Posts

Showing posts from April, 2025

Bado siku 18 Mwenge wa Uhuru uingie Jiji la Dodoma

Image
 

Kheri ya Kumbukizi ya Karume

Image
 

Zimebaki Siku 19 Kupokea Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma

Image
 

Global Affairs Canada yafurahishwa na utekelezaji wa Mradi wa AHADI katika Kata ya Chamwino

Image
  Kata ya Chamwino, imepokea ugeni kutoka Global Affairs Canada ukiongozwa na Mary Harasym aliyeambatana na Zahra Popatia ambao ni wafadhili wa mradi wa AHADI na kueleza kuridhishwa na utekelezaji wa mradi huo. Lengo la ziara hiyo ni kufanya tathimini na kujionea kwa macho namna mradi unavyotekelezwa hususan utoaji wa elimu kuhusu maswala ya Afya ya uzazi kwa vijana wa Kata ya Chamwino. Kwa upande ā€˜Promoterā€™ wa mradi, Khadija Ally alitoa maelezo ya kina kuhusu shughuli zinazofanyika na mafanikio yaliyopatikana kwa vijana kushiriki kwenye mafunzo yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kuhusu maswala Afya ya uzazi, kujikinga dhidi ya mimba zisizotarajiwa na kuwa na mipango bora ya maisha ya baadae pamoja na kuwajengea uwezo wa kuwa na shughuli za kuingiza kipato. Afisa Mtendaji wa Kata ya Chamwino, kwa niaba ya Diwani aliwashukuru wageni hao kwa kuitembelea Kata ya Chamwino na kusema kuwa mradi wa AHADI ni kielelezo kizuri cha ushirikiano baina ya kata yake...

Agenda ya Lishe yaongeza Ari ya usomaji S/M Dodoma Makulu

Image
Na. Abdul Iddi, DODOMA MAKULU Shule ya Msingi Dodoma Makulu imeshukuru agenda ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya lishe shuleni kwa sababu inawaongezea ari ya kusoma na kupata matokeo yanayokusudiwa. Shukrani hiyo ilitolewa na Mwalimu wa Lishe, Rehema Kalinga alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari waliotembelea shule ya msingi Dodoma makulu kujionea hali ya lishe kwa wanafunzi shuleni hapo. Alisema kuwa shule yake inazingatia ajenda ya Lishe kwa kuwapa wanafunzi wote kuanzi awali mpaka darasa la Saba uji. Darasa la Nne na la Saba kupata chakula cha mchana. ā€œToka ajenda hii kuanza kutekelezwa, tumeanza kuona matokeo Chanya. Kwanza kwakupunguza utoro, pia watoto darasani wanafundishikaā€ alisema Mwl. Kalinga. Aidha, alitoa pongezi kwa wazazi kwa kusikiliza ajenda ya Lishe na kuitekeleza bila kusuasua kwasababu waliweza kutoa mchango kwa kiasi walicho kubaliana na kamati ya wazazi wa shule hiyo. ā€œMuitikio ni mkubwa kwasababu watoto wote katika Shule ya Dodoma Makulu wanapata uji ...

Kata ya Ipala ipo mstari wa mbele katika Michezo

Image
Na. Nancy Kivuyo, IPALA Hamasa ya serikali katika michezo nchini ni kichocheo cha wananchi wa Kata ya Ipala kupenda kushiriki michezo ya aina mbalimbali kwa ajili ya kujenga na kuboresha afya zao ili waweze kushiriki katika shughuli za maendeleo. Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu nafasi ya michezo katika Kata ya Ipala walipotembelea kata hiyo. Diwani Magawa alisema kuwa serikali imekuwa inafanya hamasa kubwa katika michezo hali iliyopelekea kata yao kuwa na mwamko mkubwa katika kushiriki mashindano mbalimbali yanayoandaliwa katani hapo. ā€œKwakweli, mambo ya michezo tunaenda nayo vizuri, kila mwaka tunafanya mashindano yanayoitwa ā€˜Magawa Cupā€™ ambayo diwani ndiye mimi na kwa kushirikiana na mheshimiwa mbunge tuna ā€˜Mavunde Cupā€™, tunaandaa mashindano hayo ili kuwasogeza wananchi karibu zaidi na michezo. Wakati mwingine tunaunganisha michezo na kampeni za kijamii za serika...

Umeme wa REA chachu ya viwanda vidogo vidogo Kata ya Ipala

Image
Na. John Masanja, IPALA Awamu ya kwanza ya umeme wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umechochea shughuli za maendeleo na kuinua uchumi wa wananchi katika Kata ya Ipala, Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ā€˜media tourā€™ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika kata hiyo kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Alisema kuwa serikali ya awamu ya sita imepeleka huduma ya umeme katika Kata ya Ipala. ā€œKata yetu imefikiwa na awamu ya kwanza ambayo ina faida nyingi sana. Wananchi wanafanya shughuli mbalimbali zinazojumuisha matumizi ya umeme kwa kiwango kikubwa na naamini kwa siku za usoni hapa kwetu kutakuwa mtaa wa viwanda vya aina tofautiā€ alisema Magawa. Nae mkazi wa Kata ya Ipala, Mathias Masita aliishukuru serikali kwa kuwapelekea umeme kwasababu maisha yao yamebadilika na wanafanya shughuli zinazohusisha umeme kwa kiwango kikubwa. ā€œMradi wa REA umetunufaisha s...

Usipange kukosa kukimbia na Mbunge wako

Image
 

Serikali yatoa fedha kujenga Kituo cha Jemolojia ili kuongea thamani ya Madini

Image
Na. Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba amesema kuwa katika kuhakikisha Madini yanaongezewa thamani kabla ya kupelekwa nje ya nchi, Serikali imetoa fedha nyingi na kujenga Kituo kikubwa cha Jemolojia ili kuwa na kituo bora, chenye mashine bora na wataalam bora nchi nzima ili kuhakikisha Madini hasa ya vito yanaongezewa thamani hapa nchini kwa viwango vinavyohitajika kabla ya kusafirisha kwenda nje. Mhandisi Samamba aliyasema hayo jijini Dodoma katika hafla fupi ya utiaji saini wa makubaliano kati ya Kampuni Sun Set kutoka Tailand na Taasisi ya Jemolojia Tanzania iliyoko chini ya Wizara ya Madini. Alisema kuwa watahakikisha kwamba wanaweka utaratibu wa namna ambavyo makubaliano hayo yatatekelezwa ili pande zote mbili waweze kunufaika na makubaliano hayo. ā€œKupitia Kituo chetu chetu cha TGC, Mheshimiwa Rais ameweka fedha nyingi, tumejenga jengo kubwa kabisa ambacho ni kituo kikubwa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla ambapo lengo...