Posts

Showing posts from April, 2025

‘Team Aprili’ wapanda miti Shule ya Msingi Mahungu kusherehekea siku yao ya kuzaliwa

Image
Na. Nancy Kivuyo, KIZOTA Watumishi kutoka taasisi mbalimbali za Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamejumuika pamoja kusherehekea mwezi wa kuzaliwa kwa kupanda miti katika Shule ya Msingi Mahungu. Wakitoa hisia zao za furaha walipotembelea shule hiyo mpya, watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma akiwemo Afisa Elimu Kata ya Kiwanja cha Ndege, Mwl. Prisca Mgalula alisema kuwa wameichagua Shule ya Msingi Mahungu ili kuongeza uzuri wa mandhari ya shule hiyo mpya. “Mimi nimezaliwa tarehe 26 Aprili na tumeichagua shule hii kusherehekea kwa kupanda miti takribani 100. Kwa maana hiyo tunaendelea kuhamasisha agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dodoma la ‘Mti wangu, Birthday yangu’ kwa lengo la kuhamasisha wanafunzi kutunza mazingira, lakini pia itawasaidia kujifunzia kwa vitendo hapo baadae" alisema Mwl. Mgalula. Nae, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mahungu, Onesphory Massawe alianza kwa kusema kuwa wanafurahi kuwapokea watumushi hao na wanaahidi kuitunza miti hiyo ili ipendezeshe mandhari ya eneo...

Miti 100 yapandwa S/M Mahungu ‘Mti wangu, Birthday yangu’

Image
Na. Dennis Gondwe, KIZOTA AFISA Elimu Awali na Msingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Prisca Myalla ameongoza zoezi la upandaji miti 100 katika Shule ya Msingi Mahungu kwa wadau waliozaliwa Mwezi Aprili kwa lengo kuwaandalia mazingira mazuri ya kujisomea wanafunzi shuleni hapo. Alisema kuwa Shule ya Msingi Mahungu ni shule iliyojengwa kwa fedha za serikali kuu kupitia mradi wa Boost awamu ya pili Mwaka wa fedha 2024/2025. Akiongelea zoezi la upandaji miti katika shule hiyo, alisema kuwa ni kuunga mkono juhudi za serikali chini ya kauli hamasishi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ya ‘Mti wangu, Birthday yangu’. “Tupo hapa watumishi tuliojumuika kutoka taasisi mbalimbali ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuanzia walimu, wauguzi hadi maaskari. Sisi ni timu ya watumishi waliozaliwa Mwezi Aprili ‘Team Aprili’. Leo tutapanda miti kutekeleza maono ya mkuu wa mkoa kwamba ‘Mti wangu, Birthday yangu’. Kwa hiyo, tutapanda miti 100 katika eneo hili la shule ili kuendelea kukijanisha Dodoma ye...

Ujenzi Ofisi Kata Mbalawala watakiwa kukamilika kwa wakati

Image
Na. Leah Mabalwe, MBALAWALA Mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Kata ya Mbalawala watakiwa kukamilika kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma kwa urahisi. Hayo yalizungumzwa na Mhandisi wa Jiji la Dodoma, Mhandisi Ally Bella, katika zoezi la ukaguzi wa miradi ya maendeleo iliyofanywa na Kamati ya Fedha na Utawala robo ya tatu 2024/2025 katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema “ninakuagiza Afisa Mtendaji wa kata hii ya Mbalawala kusimamia mradi huu uweze kukamilika kwa haraka kwasababu wananchi wa eneo hili wanategemea ofisi hii kwaajili ya kupata huduma” alisema Mhandisi Bella. Nae, Awadhi Abdallah, Diwani wa Kata ya Zuzu aliishukuru Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kazi nzuri ambayo inaendelea kuifanya katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo. “Binafsi niishukuru Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo, kwasababu kazi za maendeleo zinaendelea kufanyika katika kila maeneno na sehemu ambazo hakuna basi Jiji la Dodo...

