Posts

Showing posts from October, 2024

Wanawake Jiji la Dodoma washauriwa kuandaa vyakula kwa nishati safi ya kupikia

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Wanawake wameshauriwa kutumia nishati safi ya kupikia katika kuandaa vyakula vya watoto kwasababu upatikanaji wake ni rahisi ukilinganisha na matumizi ya nishati chafu ya kupikia kama vile mkaa na kuni kutokana na kuwa inaokoa muda na ni salama kwa mazingira. Afisa Lishe wa Kituo cha Afya cha Makole, Frida Mollel wakati akitoa mafunzo kwa vitendo juu ya jiko darasa kwa akina mama wanaonyonyesha waliohudhuria kliniki Ushauri huo ulitolewa na Afisa Lishe wa Kituo cha Afya cha Makole, Frida Mollel wakati akiwafundisha juu ya jiko darasa kwa akina mama wanaonyonyesha waliohudhuria kliniki katika Kituo cha Afya Makole kilichopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mollel aliwataka kutumia nishati safi ya kupikia wanapoandaa chakula cha watoto wao kwasababu upatikanaji wake ni rahisi na usalama kwa mtoto ni mkubwa zaidi ukilinganisha na matumizi ya nishati chafu ya kupikia. “Sambamba na elimu ambayo tumeitoa, utumiaji wa nishati safi umekuwa ukirahisisha uandaaji wa ...

Elimu ya unyonyeshaji sahihi yatolewa kwa kina mama Jiji la Dodoma

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Akina mama wamepewa elimu ya unyonyeshaji sahihi maziwa ya mama kwa lengo la kuwajengea uelewa mpana utakaowasaidia kuwakuza vizuri watoto wao ili wawe na afya njema na lishe bora katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Afisa Muuguzi Msaidizi, Kituo cha Afya Makole, Christopher Tarimo akielezea njia sahihi ya kumshika mtoto wakati wa kumnyonyesha maziwa ya mama Hayo yalisemwa na Afisa Muuguzi Msaidizi, Kituo cha Afya Makole, Christopher Tarimo, alipokuwa akitoa elimu ya namna sahihi ya kumnyonyesha mtoto na lishe kwa akina mama waliojifungua katika wodi ya wazazi kituoni hapo. Akizungumza na akina mama hao Afisa Muuguzi Msaizidi, aliwashauri kuzingatia mikao ya unyonyeshaji pindi wanapowanyonyesha watoto wao. “Katika unyonyeshaji lazima tutenge muda, ile nusu saa ya kwanza au lisaa limoja hakikisha kwamba simu umeweka pembeni, hausumbuliwi na mtu yeyote unakuwa umetulia mawazo yote kwa mtoto. Unatakiwa uwe umekaa, tunashauri sana kumnyonyesha mtoto ukiwa um...

Jiji la Dodoma kukusanya shilingi 1,902,895,000.00 kutoka Soko la wazi la Machinga

Image
  Na. Asteria Frank, DODOMA   Halmashauri ya Jiji la Dodoma imepanga kukusanya kiasi cha shilingi 1,902,895,000.00 kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato katika Soko la wazi la Machinga ili kuweza kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2024/2025.   Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko wakati akisoma taarifa ya uendeshaji wa Soko la wazi la Machinga kwa Kamati kudumu ya Bunge ya Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa iliyofanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya soko hilo lililopo eneo la Bahi Road jijini Dodoma.   Dkt. Sagamiko alisema kuwa ujenzi wa soko hilo uligharimu kiasi cha shilingi 9,529,747,200.66. Kati ya fedha hizo shilingi 6,529,747,200.66 ni mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji, shilingi 2,500,000,000.00 ni ruzuku kutoka Serikali kuu na shilingi 500,000,00.00 ni fedha za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ...

Fursa uwekezaji kilimo cha Zabibu Dodoma

Na. Faraja Mbise, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni kivutio kikubwa katika kilimo cha zabibu nchini kutokana na zao hilo la kibiashara kustawi vizuri na kuwanufaisha wananchi. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Kilimo mjini Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Yustina Munishi alipokuwa alielezea fursa za kilimo zinazopatikana Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Mkutano wa Baraza la Biashara Wilaya ya Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba. Munishi aliwashauri wawekezaji na wakulima kuwekeza katika kilimo. “Zipo fursa nyingi za uwekezaji katika maeneo mengi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Tuna fursa kubwa ya uwekezaji kwenye kilimo cha zao la Zabibu. Zao la Zabibu inalimwa hapa Dodoma kwahiyo, mtu yeyote anaweza akatumia fursa hiyo kwa kuangalia maeneo yale yenye uwezekano mkubwa wa kulima zao hilo, ambayo yapo maeneo ya Hombolo Bwawani, Makulu, Chihanga, Matumbulu, Mpunguzi na Mbabala. Kwahiyo, tunaangalia ule ...

Jiji la Dodoma linafursa lukuki uwekezaji

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma inazo fursa lukuli kwa ajili ya wawekezaji na wafanyabiashara katika maeneo ya kilimo, viwanda, biashara, michezo na maeneo mengine yanayoweza kusisimua ukuaji wa uchumi. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Abdul Chacha alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Mkutano wa Baraza la Biashara Wilaya ya Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba. “Halmashauri ya Jiji la Dodoma ina fursa nyingi sana, una fursa ya kuwekeza katika maeneo ya michezo kwa ujumla, kwasababu saizi tunaangalia AFCON inakuja. Kwahiyo, watu wengi watahitaji sehemu ambazo zimeandaliwa kwa ajili ya michezo. Vilevile, nyumba za kupanga na kuuza (apartments). Kipindi hiki wageni wanaingia wengi sana hivyo, wanahitaji sehemu za kufikia kwa maana ya malazi, hizo ni fursa zinazopatina. Lakini biashara mbalimbali za chakula kama kuk...

Jiji la Dodoma linafursa lukuki uwekezaji

  Na. Faraja Mbise, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma inazo fursa lukuli kwa ajili ya wawekezaji na wafanyabiashara katika maeneo ya kilimo, viwanda, biashara, michezo na maeneo mengine yanayoweza kusisimua ukuaji wa uchumi. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Baraza la Biashara la Wilaya ya Dodoma, Abdul Chacha alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Mkutano wa Baraza la Biashara Wilaya ya Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba. “Halmashauri ya Jiji la Dodoma ina fursa nyingi sana, una fursa ya kuwekeza katika maeneo ya michezo kwa ujumla, kwasababu saizi tunaangalia AFCON inakuja. Kwahiyo, watu wengi watahitaji sehemu ambazo zimeandaliwa kwa ajili ya michezo. Vilevile, nyumba za kupanga na kuuza (apartment). Kipindi hiki wageni wanaingia wengi sana hivyo, wanahitaji sehemu za kufikia kwa maana ya malazi, hizo ni fursa zinazopatina. Lakini biashara mbalimbali za chakula kama kuku, nyama, mbogamboga na matunda ni...

Orodha ya Wapiga kura yabandikwa Makole

Image
 

Mtaa wa Nationa Housing na Makole wabandika orodha ya wapiga kura Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Image
  Wakazi wa Mtaa wa National housing na Makole, Kata ya Makole wamejitokeza katika ofisi ya Afisa Mtendaji Kata ya Makole ili kuhakiki majina yao kama yametoka katika orodha ya wapiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024

Kata ya Makole yabandika orodha ya wapiga kura Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Image
  Ofisi ya Afisa Mtendaji Kata ya Makole imebandika orodha ya majina ya watu waliojiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe 27 Novemba, 2024

Alhaj Jabir Shekimweri aibukia Mtaa kwa Mtaa Uchaguzi Festival kuhamasisha wananchi kujiandikisha

Image
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri akiwahamasisha wananchi kwenda kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Tamasha la Mtaa kwa Mtaa Uchaguzi Festival katika Mtaa wa Swaswa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri (wapili kushoto) na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Sakina Mbugi (wa kwanza kushoto) wakishuhudia Tamasha la Mtaa kwa Mtaa Uchaguzi Festival katika Mtaa wa Swaswa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kujiorodhesha kwenye orodha ya wapiga kura.  

Afisa Mtendaji Mnadani ndani ya Orodha ya Wapiga kura

Image
  Afisa Mtendaji Kata ya Mnadani, Caroline Masawe akijiandikisha katika Orodha ya Wapiga kura kwenye Kituo cha Ofisi ya Afisa Mtendaji Mtaa wa Mnadani

Ukomo wa Madaraka

Image
 

Kuchukua na Kurejesha Fomu za Kugombea Uongozi

Image
 

Elimu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa inaendelea

Image
 

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Wafanyabiashara wamo

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Wafanyabiashara Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamehamasishwa kujitokeza kushiriki katika mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura ili kupata viongozi walio bora ambao wanatambua wajibu wao ili kuwawezesha wafanyabiashara kutatua changamoto zao katika biashara. Meneja wa Hoteli ya Spring Hills, William Mndeme akielezea umuhimu wa wafanyabiashara kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Rai hiyo ilitolewa na Meneja wa Hoteli ya Spring Hills, William Mndeme alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa wafanyabiashara kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Meneja Mndeme aliwashauri wafanyabiashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuitikia wito wa kwenda kujiandikisha ili waweze kuchagua viongozi walio bora na wenye manufaa katika kukuza uchumi wa nchi. “Ili tuweze kufanya biashara vizuri, lazima tuwe na viongozi bora na viongozi wanaotambua wajibu wao...

Wafanyabiashara Dodoma washauriwa kujiandikisha orodha ya wapiga kura

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Wafanyabiashara wameshauriwa kutumia haki yao ya msingi ya kikatiba kupiga kura kwa kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ili waweze kupiga kura na kuwachagua viongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa. Meneja wa Kidia Vision Hotel, William Moshi Ushauri huo ulitolewa na Meneja wa Kidia Vision Hotel, William Moshi alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa wafanyabiashara kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ili kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa nje ya hoteli yake. Moshi ambae ni moja ya wafanyabiashara maarufu alisema kuwa anawahamasisha wananchi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kujitokeza kushiriki zoezi la kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura. Kupiga kura ni haki ya msingi ya kikatiba. Wananchi watumie fursa hiyo kuchagua viongozi wa Serikali za Mitaa ili kuepukana na madhara yote yatakayojitokeza pindi wasipojiandikisha katika orodha ya wapiga kura na kushindwa kuwachagua viongozi bora. “Nawasihi wakazi wot...

Ujenzi Ofisi ya Machinga Mkoa wa Dodoma

Image
 

Mabango ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa yatawanywa kila kona za Jiji la Dodoma

Image
 

Wananchi Mtaa wa Fatina wajiandikisha kwenye

Image
 

Uandikishaji Kata ya Makole na Hazina

Image
 

Wananchi waliojiorodhesha Mkonze wawe Mabalozi kuhamasisha wengine

Image
  Na. Dennis Gondwe, BWAWANI, MKONZE WANANCHI waliojiorodhesha katika orodha ya wapiga kura wameshauriwa kuwa mabalozi ili kuhamasisha wenzao ambao hawajajiorodhesha kufanya hivyo mapema ili kuepuka foleni siku ya mwisho hatua itakayowawezesha kuchagua viongozi bora. Mkazi wa Mtaa Bwawani, Kata ya Mkonze, Patrick Richard baada ya kujiandikisha Rai hiyo ilitolewa na mkazi wa Mtaa Bwawani, Kata ya Mkonze, Patrick Richard muda mfupi baada ya kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura katika kituo cha Ofisi ya Afisa Mtendaji Mtaa wa Bwawani mapema leo. Richard alisema “mimi nimetumia muda mfupi sana, chini ya dakika moja kujiandikisha katika daftari la wapiga kura wakati nilijua nitatumia muda mrefu. Kumbe hata wakija watu 10 kwa pamoja watatumia chini ya dakika 10 kujiandikisha. Wito wangu wananchi waje kwa wingi kujiandikisha katika kituo hiki kilichopo kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Bwawani. Sisi ambao tumeshajiandikisha na kuona uandikishaji ulivyo tuwe mabalozi tu...

Viongozi bora wanachaguliwa na wananchi waliojiorodhesha

Image
Na. Dennis Gondwe, MWAJA, CHAMWINO VIONGOZI bora wa serikali za mitaa wanachaguliwa na wananchi waliojiandikisha katika orodha ya wapiga kura ili waweze kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Mkazi wa Mtaa wa Mwaja, Kata ya Chamwino, Josephine Joseph wakati akijiandikisha katika orodha ya wapiga kura  Kauli hiyo ilitolewa na mkazi wa Mtaa wa Mwaja, Kata ya Chamwino, Josephine Joseph alipoongea na mwandishi wa habari hii muda mfupi baada ya kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura katika kituo cha Shule ya Msingi Chinangali. Joseph alisema kuwa kujiandikisha ni haki yake na haki ya kila mwananchi mwenye sifa za kujiandikisha. “Viongozi bora wa serikali za mitaa wanachaguliwa na wananchi wenyewe. Hivyo, ili uweze kumchagua kiongozi bora, sifa ya kwanza uwe umejiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura katika mtaa wako. Bahati nzuri sifa ni za kawaida sana, kwamba awe na umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea, awe mtanzania mwenye akili timamu zaidi awe ni mkazi wa mtaa ambao u...

Chama cha Siasa kinawakilishwa na Wakala kituoni

Image
 

Uhamasishaji Jiji la Dodoma ni Kona kwa Kona

Image
 

Mabango ya Elimu kwa Wananchi juu ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa yatapakaa Jiji la Dodoma

Image
 

Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma akikabidhi Mwongozo wa Uchaguzi kwa Mwakilishi wa Waandishi wa habari

Image
 

Hakuna Mamluki yeyote atakayeandikishwa kwenye orodha ya wapiga kura Jiji la Dodoma

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko amekanusha taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusu mwenendo wa uandikishaji kuwa wanaandikishwa mamluki kwenye orodha ya wapiga kura. Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko akifafanua mwenendo wa zoezi la uandikishaji orodha ya wapiga kura Jiji la Dodoma Kanusho hilo alilitoa ofisini kwake alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kufuatia tuhuma zilizotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kuhusu mwenendo wa uandikishaji orodha ya wapiga kura unaoendelea wakidai kuwa kituo kimoja kiliandikisha watu kinyume na utaratibu. Dkt. Sagamiko alisema “kutokana na taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii, zinazoelezea kuhusu muenendo wa uandikishaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa bahati mbaya sana taarifa ile inaelezea kuhusu mwenendo mbaya wa uandikishaji. Baada ya kupitia na kusikiliza kwa makini video il...