Watanzania watakiwa kupambana na rushwa na dawa za kulevya
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
WATANZANIA
wametakiwa kushikamana na kupambana na rushwa, dawa za kulevya na uvunjifu wa haki
za binadamu ili kujenga jamii iliyo bora.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora, George Simbachawene |
Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora, George Simbachawene alipokuwa akifungua mashindano ya mdahalo kwa shule za msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu kuhusu madhara ya rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, haki za binadamu na utawala bora katika ukumbi wa St. Gaspar Kisasa jijini Dodoma.
Waziri
Simbachawene alisema “baada ya watu kuwa wanashiba, elimu wanatapa kila kitu
kinaenda vizuri, wanatazama televisheni wamepata ‘exposure’ mambo ni mazuri
wameibuka maadui wengine. Maadui hao ni rushwa, dawa za kulevya na uvunjifu wa maadili
na haki za binadamu, hao maadui watatu ni maadui wabaya sana, ni wajibu wa kila
mmoja tushirikiane kupambana na maadui hao watatu wapya. Wale maadui watatu wa
zamani ujinga, maradhi na umasikini tumewashughulikia vizuri kwa awamu zetu
sita za uongozi wa nchi hii. Chembechembe ndogo zilizobaki tuendelee
kuzishughulikia lakini sasa tuhamie kwenye maadui hawa watatu rushwa, dawa za
kulevya na maadili haki za binadamu na utawala bora”.
Alisema
kuwa vijana ndiyo wahanga wakubwa wa maadui hao watatu. “Ninapojikuta
nimekaribishwa katika mdahalo huu unaohusisha vijana wa shule za msingi, sekondari
na vyuo ninafahamu ndiyo waathirika wakubwa wa vitendo vya rushwa na dawa za
kulevya. Ninafahamu ukitaka kupenyeza uzalendo na kutengeneza watumishi bora wa
kesho lazima tuanze na vijana. Mheshimiwa Jabir Shekimweri, Mkuu wa Wilaya ya
Dodoma na muasisi wa jambo hili na kwamba umeweza kuendeleza maadhimisho haya
yakiwa yanafanyika kila mwaka. Mwenyezi Mungu akutie moyo na akubariki sana ili
uendeleze juhudi zako hizi njema kwa vijana wa taifa letu” alisema Waziri
Simbachawene.
Aidha,
alisema kuwa ni vizuri midahalo hiyo ikawa inafanyika nchi nzima ili kuamsha
ari ya uzalendo na kuwajengea uwezo wa kujiamini vijana. “Jambo hili
linaendelea kuleta mwangwi kwa wengine wengi siyo tu kwenye mkoa kama
alivyosema Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwa vile yeye anazungumzia mkoa wake, lakini
mimi kwa nafasi yangu niseme kama lingeenda mikoa yote ingekuwa nzuri zaidi”
alisema Waziri Simbachawene.
Kwa
upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alitoa pongezi kwa
serikali kuelekea kutimiza miaka 60 ya Muungano. “Niwapongeze sana viongozi
walioanzisha Muungano na waliouendeleza. Lakini kwa sasa nimpongeze Dkt. Samia
Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Dkt. Hussein Ali Mwinyi,
Rais wa Zanzibar wao wameendelea kuuimarisha Muungano” alisema Senyamule.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule |
Vilevile,
alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Dodoma kwa kulipa nguvu suala ya mapambano dhidi
ya rushwa na kuonesha dhamira chanya. “Alipoanza mdahalo wa kwanza nilikuwepo
ila muitikio ulikuwa mdogo ila mwaka jana muitikio uliongezeka na mwaka huu umeendelea
kuimarika kama Muungano wa Tanzania, hongera sana. Mheshimiwa mkuu wa wilaya ameona
asilalamike ila ameamua kuchukua hatua, lakini nimpongeze si kwamba anachukua
hatua kwa mdomo hata yeye mwenyewe anachukua rushwa kwa vitendo” alisema
Senyamule.
Nae
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alisema kuwa zipo haki za watu
ambazo zimekuwa zikipotea kwa sababu ya vitendo vya rushwa na matumizi ya dawa
za kulevya. “Kwa maelekezo ya Rais, tushughulikie kero na tunamshukuru mkuu wa mkoa
ametuongoza tumeanzisha kampeni katika mkoa wake ya ‘Kero yako, wajibu wangu’.
Tunashiriki vita hii kwa kutoa elimu kujenga kizazi ambacho kesho kitachukia
uharibifu wa maadili katika nchi yetu, watachukia matumizi ya dawa za kulevya
kwa sababu wanajua madhara yake na watachukia rushwa, sisi samaki tunamkunja
angali mbichi. Wanafunzi hawa wakielewa nyuma yao ni wazazi, nyuma yao ni
marafiki lakini wao pia baadhi yao ni viranja wanaongea na wenzao, wanawadogo
zao naimani taarifa hizi zitafika kwa watu wengi” alisema Shekimweri.
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri |
Kwa
upande wa Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Dodoma,
John Joseph alisema kuwa lengo la kuanzishwa kwa klabu za kupinga rushwa ni
kuwajengea moyo wa uzalendo na uadilifu na kuongeza uelewa juu ya ubaya wa
rushwa kwa wanafunzi. “Uanzishwaji wa klabu hizo ulitokana na Takukuru kuamini
kwamba vijana katika taifa ni rasilimali muhimu na chimbuko la mabadiliko.
Hivyo, kuna umuhimu mkubwa kuwarithisha maarifa, uadilifu na moyo wa uzalendo.
Mkoa wa Dodoma tuna jumla ya klabu za wapinga rushwa 1,081 kwa shule za msingi,
sekondari na vyuo” alisema Joseph.
Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Dodoma, John Joseph |
MWISHO
Comments
Post a Comment