Midahalo ya kupinga rushwa kupunguza kero kwenye jamii
Na.
Dennis Gondwe, DODOMA
Mkuu
wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri anaendesha midahalo ya kupinga
rushwa, matumizi ya dawa za kulevya na kuhamasisha haki za binadamu na utawala
bora ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya
kusikiliza na kutatua kero za wananchi.
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri
Hayo
yalibainishwa wakati wa salamu za mkuu huyo wa wilaya kwenye hafla ya ufunguzi
wa mashindano ya mdahalo kwa shule za msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo
vikuu kuhusu madhara ya rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, haki za binadamu
na utawala bora katika ukumbi wa St. Gaspar, Kisasa jijini Dodoma.
Alhaj
Shekimweri alisema kuwa zipo haki za watu ambazo zinapotea kwa sababu na
rushwa, matumizi ya dawa za kulevya na ukatili dhidi ya watoto. “Kwa maelekezo
ya mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba tushughulikie kero na
tunamshukuru mkuu wa mkoa ametuongoza tumeanzisha kampeni katika mkoa wake ya ‘kero
yako, wajibu wangu’. Tunashiriki vita hii kwa kutoa elimu ili kujenga
kizazi ambacho kesho kitachukia uharibifu wa maadili katika nchi yetu, kitachukia
matumizi ya dawa za kulevya kwa sababu wanajua madhara yake na kitachukia rushwa,
sisi samaki tunamkunja angali mbichi” alisema Alhaj Shekimweri.
Alisema kuwa ushiriki wa vijana katika midahalo unasaidia kuwajengea umahiri wa kujieleza kwenye usaili wa nafasi za kazi na umahiri wa kuelewa kuwa rushwa na dawa za kulevya ni kero kwa jamii. “Mheshimiwa Rais anaijenga vizuri Tanzania na miradi mingi inatekelezwa kunufaisha vijana ambao ni taifa la kesho. Hivyo, wakikosa manufaa hayo watakuwa wameharibika” alisisitiza Alhaj Shekimweri.
Tanzania
inapoelekea kuadhimisha miaka 60 ya Muungano Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma
imeandaa mdahalo mwaka wa tatu mfululizo juu ya madhara ya vitendo vya rushwa
ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala bora.
MWISHO
Comments
Post a Comment