Tume ya Haki za Binadamu yasisitiza utawala bora
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
TUME
ya Haki za Binadamu na Utawala bora ina dhamira kuona watanzania wanaheshimu
haki za binadamu na misingi ya utawala bora na utu wa mtu.
Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora, Dkt. Thomas Masanja |
Kauli
hiyo ilitolewa na Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora, Dkt.
Thomas Masanja alipokuwa akitoa salamu za tume hiyo katika hafla ya kufungua
mashindano ya mdahalo kwa shule za msingi, sekondari, vyuo vya kati na vyuo
vikuu kuhusu madhara ya rushwa, matumizi ya dawa za kulevya, haki za binadamu
na utawala bora katika ukumbi wa St. Gaspar Kisasa jijini Dodoma.
Dkt.
Masanja alisema “tunashiriki katika shughuli hii inayohusisha wanafunzi wa
shule za msingi, sekondari na vyuo kwa sababu dira ya tume ni kuona jamii yenye
utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu na misingi ya utawala bora na utu wa
mtu. Tunataka mwisho wa siku jamii ya kitanzania inaheshimu haki za binadamu,
utu wa mtu na misingi ya utawala bora”.
Akiongelea
ushiriki wa tume hiyo katika mashindano ya mdahalo huo alisema kuwa watashiriki
kikamilifu. “Tutashiriki kwa kuhimiza haki za binadamu na tutahimiza wajibu kwa
sababu haki inakwenda na wajibu. Tukienda kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania ya mwaka 1977 inatoa haki lakini inatoa wajibu. Hivyo, tutasisitiza
mambo yote mawili. Tutasisitiza utii wa sheria kwa sababu haki za binadamu
zinalindwa na katiba lakini zinalindwa na sheria. Tutasisitiza kufanya kazi kwa
bidii kwa vijana wetu na kulinda rasilimali za nchi yetu” alisema Dkt. Masanja.
MWISHO
Comments
Post a Comment