Fursa uwekezaji kilimo cha Zabibu Dodoma

Na. Faraja Mbise, DODOMA

Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni kivutio kikubwa katika kilimo cha zabibu nchini kutokana na zao hilo la kibiashara kustawi vizuri na kuwanufaisha wananchi.


Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Kilimo mjini Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Yustina Munishi alipokuwa alielezea fursa za kilimo zinazopatikana Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Mkutano wa Baraza la Biashara Wilaya ya Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba.

Munishi aliwashauri wawekezaji na wakulima kuwekeza katika kilimo. “Zipo fursa nyingi za uwekezaji katika maeneo mengi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Tuna fursa kubwa ya uwekezaji kwenye kilimo cha zao la Zabibu. Zao la Zabibu inalimwa hapa Dodoma kwahiyo, mtu yeyote anaweza akatumia fursa hiyo kwa kuangalia maeneo yale yenye uwezekano mkubwa wa kulima zao hilo, ambayo yapo maeneo ya Hombolo Bwawani, Makulu, Chihanga, Matumbulu, Mpunguzi na Mbabala. Kwahiyo, tunaangalia ule mnyororo mzima wa zao la Zabibu, jinsi ambavyo unaweza kutengeneza ‘wine’, juisi na matunda” alisema Munishi.

Akiongelea uwekezaji wa halmashauri katika kilimo hicho alisema kuwa imewekeza kwa kiwango kikubwa kwa kuboresha zao hilo liwe la kibiashara.

“Halmashauri ya Jiji imewekeza katika kilimo hiki kwa sababu imefundisha wataalam na wengine kupelekwa nchini Afrika ya Kusini kwa ajili ya kujifunza jinsi ya kuboresha kilimo cha Zabibu. Kwahiyo, ni fursa ambayo mtanzania na mwanadodoma unakaribishwa kuwekeza kwenye mnyororo wa thamani wa zao la Zabibu” alisema Munishi.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma