DIWANI FUNDIKILA APONGEZWA UWEKEZAJI SOKO LA HAMVU

Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE

DIWANI wa Kata ya Chang’ombe, Bakari Fundikila amepongezwa kwa jitihada zake za kuwaletea maendeleo wananchi wa kata hiyo ikiwa ni pamoja na uwekezaji katika Soko la Hamvu.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy


Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Hamvu jijini Dodoma.

Iddy alisema “tunaendelea kumshukuru Diwani Bakari Fundikila kwa kufanya uwekezaji mkubwa katika Soko la Hamvu, tayari ametufahamisha kuwa kiasi cha shilingi 20,000,000 zipo tayari katika akaunti ya kata kwa ajili ya ujenzi wa soko hilo. Jitihada zote hizo anazifanya kwa kushirikiana na Mheshimiwa Athony Mavunde ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini. Huyu ndugu yetu Mbunge lazima tumwangalie kwa macho yote mawili kwasababu amejitoa katika kada zote ikiwemo elimu, michezo, afya na maendeleo. Sasa, maendeleo yote haya yatafanyika ikiwa tutawaunga mkono. Ndugu zangu twendeni tukashirikiane. Chama Cha Mapinduzi kinataka kukuza maendeleo katika maeneo yake, lakini sisi wananchi na wanachama tuwe tayari kuunga mkono”.

Nasrat Mussa mkazi wa Hamvi alisema kuwa ujenzi wa soko la Hamvu utaongeza wigo kwa wananchi kufanya biashara zao sehemu rasmi tofauti na wanavyofanya sasa.

MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma