Posts

Showing posts from July, 2024

Sekondari Zuzu yapongezwa na CCM Mkoa

Image
  Na. Dennis Gondwe, ZUZU KAMATI ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma imewashukuru walimu wa Shule ya Sekondari Zuzu kwa kazi ya ufundishaji na kusimamia ujenzi na uboreshaji wa miundombinu shuleni hapo. Shukrani hizo zilitolewa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Donald Mejiti alipoongoza Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Dodoma kutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba nane na matundu 10 ya vyo Shule ya Sekondari Zuzu. Mejiti alisema “nianze kwa kutoa pongezi kwa kazi nzuri mliyofanya na inaonekana. Walimu wetu tunawashukuru sana kwa kazi ya kufundisha wanafunzi na kusimamia ujenzi wa miundombinu katika shule hii. Nia ya mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kujenga majengo haya ni kuwawezesha watoto wetu wasome katika mazingira bora na salama. Watoto wetu wakisoma fursa za ajira zinakuwa nyingi. Lakini pia amejenga vyuo vya VETA ili kuongeza wigo kwa watoto wetu, bahati nzuri VETA ada yake ni nafuu sana”. Aidha, alimpongeza Mkurugenzi wa Halm...

CCM yawapongeza walimu Zuzu Sec

Image
Na. Dennis Gondwe, ZUZU KAMATI ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma imewashukuru walimu wa Shule ya Sekondari Zuzu kwa kazi ya ufundishaji na kusimamia ujenzi na uboreshaji wa miundombinu shuleni hapo. Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Donald Mejiti akisisitiza jambo Shukrani hizo zilitolewa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Donald Mejiti alipoongoza Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Dodoma kutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba nane na matundu 10 ya vyo Shule ya Sekondari Zuzu. Mejiti alisema “nianze kwa kutoa pongezi kwa kazi nzuri mliyofanya na inaonekana. Walimu wetu tunawashukuru sana kwa kazi ya kufundisha wanafunzi na kusimamia ujenzi wa miundombinu katika shule hii. Nia ya mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kujenga majengo haya ni kuwawezesha watoto wetu wasome katika mazingira bora na salama. Watoto wetu wakisoma fursa za ajira zinakuwa nyingi. Lakini pia amejenga vyuo vya VETA ili kuongeza wigo kwa watot...

Ukarabati Shule ya Msingi Iyumbu kupunguza msongamano darasani

Image
Na. Dennis Gondwe, IYUMBU MRADI wa ukarabati wa vyumba 10 vya madarasa katika Shule ya Msingi Iyumbu umesaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi darasani na kuwaboreshea wanafunzi mazingira bora ya kujifunzia. Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Iyumbu, Mwl. Monica Nshimba Kauli hiyo ilitolewa na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Iyumbu, Mwl. Monica Nshimba alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ukarabati wa vyumba 10 vya madarasa katika Shule ya Msingi Iyumbu kwa Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma ilipotembelea shule hiyo iliyopo Kata ya Iyumbu jijini Dodoma. Mwl. Nshimba alisema “ukarabati wa mradi umepunguza kwa kiasi kikubwa msongamano wa wanafunzi darasani kwasababu kabla ya ukarabati, kulikuwa na vyumba vinne ambavyo vilikuwa havitumiki kabisa na hata vile vilivyokuwa vinatumika vilikuwa katika hali mbaya sana. Hivyo, kwa sasa vyumba vyote vinatumika. Pia mazingira ya kujifunzia na kufundishia yamekuwa mazuri na rafiki kiasi kwamba wanafunzi na walimu wote...

Kituo cha Afya Ilazo kuboresha huduma ya mama na mtoto

Image
Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI MRADI wa ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo utawezesha kutoa huduma za upasuaji, kliniki ya mama na mtoto na huduma za kujifungua zikiwa zimeunganishwa na mfumo wa hewa ya Oksijeni. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Revocatus Baltazary alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo kwa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Dodoma ilipotembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Dkt. Baltazary alisema “m radi huu utawezesha kutoa huduma za upasuaji , kliniki ya mama na mtoto, huduma za kujifungua, wodi ya watoto wachanga , huduma za kuhifadhi miili . Wodi hizi pia zimeunganishwa na mifumo ya hewa ya Oksijeni ambayo ipo katika wodi ya wazazi, watoto na jengo la upasuaji. Mifumo hii itasaidia wagonjwa wote wenye changamoto ya upumuaji kupata huduma hapa kituoni.   Aidha, huduma za lishe zitatolewa ikiwemo elimu juu ya masuala ya lishe, upimaji wa hali za lishe na ushauri”. ...

Hospitali ya Wilaya ya Dodoma kusogeza huduma kwa wananchi

Na. Dennis Gondwe, NALA Halmashauri ilianza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma kwa lengo la kusogeza huduma za afya kwa wananchi ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Revocatus Baltazary alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma mbele ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma. Dkt. Baltazary alisema “kutokana na changamoto ya kukosa hospitali ya wilaya kwa muda mrefu na changamoto ya umbali wa kupata huduma za afya kwa ngazi ya wilaya, halmashauri na serikali kuu iliamua kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma ili kusogeza huduma kwa wananchi. Hatua hii itawezesha wananchi kupata huduma za afya kwa ngazi ya wilaya”. Akiongelea mapokezi ya fedha, alisema kuwa serikali kuu ilitoa kiasi cha shilingi 1,500,000,000 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo. “Awamu ya kwanza halmashauri ilipokea kiasi cha shilingi 1,000,0...

Hospitali ya Wilaya ya Dodoma kuboresha huduma za Afya

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Halmashauri ilianza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma kwa lengo la kusogeza huduma za afya kwa wananchi ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kaimu Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Revocatus Baltazary akisoma taarifa ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Revocatus Baltazary alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma mbele ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma. Dkt. Baltazary alisema “kutokana na changamoto ya kukosa hospitali ya wilaya kwa muda mrefu na changamoto ya umbali wa kupata huduma za afya kwa ngazi ya wilaya, halmashauri na serikali kuu iliamua kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma ili kusogeza huduma kwa wananchi. Hatua hii itawezesha wananchi kupata huduma za afya kwa ngazi ya wilaya”. Akiongelea mapokezi ya fedha, alisema kuwa serikali kuu ilitoa kiasi cha shi...

CCM yaridhishwa na miradi Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma kimeridhishwa na utendaji kazi wa serikali baada ya kutembelea na kukagua miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya shilingi 600,424,100,099 inayotekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Donald Mejiti akiongea wakati wa majumuisho ya ziara ya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Donald Mejiti alipoongoza Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Dodoma kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   Mejiti alisema kuwa kazi iliyofanyika ni kubwa na nzuri. Alisema kuwa timu yake imetembelea na kukagua miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya shilingi 600,424,100,099 na kujiridhisha kuwa imetekelezwa kwa kiwango bora.   Aidha, alipongeza ushirikiano baina ya serikali na Chama Cha Mapinduzi kuwa ni mzuri....

Kituo cha Afya Ilazo mkombozi kwa wananchi

  Na. Mwandishi wetu MRADI wa ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo utakapokamilika utahudumia wananchi 99,743 wa Kata ya Nzuguni na maeneo ya jirani ikiwa ni mkakati wa serikali ya awamu ya sita wa kusogeza huduma za afya karibu na wananchi. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alipokuwa akisoma taarifa mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo kwa Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024. Dkt. Method alisema kuwa lengo la mradi huo ni kuboresha huduma za mama na mtoto na huduma za upasuaji ukitarajiwa kuhudumia zaidi ya wananchi 99,743 wa Kata ya Nzuguni, Ipagala na maeneo menginge watapata huduma bora za afya mradi huo utakapokamilika. Akiongelea mafanikio ya mradi huo, aliyataja kuwa ni kuwezesha kutoa huduma za upasuaji, kliniki ya mama na mtoto, huduma za kujifungua, wodi ya watoto wachanga , huduma za kuhifadhi miili. Mafanikio mengine ni “wodi hizi pia zimeunganishwa na mi...

Dodoma English Medium kusomesha kwa gharama nafuu

  Na. Mwandishi wetu, MRADI wa ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi Dodoma English Medium umewasaidia wazazi wenye kipato cha kati kusomesha watoto wao katika shule ya mchepuo wa kiingereza karibu na maeneo yao kwa gharama nafuu. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prisca Myalla alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi ya Dodoma English Medium kwa Kiogozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024. Akiongelea faida za mradi huo alizitaja kuwa ni kuwasaidia wazazi wenye kipato cha kati kupata fursa ya kusomesha watoto kwenye shule ya mchepuo wa ki i ngereza . Faida nyingine aliitaja kuwa ni wananchi kusogezewa huduma ya shule karibu ambapo watoto walikuwa wanasafiri umbali mrefu kufuata huduma ya elimu pia wanafunzi wanapata elimu bora kwa gharama nafuu ukilinganisha na shule binafsi . “ Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024, m radi umelenga kutoa elimu bora amb...

BAgamoyo Garden kuipendezesha Dodoma

  Na. Mwandishi wetu, MRADI wa Bagamoyo Garden wa utunzaji na uhifadhi wa mazingira kwa njia ya upandaji miti, maua na nyasi unalenga kuunga mkono juhudi za serikali za kuifanya Dodoma kuwa ya kijani na inayopendeza. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa mradi wa Bagamoyo Garden, Rogasian Malya alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa Bagamoyo Garden wa utunzaji na uhifadhi wa mazingira kwa njia ya upandaji miti, maua na nyasi katika eneo la wazi kwa Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024. Malya alisema kuwa lengo la mradi huo ni kuunga mkono juhudi za s erikali za kuifanya Dodoma kuwa ya kijani kwa njia ya upandaji miti , k ampeni ambayo ilizinduliwa mwaka 2021 kwa kupanda miti katika chanzo cha maji Mzakwe na aliyekuwa Makamu wa Rais ambaye kwa sasa ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mhe shimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Alisema kuwa m radi hu o unatekeleza kwa vitendo ujumbe wa m bio za Mwenge wa Uhuru, 2024 usemao ‘ Tunza Mazingira na Shirik...

Mwenge wa Uhuru waweka jiwe la msingi Dodoma Media Group

  Na. Mwandishi Wetu Kituo cha vyombo vya habari cha Dodoma Media Group kutoa elimu ya mpiga kura katika kujiandaa na uchaguzi wa serikali za mitaa na utunzaji wa mazingira. Kauli hiyo ilitolewa na Mejena Mkuu wa Dodoma Media Group, Zania Miraji alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa kituo cha vyombo vya habari cha Dodoma Media Group kilichopo katika Mtaa wa Miyuji Proper jijini Dodoma kwa Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024. Miraji alisema “ kupitia vyombo vya habari vya Dodoma Media Group jamii ya Dodoma itapata haki ya upatikanaji wa taarifa na elimu juu ya masuala mbalimbali ikizingatia ujumbe wa ‘ Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa E ndelevu ’ . Elimu itakayotolewa ni pamoja na elimu ya masuala ya uchaguzi ikiwemo elimu ya mpiga kura ambapo kutakuwa na kipindi maalum cha kuelimisha Umma kujiandaa na uchaguzi wa s erikali za m itaa. Pia itatolewa elimu juu ya lishe na kutakuwa na kipindi maalum kitakachozungumzia...

Barabara ya Judiciary kupunguza msongamano katikati ya Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, TAMBUKARELI UJENZI wa barabara ya ‘Judiciary’ yenye urefu wa kilometa mbili unalenga kupunguza msongamano wa magari katikati ya Jiji la Dodoma na kuharakisha huduma kwa wananchi. Kauli hiyo ilitolewa na Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Dodoma, Mhandisi Emmanuel Mfinanga wakati akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa barabara ya Judiciary yenye urefu wa kilometa mbili kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa. Mhandisi Mfinanga alisema ”n dugu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2024, lengo la mradi huu ni kupunguza msongamano wa magari katikati ya Jiji la Dodoma, kurahisisha huduma kwa wananchi katika ofisi zilizopo katika eneo hili ambapo miongoni mwa ofisi hizo ni:- Ofisi ya Bima (NHIF), Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Wakala wa Ununuzi Tanzania (PPRA), Ofisi za Maadili ya Viongozi wa Umma na Ofisi za Mahakama Kuu ya Tanzania”.   Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Godfrey Mnzav...