CCM CHANG’OMBE YAPONGEZA MPANGO WA ULINZI KATIKA MITAA

Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chang’ombe kimepongeza mipango ya ulinzi na usalama katika mitaa ya kata hiyo na kuitaja kuwa ni mizuri.

Mwenyekiti wa CCM Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy


Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy alipokuwa akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Hamvu jijini Dodoma.

Iddy alisema “mipango yenu kwenye ulinzi na usalama ndani ya mitaa ni mizuri. Lakini pia, mipango yenu ya kuishi na wananchi ndani ya mitaa nayo ni mizuri. Wenyeviti wa mitaa nawashukuru sana kwa hilo. Vilevile, nawashukuru watendaji wetu ngazi ya kata, Mtendaji wa Kata, Afisa Maendeleo ya Jamii Kata, Afisa Ustawi wa Jamii Kata, Mratibu wa Elimu Kata, Afisa Afya Kata na wataalamu wote mnafanya kazi nzuri, kwa sababu leo Kata ya Chang’ombe ina sifa, mmeboresha mifumo ya vikundi vya ujasiriamali. Kila mtaa tumepita kuna vikundi vinavyopokea mikopo ndani ya Halmashauri yetu. Hizi ni kazi nzuri zinazoongozwa na Ofisi ya Mtendaji wa Kata”.

Mwenyekiti huyo alipongeza taatifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika mitaa. “Nawashukuru sana watendaji wote wa mitaa kwa kuandaa taarifa zenu nzuri zenye tija ambayo inatuonesha mipango yenu yote mnayoifanya katika mitaa yenu. Na hii ndiyo sifa kubwa ya CCM kujivunia elimu bora, siasa safi inayoendeshwa katika vyuo vyetu. Hali kadhalika, kupata wataalamu wazuri ambao wanakuja kusimamia ndani ya mitaa yetu” alisema Iddy.



Mwananchi Jasmin Abdallah alisema kuwa ana imani wa watedanji kutokana na kuwa wapya na kusema kuwa watawasaidia katika kutatua changamoto zinazowakabili.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma