Takukuru kuwajengea moyo wa uzalendo vijana

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ilianzisha klabu za kuzuia na kupambana na rushwa katika shule za msingi, sekondari na vyuo kwa ajili ya kuwajengea moyo wa uzalendo na uadilifu.


Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Dodoma, John Joseph 


Kauli hiyo ilitolewa na Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Dodoma, John Joseph alipotoa salamu wakati wa hafla ya kufungua mashindano ya mdahalo kwa shule za msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu kuhusu madhara ya rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, haki za binadamu na utawala bora katika ukumbi wa St. Gaspar Kisasa jijini Dodoma.

Kamanda Joseph alisema “lengo la kuanzishwa klabu za kupinga rushwa ni kuwajengea moyo wa uzalendo vijana, kuwajenga katika uadilifu na kuongeza uelewa katika makosa na ubaya wa rushwa, kuwajengea uthubutu na ushiriki wao katika kuzuia na kupambana na rushwa. Uanzishwaji wa klabu hizo ulitokana na Takukuru kuamini kwamba vijana katika taifa ni rasilimali muhimu na chimbuko la mabadiliko. Hivyo, kuna umuhimu mkubwa wa kuwarithisha maarifa, uadilifu na moyo wa uzalendo”.

Akiongelea idadi ya klabu za kupinga rushwa, alisema kuwa mkoa una jumla ya klabu 1,081. “Shule za msingi zipo 780, sekondari 274 na vyuo 27. Klabu za wapinga rushwa zina manufaa makubwa ikiwa ni pamoja na kuwajengea wanaklabu uwezo wa kutambua wajibu wao, kuzuia na kupambana na rushwa. Manufaa mengine ni kuhamasisha jamii kutoshiriki katika vitendo vya rushwa, kuwa wajasiri wa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa kwa mamkala ikiwemo Takukuru, wajibu wa kueneza ujumbe wa mapambano dhidi ya rushwa kwa jamii na kuwa wazalendo. Kuwaandaa na kuwajenga kuwa viongozi bora wa kesho wanaochukia rushwa” alisema Kamanda Joseph.




MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma