Mtaji Benki ya TADB wafikia Bil. 442

Na. Mwandishi wetu, DODOMA


Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwekeza katika uwezeshaji wakulima kwa kuwapatia mikopo ya Pembejeo.


Akitoa maelezo kwa Mhe. Rais Samia kuhusu utendaji wa Benki hiyo leo Agosti 8,2025 wakati wa maadhimisho ya kilele cha Nanenane kitaifa, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Frank Nyabundege alisema kuwa mtaji wa Benki hiyo umekuwa kutoka shilingi bilioni 60 hadi bilioni 442.


“Benki yetu itaendelea kudhamini maonesho ya NnNe Nane kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo kwa sababu imeiwezesha kuwa na mtaji mkubwa” alisisitiza Nyabundege.

Mgeni rasmi katika maonesho ya Nanenane Kitaifa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.






 

Comments

Popular Posts

Jiji la Dodoma lapewa angalizo lishe bora kwa wananchi

RC Dodoma apongeza wafugaji kwa ushiriki wa Paredi ya Mifugo

Rais Samia: Tumieni kikamilifu Miundombinu, Teknolojia na mitaji iliyowekezwa katika Kilimo, Uvuvi na Mifugo