Wananchi washirikishwe katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA NAIBU Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fadhili Chibago ametoa rai kuwa miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa wananchi washirikishwe kikamilifu ili wawe sehemu ya miradi hiyo na kusema kuwa utaratibu huo utaifanya miradi kudumu kwa muda mrefu. Kauli hiyo aliitoa alipoongoza Kamati ya Fedha na Utawala timu namba tatu kutembelea na kukagua umaliziaji wa vyumba vitatu vya madarasa katika Shule ya Msingi Nguji iliyopo Kata ya Ng’hong’onha, jijini Dodoma. Alisema kuwa halmashauri inatekeleza miradi mingi ya maendeleo. “Nitumie nafasi hii kuwasisitiza kuendelea kuwashirikisha wananchi wa eneo husika kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Wananchi wakishirikishwa wanakuwa wamiliki wa mradi husika. Wasiposhirikishwa wanajiona siyo sehemu ya mradi. Hata kama kuna mtu anataka kufanya uharibifu kwenye mradi, wananchi wanabaki wanamtazama kwa sababu hawajashirikishwa. Nitumie nafasi hii kutoa rai, kwenye miradi yetu tunapoitekeleza, tuwashirikishe wananchi ...

Shule mpya ya Kata, Sekondari Miyuji B yajengwa kisasa kutoa elimu bora

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA KAMATI ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imempongeza Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa nia yake njema ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora hasa za elimu baada ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo yenye zaidi ya shilingi 500,000,000 katika kata tatu za jiji hilo. Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fadhili Chibago alipoongoza timu namba tatu ya Kamati ya Fedha na Utawala kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika kipindi cha robo ya tatu ya Mwaka wa Fedha 2024/2025. Alisema kuwa kamati yake ilitembelea kata tatu za Ng’hong’ohna, Makole na Miyuji kukagua miradi ya maendeleo. “Leo tumekuwa na ziara nzuri ya kutembelea miradi mbalimbali katika kata tatu za Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kamati ya Fedha na Utawala tuligawana na kupeana majukumu ya kutembelea miradi ya maendeleo. Timu yangu tumekagua umaliziaji wa vyumba vitatu vya madarasa Shule ya Msingi Nguji, Kata ya Ng’hong’onha, uje...

Jengo jumuishi la kutolea huduma za Afya Makole lipo katika hatua nzuri ya ujenzi

Image
Na. Nancy Kivuyo, MAKOLE Mradi wa ujenzi wa jengo jumuishi la kutolea huduma za afya katika Kituo cha Afya Makole wenye zaidi ya shilingi bilioni moja lipo katika hatua nzuri ya utekelezaji wake. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Makole, Dkt. Salma Gwassa alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Makole kwa Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliyotembelea maendeleo ya mradi huo. Alisema kuwa kiasi cha shilingi 750,000,000 kimetolewa na serikali kuu na fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma shilingi 289,794,329 zimelipwa kwa mkandarasi kwaajili ya ujenzi huo. Alisema kuwa ujenzi upo katika hatua ya msingi na wanatarajia mradi utakapokamilika wananchi wa Kata ya Viwandani na Jiji la Dodoma kwa ujumla watapata matibabu hapo. “Mradi huu ukikamilika huduma za kliniki za kibingwa ‘speciality clinic’ zitapatikana, huduma za kiutawala zitaboreka na tutapanua wigo wa utoaji wa huduma kwa wagonjw...

Ujenzi wa Darasa Sekondari Anthony Mavunde kupunguza msongamano kwa wanafunzi

Image
Na. Nancy Kivuyo, HOMBOLO BWAWANI Mkuu wa Shule ya Sekondari Anthony Mavunde, Mwalimu Emmanuel Magumba amesema kuwa shule hiyo ilipokea kiasi cha shilingi 15,425,000 kwa ajili ya ujenzi wa darasa moja na ununuzi wa viti 50 na meza 50 kwa lengo la kuongeza miundombinu katika shule hiyo. Mwl. Magumba alisoma taarifa ya mradi huo mbele ya Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kusema kuwa pamoja na ujenzi unaoendelea anaiomba halmashauri iwaongezee fedha kwa ajili ya kumalizia darasa hilo. “Hatua tuliyofikia ni nzuri kwasababu umaliziaji darasa hili sio mkubwa kama unavyoanza ujenzi” alisema Mwl. Magumba. Aliongeza kuwa kukamilika kwa darasa hilo kutaleta chachu ya wanafunzi kusoma kwa bidii. “Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa ujenzi wa darasa hili ukikamilika naamini wanafunzi wetu watapata nafasi ya kusoma na wataongeza bidii katika masomo” aliongeza Mwl. Magumba. Nae, Mwanafunzi wa Kidato cha Kwanza, Emmanuel Mbega alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kuwajen...

Ujenzi Ofisi Kata Mbalawala watakiwa kukamilika kwa wakati

Image
Na. Leah Mabalwe, MBALAWALA Mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Kata ya Mbalawala watakiwa kukamilika kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma kwa urahisi. Hayo yalizungumzwa na Mhandisi wa Jiji la Dodoma, Mhandisi Ally Bella, katika zoezi la ukaguzi wa miradi ya maendeleo iliyofanywa na Kamati ya Fedha na Utawala robo ya tatu 2024/2025 katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema “ninakuagiza Afisa Mtendaji wa kata hii ya Mbalawala kusimamia mradi huu uweze kukamilika kwa haraka kwasababu wananchi wa eneo hili wanategemea ofisi hii kwaajili ya kupata huduma” alisema Mhandisi Bella. Nae, Awadhi Abdallah, Diwani wa Kata ya Zuzu aliishukuru Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kazi nzuri ambayo inaendelea kuifanya katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo. “Binafsi niishukuru Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo, kwasababu kazi za maendeleo zinaendelea kufanyika katika kila maeneno na sehemu ambazo hakuna basi Jiji la Dodoma...

Shekimweri awapa maua yao Vijana Wilaya ya Dodoma

Image
Na. Mussa Richard. DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma , Alhaj . Jabir Shekimweri amewapongeza v ijana walioshiriki katika Kongamano la Mwenge wa Uhuru la vijana 2025 lililofanyika katika u wanja w a Shule ya Msingi Mbwanga jijini Dodoma. Aliyasema hayo wakati akimkaribisha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025, Ndugu Ismail Ussi wakati wa kufunga Kongamano la Mwenge wa Uhuru la vijana. “Nimefarijika kuona vijana wamejitokeza kwa wingi na kushiriki ipasavyo katika mada mbalimbali ambazo zimewasi l ishwa na watoa mada pamoja na wachombeza mada . Pia n iwatoe wasiwasi vijana wote walioshiriki katika k ongamano hili kuwa mapendekezo yao nimeyapokea na nitayafanyia kazi ili kuhakikisha vijana katika Wilaya ya Dodoma wanajikwamua kimaisha kwa kutatuliwa kwa baadhi ya changamoto ambazo zinawakabi l i ” alisema Alhaj . Shekimweri. Katika hatua nyingine aliwapongeza watoa mada na wachombeza mada wote walioshiriki katika kutoa mada na mafunzo mbalimbali kwa vijana katik...

Vijana watakiwa kuchangamkia fursa mbalimbali ili kujikwamua kiuchumi

Image
Na. Leah Mabalwe, MNADANI Mwakilishi wa Kampuni ya MAINLAND inayojenga Kiwanda cha kutengeneza mafuta ya Alizeti, Fadhili Makenjula awataka vijana kujitokeza katika nafasi za kazi mbalimbali zitakazotangazwa na kiwanda hicho cha Mafuta kitakapo kamilika mwezi Juni, 2025 ili kujikwamua kiuchumi. Mwakilishi wa Kampuni ya MAINLAND inayojenga Kiwanda cha kutengeneza mafuta ya Alizeti, Fadhili Makenjula Aliyazungumza hayo kwenye Kongamano la Vijana katika Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025 lililofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Mbwanga jijini Dodoma. Alisema kuwa vijana wanapaswa kuchangamkia fursa bila kuchagua kazi ili kujikwamua kiuchumi. “Nipende kuwataarifu kuwa, tupo katika hatua ya umaliziaji wa ujenzi wa kiwanda kikubwa cha mafuta ya alizeti kilichopo Kata ya Msalato, Mtaa wa Veyula. Vijana jitokezeni kwa wingi katika kutuma maombi ya kazi, kuna vitengo mbalimbali katika kiwanda hicho. Wewe kama kijana usiogope kuleta maombi yako kwaajili ya nafasi ya kazi. Tunawapa vija...

Mzee Bukitu aongelea Falsafa ya Mwenge wa Uhuru kwa Vijana Dodoma

Image
Na. Nancy Kivuyo, MNADANI Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation, Mzee Joseph Butiku amesema falsafa ya Mwenge wa Uhuru ilianzishwa kwa lengo la kuleta upendo na mshikamano kwa taifa huku mwanga wa Mwenge ukiangazia mipaka ili kuleta matumaini palipo kukata tamaa, upendo palipo uadui na heshima palipo chuki. Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation, Mzee Joseph Butiku akielezea Falsafa ya Mwenge wa Uhuru Aliyasema hayo katika Kongamano la Mwenge wa Uhuru la Vijana 2025 lililofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Mbwanga. Alisema kuwa katika kipindi cha mwaka 1958 Mwalimu Nyerere alianzisha falsafa hiyo kipindi cha jitihada za kupata uhuru. “Niwaeleze kuwa, Mwenge wa Uhuru ni kielelezo cha amani na matumaini. Wakati sisi tunapata ufahamu kuhusu Mwenge, tuliingiwa na uzalendo wa hali ya juu ndio maana mnaona taifa letu lipo imara hadi leo” alisema Mzee Butiku. Aliongeza kuwa vijana wa kizazi cha leo wanapaswa kuisoma historia ya Mwenge wa Uhuru kwa mapenzi ...

Wilaya ya Dodoma mtekelezaji kinara Agenda ya Nishati safi ya kupikia

Image
Na. Dennis Gondwe, NALA WILAYA ya Dodoma imekuwa ikitekeleza maagizo na falsafa ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa vitendo katika utekelezaji wa dhamira yake ya nishati safi. Kauli hiyo ilitolewa na Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde alipokuwa akisalimia mamia ya wananchi wa Jiji la Dodoma waliojitokeza kuulaki Mwenge wa Uhuru ulipotembelea Shule ya Sekondari ya Wasichana Santhome - SABS kutembelea mradi wa nishati safi ya kupikia. Mavunde alisema kuwa Wilaya ya Dodoma ipo mstari wa mbele kutekeleza maagizo na falsafa ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa vitendo ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi. ”Mheshimiwa mkuu wa wilaya ninakushukuru sana kwa kusimamia kikamilifu na kuhakikisha taasisi na shule mbalimbali zinafunga mfumo wa nishati safi ya kupikia. Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Mwaka 2025, Wilaya ya Dodoma ni kati ya wilaya kielelezo kwa nchi yetu katika kutekeleza falsafa ya rais wetu” alisema Mavunde. Akisoma taarifa ya mradi wa ni...

Mwenge wa Uhuru waridhishwa na ujenzi wa Barabara yenye urefu wa KM 1.6 kiwango cha lami

Image
Na. Dennis Gondwe, NALA MWENGE wa Uhuru Mwaka 2025 umeridhishwa na kiwango cha ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 1.6 kwa kiwango cha lami kutoka barabara iendayo Singida hadi Hospitali ya Jiji la Dodoma inayojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 2.8. Kauli hiyo ilitolewa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Mwaka 2025, Ismail Ussi alipokuwa akiongea na wananchi wa Kata ya Nala na maeneo ya jirani waliojitokeza kwa wingi kuupokea na kuushangilia Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025 uliotembelea ujenzi wa barabara hiyo. Alisema kuwa Mwenge wa Uhuru ni ishara ya matumaini, upendo, heshima, amani na maendeleo chini ya serikali ya awamu ya sita. “Leo tumekuja kujionea ujenzi wa barabara ya kisasa yenye ubora, inayojengwa na serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kilometa 1.6 kwa kiwango cha lami. Wananchi wa kata waliomba barabara hii kupitia mbunge na diwani wao. Barabara hii itasaidia wananchi wanapoenda kupata huduma za afya katika Hosp...

Mwenge wa Uhuru kutembelea miradi 7 ya shilingi Bil. 11.1 Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, CHIGONGWE MWENGE wa Uhuru Mwaka 2025 utatembelea miradi saba ya maendeleo yenye gharama ya shilingi bilioni 11.1 iliyotekelezwa kwa ajili ya kuwapelekea maendeleo na kuboresha maisha ya wananchi katika Wilaya ya Dodoma. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri (kushoto) wakati akipokea Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025 kutoka kwa Mkuu wa Wilaya Bahi Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri wakati akipokea Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025 kutoka kwa Mkuu wa Wilaya Bahi tukio lililofanyika katika uwanja wa Ofisi ya Afisa Mtendaji Kata ya Chigongwe jijini Dodoma. Shekimweri alisema kuwa Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025 ukiwa katika Wilaya ya Dodoma utachochea maendeleo. “Mimi Jabir Mussa Shekimweri, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, nakiri kuupokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mheshimiwa Joachim Nyingo ukiwa unawaka, unang’aa na unameremeta. Aidha, nakiri kuwapokea wakimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa wakiwa na afya njema. Mwenge wa Uhuru ukiwa...