Kamati za kudumu zatakiwa kuchangia kasi utekelezaji miradi ya maendeleo

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alimtangaza Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Maadili ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuwa ni Omary Omary, Diwani wa Kata ya Makole, aliyepata kura zote tano kutoka kwa wajumbe wa kamati hiyo.


Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Omary Omary (kushoto) ambae ni Diwani wa Kata ya Makole. Kulia ni Naibu Meya wa Jiji la Dodoma, Bakari Fundikira ambae pia ni Diwani wa Kata ya Chang'ombe

Alisema kuwa kamati hiyo ina jumla ya wajumbe watano ambao ni Omary Omary (Diwani Kata ya Makole), Swalihina Athuman (Diwani Kata ya Viwandani), Charles Ngh’ambi (Diwani Kaya ya Mbalawala), Judith Mushi (Diwani Viti Maalum) na Mwamrisho Kasule (Diwani Viti Maalum).

Mstahiki Meya aliwasoma wajumbe wa kamati nyingine kuwa ni Robert Njama, Diwani wa Kata ya Mkonze na Flora Liacho, Diwani wa Viti Maalum kuwa wajumbe wa Kamati ya Mfuko wa Jimbo la Dodoma Mjini. Wengine ni Elis Kitendya, Diwani Kata ya Chihanga na Emmanuel Manyono, Diwani Kata ya Kikombo kuwa wajumbe wa Kamati ya Mfuko wa Jimbo la Mtumba.

Kwa upande wa Bodi ya Ajira, alimtangaza Leonard Ndama, Diwani wa Kata ya Nzuguni na Samson Mkopi, Diwani wa Kata ya Dodoma Makulu kuwa Mjumbe wa Bodi ya Vileo.

Akitangaza wajumbe wa Kamati ya Kugawa Ardhi, aliwataja kuwa ni Mugendi Kerenge, Diwani wa Kata ya Mnadani na Asma Karama, Diwani Viti Maalum. “Kamati ya ALAT Mkoa itakuwa na Edward Magawa Diwani wa Kata ya Ihumwa na Leticia Sanga, Diwani Viti Maalum” alisema Chaula.

Nae, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Dodoma, Charles Mamba aliwapongeza madiwani hao kwa kula kiapo na kwa kuchaguliwa katika kamati mbalimbali za kudumu. “Mimi sina mengi ya kusema, nawapongeza kwa hatua hii. Sasa mkafanye kazi kwa weledi na kwa ushirikiano mkubwa. Hizi kamati zinasaidia kufuatilia kwa ukaribu utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa maana hiyo ni imani yangu kuwa mtashauri na kufuatilia pale inapotakikana” alipongeza Mamba.

MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Kamati ya Kudumu Uchumi, Elimu na Afya yapata Jembe!

Agenda ya Lishe yaongeza Ari ya usomaji S/M Dodoma Makulu

Diwani Gombo kuongoza Kamati ya Mipango Miji na Mazingira