwe kueleza faidia za Kisanyansi katika bidhaa za Kilimo

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Waziri Mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda ametaka Utaalamu wa Kisanyansi uzingatiwe katika mnyororo mzima wa thamani wa sekta ya Kilimo ikiwa ni pamoja na kuzingatia ufafanuzi wa Kisanyansi katika chapa za bidhaa mbalimbali za Kilimo zilizoongezewa thamani ili kuonesha tija inayopatikana kwa mtumiaji wa bidhaa hizo. Mhe. Pinda alisema hayo alipotembelea Banda la Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kwenye Maonesho ya kimataifa ya Kilimo maarufu kama Nanenane yanayoendelea viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma ambapo TARI inashiriki ikiwa na Teknolojia mbalimbali za Kilimo. Akitolea mfano wa Korosho iliyoongezewa thamani na TARI Mhe. Pinda alieleza kufuraishwa na ufafanuzi wa kitaalamu uliopo katika mfuko wa Korosho hizo unaotoa maelezo ya Kisanyansi kumtosheleza mtumiaji kutambua tija anayopata kutokana na matumizi ya bidhaa hiyo zaidi ya kuishia kusema ni tamu yenye ladha nzuri kitu ambacho amesema kinanyima fursa zai...

Bustani inayohamishika mbombozi kwa wenye maeneo haba ya Kilimo

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Mafunzo yanayotolewa katika vyuo vya VETA yanalenga kuleta utatuzi wa changamoto mbalimbali katika jamii. Watu wengi wanaoishi katika maeneo ya mijini wamekuwa na maeneo finyu kwa ajili ya kilimo, hali hiyo ikampelekea Mwl. Gema Ngoo wa Chuo cha VETA Kihonda, kubuni bustani ya mbogamboga inayohamishika. Akizungumza katika Maonesho ya Kitaifa ya Kilimo (Nanenane), yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma Mwl. Ngoo ambaye anafundisha Fani ya Ufundi wa Zana za Kilimo alisema ubunifu huo wa bustani inayohamishika ni mahkususi kwa wale watu wanaoishi katika nyumba za kupanga, nyumba zenye maeneo finyu au zilizosakafiwa kote, hivyo kupelekea kukosa sehemu ya kupanda mbogamboga. “Ubunifu huu utawasaidia wengi wenye maeneo finyu kwaajili ya kupanda mbogamboga, tunashauri watu walime kilimo cha aina hii kwani hakiharibu mazingira lakinini pia kilimo hiki utatumia mbolea ya asili ambayo ni salama kwa afya za binadamu” alisema Mwl. Ngoo. Mwalimu G...

VETA yapongezwa kutoa mafunzo kwa wanawake na Samia

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imepongezwa kwa kuendelea kutoa  mafunzo ya ufundi stadi  kupitia Mpango wa mafunzo unaotekelezwa na  Taasisi ya Wanawake na Samia .   Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa  Dodoma , Rosemary Senyamule  ambae ndie muasisi wa Taasisi hiyo, alipotembelea  banda la VETA  lililopo katika viwanja vya Maonesho ya Kitaifa ya Kilimo (Nanenane),  Nzuguni , jijini Dodoma na kuongea na wahitimu wa mafunzo hayo wanaoonesha bidhaa mbalimbali walizotengeneza baada ya kupata mafunzo kutika vyuo vya VETA.   “Tunafahamu fika kwamba Mhe. Rais wa Jamhuri wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania , Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa akihimiza utoaji wa mafunzo ya ufundi stadi kwa makundi maalum wakiwepo wanawake. Naipongeza VETA kwa kuendelea kuunga mkono juhudi hizo kwa kuwa tunaona matokeo yake kupitia bidhaa na bunifu mbalimbali zinazofanywa na wanawake hapa Dodoma n...

Mtaji Benki ya TADB wafikia Bil. 442

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwekeza katika uwezeshaji wakulima kwa kuwapatia mikopo ya Pembejeo. Akitoa maelezo kwa Mhe. Rais Samia kuhusu utendaji wa Benki hiyo leo Agosti 8,2025 wakati wa maadhimisho ya kilele cha Nanenane kitaifa, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Frank Nyabundege alisema kuwa mtaji wa Benki hiyo umekuwa kutoka shilingi bilioni 60 hadi bilioni 442. “Benki yetu itaendelea kudhamini maonesho ya NnNe Nane kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo kwa sababu imeiwezesha kuwa na mtaji mkubwa” alisisitiza Nyabundege. Mgeni rasmi katika maonesho ya Nanenane Kitaifa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.  

Waziri Mkuu Mstaafu, Pinda atembelea NSSF, Maonesho ya Nanenane Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda ametembelea Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Ofisi hiyo pamoja na Taasisi zake ikiwemo NSSF. Maonesho ya Nanenane 2025 Kitaifa yanaendelea katika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma ambapo kilele chake ni tarehe 8 Agosti 2025.   Akitoa maelezo mbele ya Mhe. Pinda, Meneja wa NSSF Mkoa wa Dodoma, Yahya Mudhihir, alieleza namna ambavyo NSSF imeboresha utoaji wa huduma kwa kutumia mifumo ya kidijitali, hatua inayolenga kuongeza ufanisi, uwazi na kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wanachama na wadau.   Alisema kuwa mwanachama anaweza kupata huduma mbalimbali zinazotolewa na NSSF bila kulazimika kufika ofisini, ikiwemo, usajili wa wanachama wapya kupitia mfumo ya kidijitali, uwasilishaji na ukusanyaji wa michango ya waajiri na wanachama na kulipa mafao mbalimbali.   Aliongeza kuwa NSSF inashiriki maonesho haya kwa lengo la ...

Mtendaji Mkuu WMA atembelea Maonesho ya Nanenane Dodoma

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Alban Kihulla, leo Agosti 8, 2025 ametembelea Maonesho ya Nanenane kitaifa, katika uwanja wa Nzuguni jijini Dodoma. Akiwa katika Banda la WMA, Afisa Mtendaji Mkuu aliwapongeza watumishi wa Wakala kwa kazi nzuri ya kuelimisha umma ambayo wamekuwa wakiifanya tangu kuanza kwa Maonesho hayo. Aliwataka kuendelea kutoa elimu ya vipimo kwa jamii hata baada ya Maonesho ili wananchi waelewe ni kwa namna gani Serikali kupitia WMA inawalinda kwa kuhakikisha vipimo vinavyotumika katika sekta mbalimbali ni sahihi na vinatumika kwa usahihi. “Tuendelee kutumia majukwaa mbalimbali kutoa elimu ya vipimo kwa wananchi ili waelewe haki yao ya kupata huduma kwa vipimo sahihi lakini pia na wajibu wao wa kuhakikisha wanatumia vipimo sahihi katika sekta mbalimbali” alisema Kihulla. Vilevile, alitembelea mabanda mengine mbalimbali likiwemo banda la Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na Taasisi zake ili kujionea huduma zinazot...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea Maabara Kuu ya Kisasa ya Kilimo iliyopo Mtumba jijini Dodoma

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea Maabara Kuu ya Kisasa ya Kilimo iliyopo Mtumba jijini Dodoma