Posts

Showing posts from January, 2025

Dodoma Jiji FC inafukuza Mwizi Kimya Kimya

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Timu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, imeendelea na maandalizi ya kujiwinda na michezo ya Ligi kuu ya NBC Tanzania bara, kwasasa imekita kambi mkoani Arusha, na imecheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu inayoshiriki Ligi Daraja la kwanza Mbuni FC, mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha na Dodoma Jiji FC kuchomoza na ushindi wa bao 1-0. Akizungumza baada ya mchezo kutamatika Kocha wa Viungo wa Dodoma Jiji FC, Fransis Mkanula alisema “tumekuja hapa Arusha kuweka kambi ya siku tano, tumekuja hapa kupata mechi za kirafiki kwasababu timu imetoka kwenye mapumziko, baada ya ratiba kutoka tukaamua kuja hapa Arusha kucheza mechi za kirafiki ili kurudisha utimamu wa miili kwa wachezaji pia ukizingatia tuna maingizo mapya kwenye timu. Kwahiyo, tumekuja kutengeneza mazingira ya kuzoeana na wenzao na kuingia kwenye mfumo wa timu”. Nae, Nahodha wa Dodoma Jiji FC, Augustin Nsata akaelezea hali ya kambi na maandalizi ya timu kuelekea kwenye michezo ...

Dodoma Jiji U20 FC yakamiwa na Maafande wa Gunners FC

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Timu ya soka ya Dodoma Jiji chini ya umri wa miaka 20 imechezea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Timu ya Gunners FC, katika mchezo wa kirafiki uliovurumishwa katika uwanja wa Shell Complex jijini Dodoma hii leo. Akizungumza baada ya kutamatika kwa dakika tisini Kocha Mkuu wa Timu ya Dodoma Jiji U20, Jeremiah Chido alisema “mchezo umeisha salama, tumepoteza mchezo kwasababu tumekutana na timu nzuri na yenye daraja la juu. Kwetu sisi alikuwa ni mshindani sahihi kutokana na maandalizi yetu tunayoyafanya kwaajili ya michezo inayofuata ya ligi ya vijana michezo ambayo tutakuwa ugenini ndiyo maana leo tumewapa nafasi wachezaji wote ili kuwatengenezea utimamu wa mwili kwaajili ya kurudi kwenye michezo ya ligi’’. Katika hatua nyingine Chido akazungumzia hali ya majeruhi kwenye timu yake na kuwaaminisha mashabiki kuwa wachezaji hao watarejea uwanjani na kuendelea kuipambania timu. “Katika mchezo wa leo wachezaji wawili wamepata majeraha, lakini siyo majeraha makubw...

Kata 41 jijini Dodoma kunufaika na Milioni 150 za Miradi ya Maendeleo

Image
Na. Shahanazi Subeti, DODOMA Baraza la Madiwani wa Jiji la Dodoma wameipongeza Halmashauri ya Jiji chini ya Mkurugenzi na jopo lake kwa kutenga shilingi bilioni saba kwa ajili ya kumalizia miradi viporo na shilingi milioni 150 kwa kila kata kuanzisha miradi mipya ili kuleta maendeleo kwa wananchi. Madiwani waliyasema hayo katika mkutano maalum wa kupitia rasimu ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe, alisema kuwa Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma inalenga kukamilisha miradi viporo katika jumla ya kata 41 za halmashauri hiyo. “ Kwa mwaka huu, Bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma inafikia takribani shilingi Bilioni 147 inayolenga kwenda kukamilisha miradi viporo katika kata zetu 41. Miradi yote ambayo haikuisha kwa wakati kutokana na sababu zozote zile. Hivyo, tayari imetengwa kiasi cha shilingi Bilioni saba ili ...

Jiji la Dodoma kuingia ubia utekelezaji Miradi

Image
  Na. Halima Majidi, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika kuhakikisha inaimarisha na kukuza wigo wa ukusanyaji wa mapato kwa maendeleo yake na nchi kwa ujumla imeainisha miradi ya kuingia ubia na kushirikisha sekta binafsi na za umma. Akizungumza katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kupitia mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti ya Mwaka 2025/2026, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe, alisema kuwa halmashauri imekuja na mkakati mpya wa kujiweka tayari kwa kufanya miradi kwa ubia kupitia mfumo wa ushirikishaji sekta binafsi na sekta ya umma (PPP). Prof. Mwamfupe alisema kuwa miradi mingi imewekwa katika masoko ili kuweza kuita na kuvutia sekta binafsi ili waweze kushiriki na kuwekeza katika miradi hiyo. “Kwa kuangalia miradi ambayo tulikuwa nayo kipindi cha nyuma na kwa kujifunza kutokana na hiyo tumepata tabu sana kukamilisha miradi miwili ya hoteli. Kwahiyo, tumeweka mkaka...

