WANANCHI MAZENGO WATAKIWA KULEA WATOTO KATIKA MAADILI
Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE
JAMII imetakiwa kuwalea watoto katika
maadili mema ili kuwa na taifa imara lenye watu wawajibikaji.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara |
Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Hamasa
na Chipukizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma, Nasra Seif
alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa Mazengo kwenye mkutano wa hadhara
ulioandaliwa na CCM na kufanyika katika Ofisi ya CCM Tawi la Chang’ombe Magharibi.
Seif alisema “ndugu zangu tukiwalea
watoto wetu katika maadili, tutakuwa na taifa ambalo ni imara lenye watu wanaowajibika
ipasanyo. Siku hizi kumekuwa na tatizo kubwa sana la ukatili wa kijinsia kwa
watoto. Twende tukawalee watoto kwa maadili na nidhamu. Kumbukeni alivyosema
Afisa Mtendaji wetu wa Kata, Chang’ombe haitakuwa Chang’ombe ya matukio ya
uhalifu, twende tukajifunze kutoka kwa wenzetu wa huko. Isionekane kama
Chang’ombe ni sehemu ya watu ambao wameshindikana, hatutaki kuona ‘defender’ za
Polisi zikipita Chang’ombe mara kwa mara kwa ajili ya uhalifu. Tumemsikia Afisa
Ustawi wa Jamii wa Kata ya Chang’ombe alivyotoa elimu nzuri ya malezi ya
watoto, tubadilike kuanzia sasa”.
Akiongelea umuhimu wa CCM kufanya ziara
hizo, alisema kuwa ni utekelezaji wa maagizo ya Mwenyekiti wa CCM Taifa. “Ziara
hii imefanyika si kwa bahati mbaya, Mwenyekiti wa CCM Taifa, Mama Samia Suluhu
Hassan siku ya Mkutano Mkuu wa CCM Taifa alielekeza wanachama kwa ngazi zote
waende kuhoji utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Watu wa Serikali kwa
maana ya watendaji wa kata na mitaa, maafisa wote pamoja na wakuu wa divisheni
waende wakawaeleze wananchi juu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ili
tukirudi kwenye uchaguzi mkuu sisi kama Chama Cha Mapinduzi ambacho kinaomba
ridhaa kwa wananchi tusiwe tuna maswali mengi ya kujibu kutoka kwa wapiga kura
wetu” alisema Seif.
MWISHO
Comments
Post a Comment