Wanawake Jiji la Dodoma washauriwa kuandaa vyakula kwa nishati safi ya kupikia
Na. Faraja Mbise, DODOMA Wanawake wameshauriwa kutumia nishati safi ya kupikia katika kuandaa vyakula vya watoto kwasababu upatikanaji wake ni rahisi ukilinganisha na matumizi ya nishati chafu ya kupikia kama vile mkaa na kuni kutokana na kuwa inaokoa muda na ni salama kwa mazingira. Afisa Lishe wa Kituo cha Afya cha Makole, Frida Mollel wakati akitoa mafunzo kwa vitendo juu ya jiko darasa kwa akina mama wanaonyonyesha waliohudhuria kliniki Ushauri huo ulitolewa na Afisa Lishe wa Kituo cha Afya cha Makole, Frida Mollel wakati akiwafundisha juu ya jiko darasa kwa akina mama wanaonyonyesha waliohudhuria kliniki katika Kituo cha Afya Makole kilichopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mollel aliwataka kutumia nishati safi ya kupikia wanapoandaa chakula cha watoto wao kwasababu upatikanaji wake ni rahisi na usalama kwa mtoto ni mkubwa zaidi ukilinganisha na matumizi ya nishati chafu ya kupikia. “Sambamba na elimu ambayo tumeitoa, utumiaji wa nishati safi umekuwa ukirahisisha uandaaji wa ...