Elimu Sekondari yafanya usafi Kituo cha Afya Makole
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
DIVISHENI
ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeadhimisha maadhimisho ya
kuelekea kilele cha miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanya
usafi katika Kituo cha Afya Makole kwa lengo la kuwawekea mazingira safi na
salama wagonjwa wanaopata huduma kituoni hapo.
Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Zainabu Abdallah akiongea na mamia ya walimu, wanafunzi na Jumuiya ya Kituo cha Afya Makole
Kauli
hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la
Dodoma, Mwl. Zainabu Abdallah alipokuwa akiongea na mamia ya walimu, wanafunzi
na jumuiya ya wafanyakazi wa Kituo cha Afya Makole kufanya usafi katika kituo
hicho.
Mwl.
Abdallah alisema “sisi Divisheni ya Elimu Sekondari katika Halmashauri ya Jiji
la Dodoma tumeamua kuadhimisha maadhimisho ya kuelekea miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania kwa kufanya usafi katika Kituo cha Afya Makole. Kama mnavyofahamu Makole
ni kituo cha afya cha kimkakati kinachohudumia watu wengi, tumeona ni busara
kushiriki zoezi la usafi wa mazingira. Hapa tumekuja walimu na wanafunzi wa
shule za sekondari zilizo karibu na kituo hiki kufanya usafi. Tunafanya usafi
kwa sababu ni muhimu katika maisha yetu na tunawafundisha watoto wetu tabia ya
kupenda usafi. Hospitali ni moja ya sehemu muhimu inayotakiwa kuwa safi na
mazingira yakuvutia kwa wanaopata na kutoa huduma”.
Alisema
kuwa zaidi ya zoezi la usafi, maadhimisho hayo yamewakutanisha walimu kwa
walimu na wanafunzi kwa wanafunzi kuungana na kuwa wamoja kwa kufanya usafi wa
pamoja.
Akitoa
salamu za Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Afisa Tarafa ya Dodoma mjini, Zainabu Mabuye
alisema kuwa siku hiyo imekuwa na shughuli nyingi za kijamii kuelekea kilele
cha maadhimisho ya miaka 60 ya muungano wa Tanzania. “Mfano hapa Makole
tunafanya usafi kwa kushirikiana na Divisheni ya Elimu Sekondari Jiji la Dodoma
na walimu na wanafunzi wa sekondari. Zoezi hili pia linafanywa na Divisheni ya
Elimu ya Awali na Msingi Jiji la Dodoma kule Shule ya Msingi Dodoma Mlimani na Amani
kwa kupanda miti ya aina mbalimbali na baadae kufuatiwa na bonanza la michezo
katika uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma. Pia kutakuwa na zoezi la uchangiaji
damu litakaloanza muda mfupi ujao ni zoezi muhimu kwa kila mmoja wetu
kushiriki” alisema Mabuye.
Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma ambae ni Afisa Tarafa ya Dodoma mjini, Zainabu Mabuye akitoa salamu za Mkuu wa Wilaya
Alisema
kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya imeandaa mkesha mkubwa katika Shule ya Msingi
Makole tarehe 25 Aprili, 2024. “Nichukue nafasi hii kuwaalika wananchi wate
kwenye mkesha mkubwa kesho kuanzia saa 11 jioni mpaka saa 6 usiku. Burudani
mbalimbali zitakuwepo, wajasiriamali watakuwa wakionesha bidhaa zao nyama choma
za kutosha, usijaribu kukosa” alisema Mabuye.
Kwa
upande wa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Dodoma, Husna Juma alisema “Tupo
hapa Kituo cha Afya Makole tunaadhimisha miaka 60 ya Muungano wa Tanzania na
tumekuja kusaidia usafi ili kuboresha afya zetu, kuboresha mazingira na
kupunguza hewa chafu katika anga”.
Ikumbukwe
kuwa zoezi la usafi zimeratibiwa na divisheni ya elimu sekondari likijumuisha
kufanya usafi katika vituo vingine vya afya vilivyopo nje kidogo ya Halmashauri
ya Jiji la Dodoma.
MWISHO
Comments
Post a Comment