Sekta binafsi kugharamia miradi Jiji la Dodoma Bajeti ya 2025/2026

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Sekta binafsi itashiriki kugharamia miradi ya maendeleo kwa njia ya ubia katika utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 kutokana na umuhimu wa sekta hiyo kwa maendeleo ya Jiji la Dodoma. Katibu wa Baraza la Madiwani, Dkt. Frederick Sagamiko Mapendekezo ya Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, imeshirikisha sekta binafsi kutokana na matamanio na mahitaji kuwa makubwa kuliko makusanyo ya mapato. Hayo yalisemwa na Katibu wa Baraza la Madiwani ambaye ni Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko, alipokuwa anatolea ufafanuzi katika baadhi ya masuala yaliyowasilishwa katika Mkutano wa Baraza la Madiwani maalum kwa ajili ya kupokea na kupitia mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/26 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma tarehe 30 Januari, 2025. Dkt. Sagamiko alisema “ matamanio yetu na mahitaji yetu ni makubwa kul...

Wananchi Dodoma wahimizwa kutunza Mazingira

Image
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Mkuu wa Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa taka ngumu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro, alisema kitengo kicho kimejipanga kikamilifu katika kuendelea kutekeleza shughuli mbalimbali za udhibiti na uondoshaji wa taka ili kuhakikisha Jiji la Dodoma linakuwa katika hali ya usafi na kuvutia. Aliyasema hayo nje ya Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani la kupitia rasimu ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Akizungumzia kuhusu udhibiti wa taka ngumu, Dickson Kimaro, alisema kupitia bajeti iliyotengwa na halmashauri, kitengo hicho kinajiandaa na mchakato wa kununua mitambo maalum kwaajili ya kuchakata takataka na kuwepo kwa gari ili kukusanya na kupeleka eneo la dampo kuu la Chidaya. “Tunatarajia kwenda kununua mitambo ya kuchakata takataka, lakini kununua malori kwaajili ya uondoshaji wa taka ili kuondokana na mfumo wa ‘Collection Point’, bali kuchuku...

Sekta ya Michezo yaguswa Bajeti 2025/2026 Halmashauri ya Jiji la Dodoma

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imepanga kujenga viwanja vya michezo ikiwemo uwanja wa mpira wa miguu uliopo katika mchakato wa ujenzi, kuelekea michuano ya Mataifa ya Afrika (Afcon) 2027 ambapo kwa pamoja nchi za Afrika Mashariki Tanzania, Kenya na Uganda zitakuwa wenyeji wa michuano hiyo. Mpango huo umewekwa wazi na Mchumi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Francis Kaunda kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Dkt.   Frederick Sagamiko, wakati akiwasilisha Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 katika Baraza Maalum la Madiwani, lililofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kwa upande wake Daudi Fundikira, Diwani wa Kata ya Chang'ombe baada ya kupitishwa kwa Bajeti hiyo alisema "Tumepanga kujenga viwanja vya michezo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambavyo vitakua ni sehemu ya kuongeza mapato kwa jiji letu la Dodoma, lakini pia ni fursa kwa vijana wetu kufanya mazoezi na kuweza kuonekana, kwani michezo ni ajira na mic...

Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma launga mkono maono ya Rais Dkt. Samia Nishati safi

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inaunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha nishati safi kwa wote inapatikana kwa lengo la kuboresha maisha ya watanzania. Kauli hiyo ilitolewa na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Prof. Davis Mwamfupe alipokuwa akifungua mkutano wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujadili na kupitia mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/ 2026 mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Prof. Mwamfupe alisema “ sisi Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma tunatoa pongezi kwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara wa nishati safi. Mwanzo mwa wiki hii dunia yote macho yalikuwa Tanzania kwa ajili ya mkutano wa nishati kwa ajili ya afya kwa manufaa ya wananchi wetu na mazingira bora. Dodoma ni wanufaika wakubwa wa dhana hiyo kwasababu miti yetu itabaki salama. Sisi ni waungaji mkono namba moja wa dhana hii ”. ...

Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma lapitisha Bajeti 2025/2026 shilingi bil. 147

Image
Na. Coletha Charles, DODOMA Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma lapitisha kwa kauli moja rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 jumla ya shilingi bilioni 147.9 ikiwa ni ongezeko la asilimia 7.04 ukilinganisha na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2024/2025. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri wa jiji hilo, ambao ulilenga kupitisha mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026. Akiwasilisha rasimu hiyo, Mchumi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Francis Kaunda, alisema kuwa h almashauri imekasimia kukusanya shilingi bilioni 67.3 kati ya fedha hizo bilioni 43 ni mapato yasiyolindwa na shilingi 24.3 ni mapato lindwa, ambapo halmashauri ipo kwenye kundi ambalo asilimia 70 ya mapato yasiyolindwa inayoelekezwa kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 30 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida. Alisema kuwa, rasimu ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 itagharamiwa na vyanzo vikuu vinn...

Matukio katika Picha wakati wa kukabidhi Taarifa ya ubainishaji wa watoto wenye mahitaji maalumu kwa mwaka 2025 Jiji la Dodoma

Image
 

Wataalam wa Mawasiliano na Maendeleo ya Jamii washiriki kubainisha watoto wenye mahitaji maalum

Image
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo, aliwataka watumishi wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi, kuongeza wigo kwa kutumia wataalam wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Maendeleo ya Jamii ili kuhakikisha wanasambaza taarifa za uhamasishaji na kubainisha watoto wenye mahitaji maalumu katika jamii. Fungo aliyasema hayo ofisini kwake alipopokea taarifa ya ubainishaji wa watoto wenye mahitaji maalumu kwa mwaka 2025 kutoka Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Jiji la Dodoma baada ya kukamilika zoezi la utambuzi na ubainishaji wa watoto wenye mahitaji maalum kwa jili ya kuandikishwa elimu ya awali na darasa la kwanza zoezi lililoanza 07 hadi 22 Januari, 2025. Akitoa pongezi kwa kazi nzuri ya ubainishaji wa watoto wenye mahitaji maalumu, Kaimu Mkurugenzi, alisema kuwa serikali inafanya juhudi kubwa kuhakikisha watoto hao wanapata haki stahiki na huduma za msingi ili kujiona wako sawa na binadamu wengine. “Mpaka serikali inafan...

Alhaj Shekimweri ahamasisha umuhimu wa mazoezi kwa wachezaji Dodoma Jiji FC

Image
Na. Coletha Charles, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, ameitembelea Timu ya Dodoma Jiji FC, inayondelea na mazoezi ya maandalizi ya msimu wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa lengo la kuwahamasisha wachezaji na viongozi wa timu kwa ajili ya kujiandaa vema. Akizungumza na wachezaji na viongozi wa timu kwenye uwanja John Merlin, Mkuu wa Wilaya alisisitiza umuhimu wa maandalizi mazuri kwa ajili ya msimu wa pili wa ligi kuu na kuwataka wachezaji kufanya mazoezi ili kuhakikisha wanapata mafanikio. Alisema kuwa, wanatakiwa kuweka mikakati yenye uhalisia kwa sababu wanaenda kwenye kipindi kibaya ambapo kusipokuwa na utulivu na maelewano wataishia kulaumiana na kushutumiana. “ Tunaenda ‘second round’ ya ligi yetu hatuko sehemu nzuri sana, hatuko sehemu mbaya sana katika mechi 16 nafikiri tuna ‘point’ 19 wastani wa ‘point’ moja kwa kila mechi. Kwahiyo, kuna haja ya kuwa familia moja kama alivyoongea mwalimu kwa kuelewa nini kipo mbele yetu. Tuna mechi 14 tu za kuju...

Dodoma Jiji FC kujichimbia Arusha kujiwinda na duru ya pili ya NBC PL

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, imepanga kwenda kukita kambi jijini Arusha ili kujiandaa na mbilinge mbilinge za duru ya pili ya Ligu kuu ya NBC Tanzania bara, ambapo imepanga kucheza michezo miwili ya kirafiki kujiandaa na michezo ya Ligi kuu, Dodoma Jiji itaanza kuzisaka alama tatu mbele ya Pamba Jiji katika uwanja wa Jamhuri Dodoma Februari 05, 2025. Akizungumzia kambi hiyo Mtendaji Mkuu wa Dodoma Jiji FC, Johnson Fourtnatus alisema “ Tumekubaliana kwenda kuweka kambi mkoani Arusha kwa muda wa siku sita, na tutacheza michezo miwili ya kirafiki na timu zinazoshiriki Ligi daraja la kwanza Tanzania bara, tukianzia kesho ambapo tutacheza na Mbuni FC, na tarehe 31 tutacheza mchezo wa mwisho wa kirafiki kukamilisha kambi yetu na tarehe 2 Februari, 2025 timu itarudi Dodoma kuendelea na kambi kuelekea mchezo dhidi ya Pamba Jiji FC ". Katika hatua nyingine Fourtnatus akaweka wazi mpango mkakati wa klabu ya Dodoma Jiji FC, katika duru ya pili ya Ligi kuu ...