CCM CHANG’OMBE YAMPONGEZA DIWANI FUNDIKILA KUBORESHA HUDUMA ZA JAMII
Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE
CHAMA
Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chang’ombe kimempongeza Diwani wa kata hiyo Bakari Fundikila
kwa kuhakikisha huduma za kijamii zinawafikia wananchi ikiwa ni pamoja na
ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe.
Wananchi wakifuatilia mkutano wa hadhara |
Pongezi
hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Chang’ombe, Bashir Iddy katika
mkutano wa hadhara uliofanyika Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Hamvi jijini
Dodoma.
Iddy
alisema kuwa Kata ya Chang’ombe inapiga hatua ya maendeleo kwa kasi kutokana na
Diwani wake kusimamia maendeleo. “Maendeleo haya tunayoyaona ni baada ya Diwani
kusimama na kuizungumzia na kuitetea Chang’ombe. Mheshimiwa Diwani umekwenda
kufanya harakati za namna gani wananchi wa Kata ya Chang’ombe wanaenda kupata
huduma bora za kijamii. Leo tumekuwa na Kituo cha Afya Chang’ombe ambacho ni
kituo cha mfano kwa ubora wa majengo, ukubwa wa eneo na huduma. Pale kuna jengo
la mama na mtoto na huduma za upasuaji mdogo zitapelekwa” alisema Iddy.
Diwani Bakari Fundikila akiongea na wananchi |
Mwanaidi
Jamal, mkazi wa Chang’ombe alisema kuwa ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe ni
suluhisho la tiba kwa wananchi. “Kabla ya kujengwa kwa Kituo cha Afya
Chang’ombe ilikuwa lazima kufunga safari kwenda mjini kufuata huduma za afya”
alisema Jamal.
MWISHO
Comments
Post a Comment