Kamati ya Kudumu Uchumi, Elimu na Afya yapata Jembe!

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

DIWANI wa Viti Maalum, Joan Mazanda aliibuka kidedea kwa kupata kura 15 na kuongoza Kamati ya kudumu ya Uchumi, Elimu na Afya katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.


Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Uchumi, Elimu na Afya, Joan Mazanda

Akitangaza matokeo hayo, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alisema kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Uchumi, Elimu na Afya ni Joan Mazanda. “Kamati ya kudumu ya Uchumi, Elimu na Afya ilikuwa na wagombea watatu wa nafasi ya mwenyekiti. Matokeo yalikuwa ni kama ifuatavyo. Mheshimiwa Andrew Muholo, Diwani wa Ipala alipata kura tatu; Mheshimiwa Fatuma Zollo, Diwani wa Viti Maalum alipata kura nne na Mheshimiwa Joan Mazanda, Diwani wa Viti Maalum alipata kura 15. Hivyo, mshindi ni Mheshimiwa Joan Mazanda” alisema Chaula.

Katika hatua nyingine, Diwani wa Kata ya Madukani, Prof. Davis Mwamfupe alitoa pongezi kwa Diwani Mazanda kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Uchumi, Elimu na Afya. “Nampongeza sana kwa nafasi hiyo aliyochaguliwa kwa kura nyingi zaidi, ni imani yangu kuwa atawajibika kwa weledi mkubwa katika kuhakikisha upatikanaji wa miundombinu bora ya elimu na afya inastawi na kuwapa wananchi huduma bora. Lakini pia, eneo la uchumi sina shaka nalo nina amini atalisimamia kikamilifu” alipongeza.

Nae, Diwani wa Kata ya Mtumba, Ringo Iringo alieleza furaha yake baada ya baraza kuundwa na kamati za kudumu kupata viongozi wenye weledi. “Sasa tunaenda kuwatumikia wananchi wa majimbo yetu mawili yaani Dodoma Mjini na Mtumba. Viongozi wenzangu tuwaunge mkono waliochaguliwa katika nafasi zote ili kazi ya kuwatumikia wananchi ifanikiwe” alieleza.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Agenda ya Lishe yaongeza Ari ya usomaji S/M Dodoma Makulu

Diwani Gombo kuongoza Kamati ya Mipango Miji na Mazingira