Posts

Showing posts from August, 2023

CCM CHANG’OMBE YAMPONGEZA DIWANI FUNDIKILA KUBORESHA HUDUMA ZA JAMII

Image
Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chang’ombe kimempongeza Diwani wa kata hiyo Bakari Fundikila kwa kuhakikisha huduma za kijamii zinawafikia wananchi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe. Wananchi wakifuatilia mkutano wa hadhara Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy katika mkutano wa hadhara uliofanyika Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Hamvi jijini Dodoma. Iddy alisema kuwa Kata ya Chang’ombe inapiga hatua ya maendeleo kwa kasi kutokana na Diwani wake kusimamia maendeleo. “Maendeleo haya tunayoyaona ni baada ya Diwani kusimama na kuizungumzia na kuitetea Chang’ombe. Mheshimiwa Diwani umekwenda kufanya harakati za namna gani wananchi wa Kata ya Chang’ombe wanaenda kupata huduma bora za kijamii. Leo tumekuwa na Kituo cha Afya Chang’ombe ambacho ni kituo cha mfano kwa ubora wa majengo, ukubwa wa eneo na huduma. Pale kuna jengo la mama na mtoto na huduma za upasuaji mdogo zitapelekwa” alisema Iddy. Diw...

CCM CHANG’OMBE YAPONGEZA MPANGO WA ULINZI KATIKA MITAA

Image
Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chang’ombe kimepongeza mipango ya ulinzi na usalama katika mitaa ya kata hiyo na kuitaja kuwa ni mizuri. Mwenyekiti wa CCM Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy alipokuwa akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Hamvu jijini Dodoma. Iddy alisema “mipango yenu kwenye ulinzi na usalama ndani ya mitaa ni mizuri. Lakini pia, mipango yenu ya kuishi na wananchi ndani ya mitaa nayo ni mizuri. Wenyeviti wa mitaa nawashukuru sana kwa hilo. Vilevile, nawashukuru watendaji wetu ngazi ya kata, Mtendaji wa Kata, Afisa Maendeleo ya Jamii Kata, Afisa Ustawi wa Jamii Kata, Mratibu wa Elimu Kata, Afisa Afya Kata na wataalamu wote mnafanya kazi nzuri, kwa sababu leo Kata ya Chang’ombe ina sifa, mmeboresha mifumo ya vikundi vya ujasiriamali. Kila mtaa tumepita kuna vikundi vinavyopokea mikopo ndani ya Halmashauri yet...

CHANG’OMBE WAJIVUNIA UJENZI KITUO CHA POLISI

Image
  Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE WANANCHI wa Kata ya Chang’ombe wanajivunia mradi wa ujenzi wa Kituo cha Polisi katika kata yao jambo litakaloondoa uhalifu na kuwahakikishia usalama wao na mali zao. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy alipokuwa akiongea na wanachama wa CCM na wananchi wa Kata ya Chang’ombe katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Hamvu jijini Dodoma. Iddy alisema kuwa Diwani wa Kata ya Chang’ombe, amekuwa akiipambania kata hiyo katika miradi mbalimbali ya maendeleo. “Ndugu wanachama wa CCM na wananchi, Diwani wenu Bakari Fundikila amekwenda kusimamia mradi wa ujenzi wa Kituo cha Polisi Chang’ombe. Kituo kile takwimu zinaonesha baada ya Makao Makuu ya Polisi Wilayaya Dodoma, kinachofuata ni kituo hiki cha Polisi Chang’ombe. Na tumemsikia Diwani hapa amesema kituo hiki mmekijenga wanachama wa CCM na ...

USALAMA MTAA WA MAZENGO NI SHWARI

Image
Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE HALI ya ulinzi na usalama katika Mtaa wa Mazengo ni shwari na wananchi wanaendelea kutekeleza shughuli za maendeleo. Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Mazengo, Godfrey Nkinda akisoma taarifa ya Mtaa Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Mazengo, Godfrey Nkinda alipowasilosha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Mazengo. Nkinda alisema kuwa hali ya ulinzi na usalama katika Mtaa wa Mazengo uliyopo Kata ya Chang’ombe ni shwari. “Uongozi wa serikali ya Mtaa wa Mazengo umekuwa ukishirikiana na Jeshi la Polisi kuhakikisha mtaa unakuwa salama. Polisi wamekuwa wakikabiliana na matukio madogomadogo ambayo ni viashiria vya uhalifu. Jeshi la Polisi kupitia Polisi kata na jamii wamekuwa wakifanya doria na misako ili kubaini maeneo chochezi ambayo ni vijiwe vya kuvutia bangi hasa maeneo ya Mapagale jambo ambalo Polisi wamefanikiwa kulipunguza na kazi ya kukabiliana na hali hiyo bado inaendelea” a...

DIWANI FUNDIKILA APONGEZWA UWEKEZAJI SOKO LA HAMVU

Image
Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE DIWANI wa Kata ya Chang’ombe, Bakari Fundikila amepongezwa kwa jitihada zake za kuwaletea maendeleo wananchi wa kata hiyo ikiwa ni pamoja na uwekezaji katika Soko la Hamvu. Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Hamvu jijini Dodoma. Iddy alisema “tunaendelea kumshukuru Diwani Bakari Fundikila kwa kufanya uwekezaji mkubwa katika Soko la Hamvu, tayari ametufahamisha kuwa kiasi cha shilingi 20,000,000 zipo tayari katika akaunti ya kata kwa ajili ya ujenzi wa soko hilo. Jitihada zote hizo anazifanya kwa kushirikiana na Mheshimiwa Athony Mavunde ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini. Huyu ndugu yetu Mbunge lazima tumwangalie kwa macho yote mawili kwasababu amejitoa katika kada zote ikiwemo elimu, michezo, afya na maendeleo. Sasa, maendeleo yote haya...

WAZAZI MTAA WA MAZENGO WASHAURIWA KULEA WATOTO KATIKA MAADILI

Image
  Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE WAZAZI wa Mtaa wa Mazengo Kata ya Chang’ombe wametakiwa kijikita katika malezi ya watoto ili wawe na maadili mema yatakayowawezesha kuwa raia wema na wawajibikaji katika jamii. Afisa Ustawi wa Jamii wa Kata ya Chang’ombe, Debora Kanuya Kauli hiyoilitolewa na Afisa Ustawi wa Jamii wa Kata ya Chang’ombe, Debora Kanuya alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa Mazengo kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kufanyika katika Ofisi ya CCM Tawi la Chang’ombe Magharibi jijini Dodoma. Kanuya alisema “ninawaomba sana akina mama wa Mtaa wa Mazengo, tuwe na maneno mazuri kwa watoto wetu ili watoto wanapokuwa wawe wanafahamu maneno mazuri, wasiwe na maneno ya matusi na maneno ya mtaani. Lakini pia kuna baadhi ya akina mama ambao wamekuwa wakipiga sana watoto wao na kutoa lugha ya matusi. Unakuta baadhi ya kina mama wametelekezwa kwa hiyo zile hasira za kutelekezwa wanazihamishia kwa watoto, huo ni ukatili. Niwaombe sana wanawake...

MALEZI YA WATOTO YANAMCHANGO KATIKA USALAMA KATA YA CHANG’OMBE

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA AMANI na usalama wa Kata ya Chang’ombe inatokana na jinsi jamii inavyowalea watoto katika misingi bora na maadili mema. Kaimu Afisa Mtendaji wa Kata ya Chang’ombe, Daria Kapinga akiongea na wananchi Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Afisa Mtendaji wa Kata ya Chang’ombe, Daria Kapinga alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa Mazengo kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chama Cha Mapinduzi na kufanyika katika Ofisi ya CCM Tawi la Chang’ombe Magharibi. Kapinga alisema “ninatamani kuzungumza na mitaa miwili Mazengo pamoja na Msamalia suala la amani na ulinzi. Mitaa yetu imekuwa ni mitaa ambayo inatajwa sana kwenye sifa mbalimbali. Lakini chanzo nilichobaini ni kutoka kwenye mizizi ambapo ni kwa watoto wetu, kwenye malezi ya watoto wetu tumeshindwa kuidumisha amani, tumeshindwa kudumisha ulinzi kwa sababu ya malenzi tuliyonayo kwa watoto wetu. Malezi yasiyo mema kwa watoto matokeo yake ya muda mrefu yanapelekea kwenye uvunjifu wa amani na usalama”   ...

WANANCHI MAZENGO WATAKIWA KULEA WATOTO KATIKA MAADILI

Image
  Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE JAMII imetakiwa kuwalea watoto katika maadili mema ili kuwa na taifa imara lenye watu wawajibikaji. Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Hamasa na Chipukizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma, Nasra Seif alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa Mazengo kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na CCM na kufanyika katika Ofisi ya CCM Tawi la Chang’ombe Magharibi. Seif alisema “ndugu zangu tukiwalea watoto wetu katika maadili, tutakuwa na taifa ambalo ni imara lenye watu wanaowajibika ipasanyo. Siku hizi kumekuwa na tatizo kubwa sana la ukatili wa kijinsia kwa watoto. Twende tukawalee watoto kwa maadili na nidhamu. Kumbukeni alivyosema Afisa Mtendaji wetu wa Kata, Chang’ombe haitakuwa Chang’ombe ya matukio ya uhalifu, twende tukajifunze kutoka kwa wenzetu wa huko. Isionekane kama Chang’ombe ni sehemu ya watu ambao wameshindikana, hatutaki kuona ‘defender’ za Polisi zikipita Chang’ombe mara kw...

COSTECH YAFADHILI MIRADI YA UTAFITI KUHUSU SOMO LA HISABATI

Image
Na Janeth Raphael - MichuziTv - Dodoma. TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imefadhili miradi miwili wenye thamani ya Sh.milioni 120 kwa kila mradi kwa lengo la kufanya utafiti katika somo la hisabati kutokana na matokeo mabaya ya somo hilo katika mtihani wa darasa la saba na kidato cha nne. Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt.Amos Nungu Akizungumza leo Agosti 25,2023 na waandishi wa habari jijini Dodoma Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu amesema  imeidhinisha miradi miwili kwa thamani ya Sh.milioni 120 kila mradi na utekelezaji wa mradi unahusisha watafiti kutoka vyuo mbalimbali hapa nchini. Amefafanua mradi utafanyika katika kipindi cha miaka miwili na hatua iliyopo sasa ni kusaini mikataba. "Somo la hisabati bado ni changamoto kwani matokeo yake yamekuwa mabaya kwa kidato cha nne na darasa la saba. " Hivyo kwa kuondoa tatizo hilo  Tume tumeidhinisha miradi miwili ambayo kila mmoja thamani yake ni Sh.milioni 120,"amesema na kuongeza miradi m...

RAIS SAMIA AZUNGUMZA KWENYE MKUTANO WA 15 WA BRICS UNAOFANYIKA JOHANNESBURG NCHINI AFRIKA KUSINI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Iran Mhe. Dkt. Seyyed Ebrahim Raisi kabla ya kuanza mazungumzo kando ya mkutano wa 15 wa BRICS unaofanyika Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Iran Mhe. Dkt. Seyyed Ebrahim Raisi kabla ya kuanza mazungumzo kando ya mkutano wa 15 wa BRICS unaofanyika Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisoma hotuba yake kwenye Mkutano wa 15 wa BRICS unaofanyika Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini

TRA YAZINDUA KAMPENI KUELEZEA UMUHIMU RISITI ZA MASHINE ZA EFD

Image
Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV MENEJA wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa kikodi Kinondoni mkoani Dar es Salaam, Husna Nyange amesema kodi sahihi inatokana na kumbukumbu sahihi za kikodi hivyo amewahimiza wafanyabiashara kutoa risiti kila wanapofanya mauzo. Pia na wanunuzi kudai risiti sahihi za EFD kila wanaponunua bidhaa au kupata huduma lengo likiwa kila mmoja kwa nafasi yake anatunza kumbukumbu zake. Nyange ameyasema hayo leo wakati wa uzinduzi wa mabango ya uhamasishaji kuhusu matumizi sahihi ya EFD. Hivyo pamoja na mambo mengine ameelezea umuhimu wa wafanyabiashara kuwa na kumbukumbu sahihi za kikodi hivyo lakini wanunuzi nao ni vema wakajenga utamaduni wa kudai risiti kutoka kwa wafanyabiashara. Kwa upande wake Meneja Msaidizi wa Huduma kwa Mlipakodi Mkoa wa kikodi Kinondoni Emanuel Lucian Dafay amesema kampeni hiyo ya EFD ni endelevu na kwa mkoa wa Kinondoni walianza kwa kutuma ujumbe mfupi (sms) kwa wafanyabiashara kupitia simu zao za mkononi. Amefafanu leng...

MENEJIMENTI YA TANESCO YARIDHISHWA NA UJENZI WA MRADI WA BWAWA LA KUFUA UMEME WA JULIUS NYERERE (JNHPP)

Image
  Na Neema Mbuja, Rufiji Timu ya Menejimenti ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) imetembelea mradi wa Bwawa la Julius Nyerere JNHPP huku ikieleza madhumuni ya ziara hiyo ikiwemo kufanya tathimini ya mwenendo wa ujenzi wa mradi unaokaribia asilimia 91 ifikapo Agosti mwishoni. Lengo jingine la ziara hiyo ni kuangalia mwenendo wa ujenzi wa mradi na tathimini ya hali ya mvua za vuli zinazotarajiwa kunyesha kati ya Oktoba hadi Disemba kama ilivyotangazwa na Mamlaka ya Utabiri wa Hali ya Hewa Tanzania (TMA).Timu hiyo imeongozwa na Mkurugenzi mkuu wa Tanesco Maharage Chande. Akizungumza na waandishi wa habari, Chande amesema maendeleo ni mazuri hadi Julai tulifikia asilimia 90 na tunatarajia mwishoni mwa Agosti tutafikia asilimia 91 huku akiwapongeza wahandisi na wafanyakazi wa shirika hilo wanaosimamia mradi huo.   Amesema ukamilikaji wa mradi huu utatuwezesha kushinda mashindano haya kwa kuwa na umeme wa uhakika utakaokidhi mahitaji ya uchumi. Amesema timu ya menejim...

MTENDAJI MKUU TARURA AZUNGUMZIA UTEKELEZAJI, MAJUKUMU NA MWELEKEO WA WAKALA HIYO MWAKA WA FEDHA 2023/24

Image
  YALIYOJIRI LEO WAKATI MTENDAJI MKUU WA WAKALA YA BARABARA ZA VIJIJINI NA MIJINI (TARURA), MHANDISI VICTOR SEFF AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU WA WAKALA HIYO NA MWELEKEO WAKE KATIKA MWAKA WA FEDHA 2023/24 Mtendaji Mkuu wa TARURA, Eng. Victor Seff akiongea na wanahabari #Jukumu kubwa la TARURA ni kusimamia ujenzi, ukarabati na matengenezo ya mtandao wa barabara za Wilaya. Serikali ya Awamu ya Sita imeiongezea TARURA bajeti yake mara tatu zaidi ikiwa ni kuendeleza juhudi za Awamu zilizopita za kuboresha barabara za vijini. #Kwa sasa TARURA ipo kwenye utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Pili toka kuanzishwa kwake mwaka 2017 ikiwa na lengo kuwa, ifikapo mwaka 2025 angalau asilimia 85 ya barabara za Wilaya ziwe zinapitika kwa misimu yote. #Lengo hilo linaakisi kaulimbiu ya TARURA Mpango Mkakati wa Pili inayosema "TARURA tunakufungulia barabara kufika kusikofikika." #Mtandao wa barabara za Wilaya chini ya TARURA una jumla ya kilomita 144,429...