Jiji la Dodoma kuchangamkia fursa ujio wa Bandari Kavu Ihumwa
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula apongeza Mkakati wa Uendelezaji Bandari Kavu na kuahidi kujipanga kuhakikisha wafanyabiashara wadogo wanapata fursa ya kufanya biashara katika eneo hilo na kuchochea ukuaji wa uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla. Akizungumza katika ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwenye Bandari Kavu Ihumwa iliyokuwa na lengo la kujiridhisha na mkakati wa uendelezaji wa miundombinu hiyo, alisema kuwa uongozi wa jiji utakaa kikao na kutathmini namna ya kuandaa mazingira rafiki ya biashara ili kuwawezesha wajasiriamali wa ndani kushiriki kikamilifu katika shughuli za upokeaji, uhifadhi na usafirishaji wa mizigo. Alieleza kuwa pamoja na fursa za moja kwa moja zitakazotokana na shughuli za bandari hiyo, jiji pia linatarajia kuimarisha sekta ya usafirishaji, uhudumu na biashara ndogondogo hivyo kuongeza ajira na kipato kwa wananchi. Aidha, Mstahiki Meya Chaula aliongeza kuwa jiji litafanya utaratibu wa kufanya mazungumzo na Mam...