Wananchi waliojiorodhesha Mkonze wawe Mabalozi kuhamasisha wengine

 Na. Dennis Gondwe, BWAWANI, MKONZE

WANANCHI waliojiorodhesha katika orodha ya wapiga kura wameshauriwa kuwa mabalozi ili kuhamasisha wenzao ambao hawajajiorodhesha kufanya hivyo mapema ili kuepuka foleni siku ya mwisho hatua itakayowawezesha kuchagua viongozi bora.


Mkazi wa Mtaa Bwawani, Kata ya Mkonze, Patrick Richard baada ya kujiandikisha


Rai hiyo ilitolewa na mkazi wa Mtaa Bwawani, Kata ya Mkonze, Patrick Richard muda mfupi baada ya kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura katika kituo cha Ofisi ya Afisa Mtendaji Mtaa wa Bwawani mapema leo.

Richard alisema “mimi nimetumia muda mfupi sana, chini ya dakika moja kujiandikisha katika daftari la wapiga kura wakati nilijua nitatumia muda mrefu. Kumbe hata wakija watu 10 kwa pamoja watatumia chini ya dakika 10 kujiandikisha. Wito wangu wananchi waje kwa wingi kujiandikisha katika kituo hiki kilichopo kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Bwawani. Sisi ambao tumeshajiandikisha na kuona uandikishaji ulivyo tuwe mabalozi tuwashawishi na wengine ambao hawajajiandikisha kuja kwa sababu hawapotezi muda kabisa”.

Akiongelea lengo la kujiandikisha kwake alisema kuwa pamoja kuwa ni haki yake ya kikatiba, pia anategemea kugombea nafasi ya uongozi katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. “Mfano, mimi natarajia kugombea nafasi ya mjumbe wa kamati ya mtaa. Hivyo, ninawajibu wa kuhamasisha wananchi wajitokeze kujiandikisha ili waje kushiriki katika kupiga kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa” alisema Richard.

Zoezi la kuandikisha wananchi katika orodha ya wapiga kura katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma lilianza tarehe 11 Oktoba, 2024 likitarajiwa kukamilika tarehe 20 Oktoba, 2024 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utafanyika tarehe 27 Novemba, 2024.


Mabango ya taarifa muhimu yalimoyandikwa katika Ofisi ya Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Bwawani


MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma