Posts

Showing posts from April, 2024

RC Senyamule aagiza utengenezaji Viti uende sambamba na ujenzi wa madarasa Sekondari Mtumba

Na. Dennis Gondwe, MTUMBA MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ameagiza ujenzi wa madarasa uende sambamba ya utengenezaji wa viti na meza kwa ajili ya wanafunzi ili vyote vikamilike pamoja na kuanza kutoa huduma. Kauli hiyo aliitoa alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa madarasa nane na matundu 10 ya vyoo katika Shule ya Sekondari Mtumba iliyopo Kata ya Mtumba, Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Baada ya kukagua hatua ya ujenzi wa miundombinu hiyo alihoji hatua ya utengenezaji wa viti na meza ambao ulikuwa haujaanza. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma aliagiza utaratibu wa kutengeneza viti na meza uanze ili uende sambamba ya ujenzi wa miundombinu hiyo na kukamilika pamoja ili isicheleweshe utoaji wa huduma. Akisoma taarifa ya ujenzi wa madarasa nane na matundu 10 ya vyoo kwa ajili ya mapokezi ya wanafunzi wa kidato cha tano mwaka 2024/2025 Mkuu wa Shule ya Sekondari Mtumba, Mwl. Stephen Moshi alisema kuwa ujenzi unaendelea vizuri. “Shule ilipokea shilingi 201,000,000 tarehe 6 Ja...

RC Dodoma afurahishwa ujenzi Sekondari Mtemi Chiloloma

Na. Dennis Gondwe, HOMBOLO MAKULU MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ameagiza ujenzi wa Shule ya Sekondari Mtemi Chiloloma kusimamiwa vizuri ili ukamilike katika muda uliopangwa kwa ajili ya kutoa huduma. Agizo hilo alilitoa alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule hiyo iliyopo katika Kata ya Hombolo Makulu, jijini Dodoma. Awali akikagua ujenzi huo alieleza kufurahishwa kwake na hatua ya ujenzi wa shule hiyo. Aliwataka viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kusimamia vizuri mradi huo ili uweze kukamilika katika muda uliopangwa. Akisoma taarifa ya ujenzi wa vyumba nane vya madarasa na matundu 18 ya vyoo kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mkuu wa Shule ya Sekondari Mtemi Chiloloma, Mwl. Livinus Tanganyika alisema shule yake ilipokea shilingi 216,000,000 kutoka serikali kuu. “Ujenzi ulianza tarehe 25 Novemba, 2023 mpaka sasa ujenzi wa madarasa umekamilika kwa asilimia 100, matundu ya vyoo 18 yapo hatua ya umaliziaji, kazi inayoendelea ni kuweka mar...

Matukio katika picha ziara ya Kamati ya Fedha na Utawala kutembelea na kukagua miradi ya Maendeleo kipindi cha robo ya tatu mwaka 2023/2024

Matukio katika picha ziara ya Kamati ya Fedha na Utawala kutembelea na kukagua Miradi ya Maendeleo kipindi cha robo ya tatu mwaka 2023/2024

Matukio katika picha zoezi la kupanda miti Shule ya Msingi Amani na Dodoma Mlimani kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania lilifanywa na Divisheni ya Elimu Awali na Msingi Jiji la Dodoma

Image
 

Matukio katika picha zoezi la usafi wa Mazingira Kituo cha Afya Makole kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano lililofanywa na Divisheni ya Elimu Sekondari Jiji la Dodoma

Image
 

Elimu Sekondari yafanya usafi Kituo cha Afya Makole

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA DIVISHENI ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeadhimisha maadhimisho ya kuelekea kilele cha miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanya usafi katika Kituo cha Afya Makole kwa lengo la kuwawekea mazingira safi na salama wagonjwa wanaopata huduma kituoni hapo. Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Zainabu Abdallah akiongea na mamia ya walimu, wanafunzi na Jumuiya ya Kituo cha Afya Makole Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Zainabu Abdallah alipokuwa akiongea na mamia ya walimu, wanafunzi na jumuiya ya wafanyakazi wa Kituo cha Afya Makole kufanya usafi katika kituo hicho. Mwl. Abdallah alisema “sisi Divisheni ya Elimu Sekondari katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma tumeamua kuadhimisha maadhimisho ya kuelekea miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanya usafi katika Kituo cha Afya Makole. Kama mnavyofahamu Makole ni kituo cha ...

Matukio Dua na Sala ya Kitaifa kuliombea Taifa la Tanzania katika uwanja wa Jamhuri Dodoma

Image
 

Midahalo ya kupinga rushwa kupunguza kero kwenye jamii

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri anaendesha midahalo ya kupinga rushwa, matumizi ya dawa za kulevya na kuhamasisha haki za binadamu na utawala bora ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri Hayo yalibainishwa wakati wa salamu za mkuu huyo wa wilaya kwenye hafla ya ufunguzi wa mashindano ya mdahalo kwa shule za msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu kuhusu madhara ya rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, haki za binadamu na utawala bora katika ukumbi wa St. Gaspar, Kisasa jijini Dodoma. Alhaj Shekimweri alisema kuwa zipo haki za watu ambazo zinapotea kwa sababu na rushwa, matumizi ya dawa za kulevya na ukatili dhidi ya watoto. “Kwa maelekezo ya mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba tushughulikie kero na tunamshukuru mkuu wa mkoa ametuongoza tumeanzisha kampeni katika mkoa wake ya ‘ kero yako, wajibu wang...

Tume ya Haki za Binadamu yasisitiza utawala bora

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA TUME ya Haki za Binadamu na Utawala bora ina dhamira kuona watanzania wanaheshimu haki za binadamu na misingi ya utawala bora na utu wa mtu. Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora, Dkt. Thomas Masanja Kauli hiyo ilitolewa na Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora, Dkt. Thomas Masanja alipokuwa akitoa salamu za tume hiyo katika hafla ya kufungua mashindano ya mdahalo kwa shule za msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu kuhusu madhara ya rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, haki za binadamu na utawala bora katika ukumbi wa St. Gaspar Kisasa jijini Dodoma. Dkt. Masanja alisema “tunashiriki katika shughuli hii inayohusisha wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo kwa sababu dira ya tume ni kuona jamii yenye utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu na misingi ya utawala bora na utu wa mtu. Tunataka mwisho wa siku jamii ya kitanzania inaheshimu haki za binadamu, utu wa mtu na misingi ya utawala bora”. Akiongelea ushir...

Takukuru kuwajengea moyo wa uzalendo vijana

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ilianzisha klabu za kuzuia na kupambana na rushwa katika shule za msingi, sekondari na vyuo kwa ajili ya kuwajengea moyo wa uzalendo na uadilifu. Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Dodoma, John Joseph  Kauli hiyo ilitolewa na Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Dodoma, John Joseph alipotoa salamu wakati wa hafla ya kufungua mashindano ya mdahalo kwa shule za msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu kuhusu madhara ya rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, haki za binadamu na utawala bora katika ukumbi wa St. Gaspar Kisasa jijini Dodoma. Kamanda Joseph alisema “lengo la kuanzishwa klabu za kupinga rushwa ni kuwajengea moyo wa uzalendo vijana, kuwajenga katika uadilifu na kuongeza uelewa katika makosa na ubaya wa rushwa, kuwajengea uthubutu na ushiriki wao katika kuzuia na kupambana na rushwa. Uanzishwaji wa klabu hizo ulitokana na Takukuru kuamini kwamba vijana katika taifa ni rasilimali muhimu na chimbuko la ma...

Mikopo ya Makundi Maalum kurejeshwa Julai, 2024

Image
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kurejesha utoaji wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu utakaoanza Julai, 2024. Akiwasilisha bungeni utekelezaji wa bajeti ya Mwaka 2023/24 na makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka 2024/25, Mchengerwa mikopo hiyo itaanza kwa utaratibu wa kutumia benki kwa halmashauri 10 za majaribio ambazo ni Dar  es Salaam, Dodoma, Kigoma Ujiji na Songea, Miji ya Newala na Mbulu, Wilaya za Siha, Nkasi, Itilima na Bumbuli. Aidha, alisema halmashauri 174 zilizobaki zitatumia utaratibu ulioboreshwa ili kuondoa mapungufu yaliyosababisha changamoto za awali kwa kufanya mambo yafuatayo; uanzishwaji wa kitengo cha usimamizi wa mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika Ofisi ya Rais – TAMISEMI, na uanzishwaji wa kamati za usimamizi wa mikopo katika ngazi za ofisi za wakuu wa mikoa, halmashauri na kata. “M...

Vipaumbele 13 vya mageuzi elimu msingi na sekondari 2024/2025

Image
OFISI ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa mwaka 2024/25 imepanga kutumia shilingi trilioni 1.02 ili kutekeleza vipaumbele 13 kwenye sekta ya elimu vinavyolenga kusimamia na kuendesha elimu msingi na Sekondari. Akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka huo, Waziri wa Nchi, TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa alisema fedha hizo zitajenga  vyumba vya madarasa 6,357, matundu ya vyoo 1,482, umaliziaji wa mabwalo 362 kati ya mabwalo hayo 15 ni msingi na 347 ni ya sekondari na umaliziaji mabweni 36 kwenye shule za awali na msingi. Pia alisema shule mpya 184, nyumba za walimu 184 na mabweni 186 katika shule za sekondari yatajengwa, sambamba na ununuzi wa vifaa vya TEHAMA kwenye shule za awali tatu, msingi 400 na shule za sekondari 500, ununuzi wa kemikali za maabara katika shule mpya 234. Mchengerwa alisema fedha hizo zitatumika katika utoaji wa ruzuku ya elimu bila ada kwa shule za msingi 17,986 na sekondari 4,894; ununuzi na usambazaji wa vita...

Watanzania watakiwa kupambana na rushwa na dawa za kulevya

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WATANZANIA wametakiwa kushikamana na kupambana na rushwa, dawa za kulevya na uvunjifu wa haki za binadamu ili kujenga jamii iliyo bora. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora, George Simbachawene Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora, George Simbachawene alipokuwa akifungua mashindano ya mdahalo kwa shule za msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu kuhusu madhara ya rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, haki za binadamu na utawala bora katika ukumbi wa St. Gaspar Kisasa jijini Dodoma. Waziri Simbachawene alisema “baada ya watu kuwa wanashiba, elimu wanatapa kila kitu kinaenda vizuri, wanatazama televisheni wamepata ‘exposure’ mambo ni mazuri wameibuka maadui wengine. Maadui hao ni rushwa, dawa za kulevya na uvunjifu wa maadili na haki za binadamu, hao maadui watatu ni maadui wabaya sana, ni wajibu wa kila mmoja tushirikiane kupambana na maadui hao wa...

Shilingi Bilioni 1.5 kujenga Hospitali ya Wilaya Dodoma

Image
  Na. Dennis Gondwe, DODOMA SERIKALI imetoa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma katika jitihada za kusogeza huduma bora za afya karibu zaidi na wananchi. Moja ya majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwa kipindi cha miaka mitatu kwa waandishi wa habari ofisini kwake jijini hapa. Dkt. Method alisema “tunapoongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwa kipindi cha miaka mitatu, mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma. Na hiyo hospitali ya wilaya ipo kimkakati kabisa, inajengwa eneo la Kata ya Nala. Ni eneo ambalo linaweza kufikiwa na rufaa ya vituo vyote vya afya ambavyo vinapitiwa na barabara ya mzunguko ‘ring road’. Kwa hiyo utaona hii barabara ya mzunguko inae...

Jiji la Dodoma lajenga vituo 8 vya Afya miaka 3 ya SSH

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeshuhudia ongezeko kubwa la ujenzi wa vituo vya afya nane katika serikali ya awamu ya sita inayolenga kuongeza miundombinu na kusogeza huduma za afya karibu na wananchi. Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method akielezea mafanikio ya divisheni yake Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alipokuwa akiongelea mafanikio ya miaka mitatu ya serikali ya awamu ya sita kwa waandishi wa habari ofisini kwake jijini hapa. “Ndugu waandishi wa habari, katika kipindi hiki cha miaka mitatu ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita tumeshuhudia ongezeko kubwa la ujenzi wa vituo vya afya katika Jiji la Dodoma, tumejenga vituo vya afya nane. Mpaka sasa vituo viwili vimekamilika. Kituo cha Afya Chang’ombe kimekamilika. Mnafahamu eneo la Chang’ombe lina wakazi wengi zaidi ya 40,000 lakini hawakuwa n...

Miundombinu chachu ongezeko uandikishaji wanafunzi Jiji la Dodoma

Image
  UBORESHAJI wa miundombinu ya elimu unaoendelea kufanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan umekuwa chachu ya ongezeko la uandikishwaji wa wanafunzi wa darasa la kwanza na awali Jiji la Dodoma kutoka asilimia 98 hadi 115 kwa mwaka 2024. Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Prisca Myalla Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Prisca Myalla alipokuwa akiongelea mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita kwa miaka mitatu ofisini kwake. “Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Jiji la Dodoma tunampongeza sana Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya elimu na kutujengea shule mpya kupitia mradi wa BOOST na EP4R. Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeweza kujengewa madarasa mapya na kuboreshewa miundombinu hali iliyopelekea wazazi na jamii kuona fursa ya kuwaleta watoto wao kupata elimu. Serikali imejitahidi sana kuhakiki...