Posts

Showing posts from March, 2025

Kata ya Makole yang’ara miaka minne ya Samia

Image
Na. Emanuel Charles, MAKOLE   Diwani wa Kata ya Makole, Omary Omary, aishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu ya maendeleo kwenye sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya, ujenzi wa barabara na ofisi ya wafanyabiashara wadogo katika kata yake.   Akizungumza katika ziara ya waandishi wa habari waliotembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa kuanzia mwaka 2020 hadi sasa katika Kata ya Makole, Diwani Omary alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kuijali Kata ya Makole kuwaboreshea miundombinu muhimu. “Kipekee nimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa miaka hii minne ambapo yupo madarakani, maboresho ambayo ametufanyia hususani sisi wana Makole kwa kutuletea miundombinu sahihi ni makubwa sana. Mheshimiwa Rais, ameboresha sekta ya elimu kwa kujenga shule ya jengo la ghorofa lenye madarasa nane na ofisi mbili za waalimu katika Shule ya Msingi Makole. Katika sekta ya afya, Za...

Dodoma Jiji FC, yatua Dar kibabe kumenyana na Mnyama

Image
Na. Mussa Richard, Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, itashuka dimbani hapo kesho kumenyana na klabu ya Soka ya Simba SC, katika mchezo wa ligi kuu ya NBC Tanzania bara, mchezo utakaopigwa katika dimba la KMC Complex Mwenge, Dar es salaam majira ya saa 10 kamili jioni. Akizungumzia maandalizi ya timu, Kocha mkuu wa Dodoma Jiji FC, Mecky Mexime wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa Simba SC, alisema “tunamshukuru Mungu tumefika Dar es Salaam salama, jana tumefanya mazoezi mepesi ya kuiweka miili sawa, tunajua mchezo utakuwa ni mgumu kwa pande zote, ukizingatia kwasasa ligi inaelekea ukingoni. Alama tatu kwa kila mchezo ni muhimu ili tuweze kifikia malengo yetu ya kumaliza ligi tukiwa nafasi za juu kwenye msimamo, maandalizi yote ya kucheza na Simba SC, tumeyafanya tukiwa Dodoma. Hapa tumekuja kukifanyia kazi kile tulichojifunza kwenye uwanja wa mazoezi’’. Nae Abdi Banda, mchezaji wa Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, akawaita mashabiki wa Dodoma Jiji FC, waliopo Da...

Habari Picha, Lishe wanafunzi wa Awali Shule ya Msingi Mlezi

Image
  Wanafunzi wa Awali katika Shule ya Msingi Mlezi wakipata uji shuleni hapo wakati wa asubuhi

Habari Picha ya Lishe Shule ya Msingi Mlezi

Image
  Watoto wenye mahitaji maalum wa Shule ya Msingi Mlezi wakipata chakula cha mchana mara baada ya masomo yao

Wazazi watakiwa kutoa kipaumbele kwa maendeleo ya watoto

Image
Na. Leah Mabalwe, HAZINA   Diwani wa Kata ya Hazina, Samwel Mziba, amewataka wazazi pamoja na walezi kuwa kipaumbele katika maendeleo ya watoto wao shuleni.   Mziba, alisema hayo wakati wa kikao cha walimu pamoja na wazazi kilichofanyika katika Shule ya Msingi Mlezi kwa lengo la kuzungumzia maendeleo ya lishe bora kwa wanafunzi wa shule hiyo. “Kwanza kabisa napenda kuwashukuru wazazi wote mliofika katika kikao hiki, najua mnaelewa lengo na dhumuni la kuitisha kikao hiki cha leo, tukianzia kuzungumzia suala zima la malezi kwa watoto, tunashuhudia wazazi wengi wanakuwa wametingwa sana na kazi zao, kiasi kwamba wanakua hawana muda wa kufuatilia maendeleo ya watoto wao shuleni. Hii hali si nzuri kwasabu inamjengea mtoto kufanya kila kitu anachojisikia kwa vile hakuna mtu yeyote anae weza kummfuatilia. Hivyo, basi napenda kuwahamasisha wazazi pamoja na walezi tuwe mstari wa mbele kufuatilia maendeleo ya watoto wetu shuleni’’alisema Mziba. Pia aliongezea kwa kuwataka wazaz...

Mavunde apongeza Baraza la madiwani kupendekeza kugawanywa Jimbo la Dodoma Mjini

Image
  Na. Nancy Kivuyo Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini, Anthony Mavunde, ametoa pongezi kwa baraza la madiwani kwa kuridhia taarifa ya mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Uchaguzi la Dodoma Mjini kuwa majimbo mawili. Katika salamu zake fupi aliishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mabadiliko makubwa katika sekta mbalimbali. Akizungumzia mgawanyo wa Jimbo la uchaguzi la Dodoma Mjini na kuwaeleza madiwani faida zitakazopatikana baada ya kugawanya kwa jimbo hilo. “Jimbo la Dodoma mjini ndilo jimbo kubwa kuliko majimbo yote hapa nchini likiwa na Tarafa nne, kata 41 na mitaa 222. Nipende kuwaambia, mgawanyo wa jimbo utaongeza fursa nyingi za kuhudumia wananchi. Mfuko wa jimbo utasogeza huduma kwa jamii kwa urahisi zaidi, kupitia uwepo wa majimbo mawili, fedha nzuri itapatikana kwa ajili ya kuboresha miundombinu” alisema Mavunde. Aliongeza kuwa mipango ya kiserikali inasaidia huduma za kijimbo kupatika...

Wapiga kura 795,000 Kugawanywa, Jimbo la Dodoma Mjini

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma yawasilisha mapendekezo ya kugawanya Jimbo la Uchaguzi la Dodoma Mjini lenye jumla ya wapiga kura 795,000 na kuwa majimbo mawili, Jimbo la Mtumba lenye jumla ya wapiga kura 412,000 na Jimbo la Dodoma Mjini lenye jumla ya wapiga kura 383,000 kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi. Hayo yalisemwa na Afisa Uchaguzi wa Halmashauri hiyo, Albert Kasoga alipokuwa akiwasilisha taarifa kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, ya mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini, mbele ya Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Akizungumza wakati wa kuwasilisha taarifa hiyo, alisema kuwa mgawanyo huo umezingatia hali ya kiuchumi ya jimbo husika hasa katika ukusanyaji wa mapato ya ndani sambamba na kuzingatia ukubwa wa eneo husika. “Mgawanyo umezingatia hali ya kiuchumi ya jimbo hasa katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ya jimbo husika. Lengo ni kuona kuwa maene...

Dkt. Sagamiko asema, ugawaji jimbo hauna athari kwa huduma zinazotolewa na Jiji la Dodoma

Image
Na, Nancy Kivuyo, DODOMA Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alitoa hofu Baraza la Madiwani kuwa kukidhi vigezo vya ugawaji wa Jimbo la Dodoma Mjini hauna athari katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo katika kuwahudumia wananchi. Aliyasema hayo wakati akijibu hoja za madiwani waliohudhuria katika Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupokea taarifa ya mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. “Mgawanyo wa jimbo kwa upande wa tarafa hauna kikwazo chochote, kama ni kata ni kikwazo kwasababu kata moja haiwezi kuwa katika majimbo mawili. Leo tutaangalia zaidi kwenye kata” alisema Dkt. Sagamiko. Aliongeza kuwa, athari za mgawanyo wa jimbo kimapato unalenga mgawanyo wa majimbo na sio shughuli za kiutendaji. “Niwatoe wasiwasi, utoaji wa huduma kwa wananchi utaendelea kama ilivyokua awali na Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Baraza litakua moja bila kujali jimbo analotoka diwani. M...

DC SHEKIMWERI: “Tufuate Utaratibu Mzuri wa Tume Huru ya Taifa Uchaguzi ili tulinde Jiji la Dodoma”

Image
Na. Leah Mabalwe, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri, awataka viongozi wa vyama vya siasa pamoja na wananchi kufuata maelekezo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili kutovuruga maendeleo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   Aliyasema hayo katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Dodoma kilichoketi kujadili taarifa ya mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini na kuzalisha Jimbo la Mtumba pamoja na Jimbo la Dodoma mjini. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la leo tarehe 12 Machi, 2025. “Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, inatoa fedha nyingi kwaajili ya kuboresha Mji wa Dodoma. Hivyo, napenda kuwaomba sana viongozi wangu mbalimbali wa vyama vya siasa pamoja na vijana wote kwa ujumla kuelekea katika uchaguzi mkuu wa serikali, kufuata taratibu nzuri na kuepuka vurugu, na ili kuepuka vurugu ni kufuata utaratibu mzuri wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kuanzia wakati wa kujian...

Halmashauri ya Jiji la Dodoma Kuhudumia Majimbo Mawili ya Uchaguzi

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imejipanga vema kutoa huduma kwa wananchi wote kwa kuzingatia mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini wenye mapendekezo ya kuligawa jimbo hilo kuwa Jimbo la Mtumba lenye jumla ya kata 20 na Jimbo la Dodoma Mjini lenye kata 21. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko, mara baada ya majadiliano kutoka kwa Madiwani kuhusu taarifa iliyowasilishwa na Afisa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Albert Kasoga ya kuwasilisha mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini, katika Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani lililofanyika tarehe 12 Machi, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Dkt. Sagamiko alisema “mgawanyo huu kwa sasa unalenga mgawanyo wa jimbo kuwa majimbo mawili, bado tutaendelea kuwa na halmashauri moja kwa maana ya utoaji huduma kwa ngazi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Jiji litaendelea kuwajibika katika utoaji wa huduma katika majimbo yote mawili”. Akizung...

Dkt. Sagamiko amshukuru Rais Dkt. Samia, Jiji la Dodoma kuwa la mfano

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko, amshukuru Rais, Dkt. Samia kwa kulifanya jiji hilo kuwa la mfano nchini na kuahidi utoaji wa huduma bora kwa wananchi alipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya shughuli zinazotekelezwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini.   Aliyasema hayo wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipotembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Center kabla ya ufunguzi wa Mkutanao wa 39 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT). “Mheshimiwa Rais, Halmashauri ya Jiji la Dodoma ndiyo halmashauri pekee yenye muundo wa kipekee katika halmashauri zote 184 zilizopo Tanzania. Moja ya upekee huo ni Divisheni ya Uendelezaji Makao Makuu. Baada ya Dodoma kuwa makao makuu mwaka 1976 iliweza kuandaliwa Mpango Kabambe wa kuuendeleza Mji wa Dodoma ikiwemo Uwanja wa Ndege wa Msalato pamoja na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)” alisema Dkt. Sagamiko...

Ujenzi Shule za Sekondari za ziada Suluhu Changamoto ya Umbali

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Kata 41 za Halmashauri ya Jiji la Dodoma zinatarajiwa kunufaika na ujenzi wa shule za sekondari za ziada kwa ajili ya kuhakikisha mtoto anapata elimu katika mazingira mazuri na kutatua changamoto ya umbali wa kupata huduma ya elimu. Hayo yalisemwa na Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde, alipokuwa akitoa hotuba kwa madiwani, wakuu wa divisheni na vitengo, walimu, watendaji wa kata na wanafunzi waliohudhuria katika hafla ya Ugawaji Kompyuta na Printa kwa Shule za Sekondari na maafisa watendaji wa kata jijini Dodoma. Mbunge wa Jimbo la Dodoma, Anthony Mavunde alisema “moja kati ya mipango yangu mikubwa nayoendelea nayo ni kuendelea kuhakikisha kata zote za Dodoma zina sekondari, tukimaliza hayo tuongeze sekondari za ziada hasa zile ambazo watoto wanatembea umbali mrefu. Mheshimiwa mkuu wa wilaya ukienda pembezoni mwa Jiji la Dodoma, kuna maeneo ambayo watoto walikuwa wanatembea mpaka kilomita 16 kufuata shule. Ukienda Kata ya Chahwa eneo la Mahoma Makulu...

Mbunge Mavunde akabidhi Kompyuta kwa Kata 41 za Jiji la Dodoma

Image
Na. Nancy Kivuyo, VIWANDANI Watendaji wa Kata 41 za Halmashauri ya Jiji la Dodoma wapokea Kompyuta na Printa kwa ajili ya kurahisisha na kuboresha utendaji kazi wenye ufanisi za kuwahudumia wananchi. Vifaa hivyo, viligawiwa katika hafla ya Ugawaji Kompyuta na Printa kwa Shule za Sekondari za Serikali na Watendaji wa Kata jijini Dodoma, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Viwandani.   Akizungumza wakati wa ugawaji kompyuta hizo, Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde, alisema kuwa anawapa kompyuta maafisa watendaji wa kata zote 41 kwaajili ya kuwasaidia kufanya kazi zao kidigitali zaidi. “Kompyuta na printa hizi natumaini zitachochea utendaji kazi ulio mzuri. Tuipongeze serikali chini ya uongozi wa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maboresho makubwa ya miundombinu kwenye sekta ya elimu jijini Dodoma ambapo kwa mwaka huu wa fedha zimetengwa shilingi bilioni 16” alisema Mavunde. Nae, Afisa Mtendaji wa Kata ya Hazina, Tunu Mahmoud, alisema kuwa ameguswa na tukio l...

Mkutano Mkuu wa 39 wa ALAT wafanyika Dodoma

Image
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Mkutano mkuu wa 39 wa Mwaka wa Mamlaka ya Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) umefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Convention Center jijini Dodoma, uliofunguliwa na mgeni rasmi ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kujadili na kufanya tathmini ya mipango ya ALAT na mambo mbalimbali yanayoendelea katika serikali za mitaa. Akitoa taarifa wakati wa mkutano huo, Mwenyekiti wa ALAT Taifa, Murshid Ngeze, alisema kuwa katika mkutano wa mwaka huo wamejitahidi kualika viongozi mbalimbali wakiwemo wenyeviti wa mitaa ili kupata maarifa mbalimbali yanayohusiana na uendeshaji wa serikali za mitaa. Hivyo, kwenda kuwa viongozi bora katika mitaa yao. “Mkutano huu tunafanya kila mwaka, lakini mwaka huu tumeenda mbali zaidi kwa kuwaalika wenyeviti wa serikali za mitaa ili watakapofika hapa waweze kupata ujumbe wa moja kwa moja na kujifunza namna ya uendeshaji na utekelezaji wa shughuli zote zinazohus...

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma atoa angalizo matumizi ya ‘Internet’ Viwandani Sekondari

Image
Na. Nancy Kivuyo, VIWANDANI Walimu watakiwa kudhibiti matumizi mabaya ya ‘internet’ kwa wanafunzi shuleni ili kukabiliana na mabadiliko makubwa ya utandawazi na matumizi ya teknolojia. Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri wakati wa Hafla ya Ugawaji wa Kompyuta na Printa kwa Shule za Sekondari za Serikali jijini Dodoma, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Viwandani. “Rai yangu ni kwamba tujitahidi kuweka ‘internet’ ili kusudi matumizi chanya kabisa ya maabara hiyo iweze kufanyika. Tukishaweka hiyo ‘internet’ tusisahau kuweka udhibiti ili vijana wetu wawe salama na matumizi yasiyo rafiki ya mitandao. Bahati mbaya wapo vijana wanaotumia mitandao kupenyeza agenda husuani mitaala ambayo haifai kwenye elimu yetu, kwahiyo ili kuzuia hayo ni muhimu kuweka vidhibiti na kuwa makini” alisema Alhaj Shekimweri. Nae, Mwalimu wa Shule ya Sekondari Viwandani, Mwl. Dickson Massatu, alieleza kuwa amefurahi Shule ya Sekondari Viwandani kupatiwa vifaa hivyo kwasababu...

Mbunge Mavunde agawa Kompyuta na Printa Shule za Sekondari za Serikali Dodoma

Image
Na. Leah Mabalwe, VIWANDANI Wanafunzi wa shule za sekondari za serikali waaswa kuongeza jitihada katika masomo yao ili kuzidisha ufaulu. Hayo yalisemwa na Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde wakati wa hafla ya ugawaji wa komputa na printa katika shule zote za serikali za sekondari jijini Dodoma na uzinduzi wa maabara ya kisasa ya kompyuta ya Shule ya Sekondari Viwandani. “Napenda kuhamasisha wanafunzi wote wa shule za sekondari kuongeza jitihada sana katika masomo yenu. Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sasa anawekeza sana katika sekta ya elimu ili wanafunzi wote mpate mazingira mazuri kwa ajili ya kujisomea. Kwa sasa tunahitaji kujenga Jiji la Dodoma katika sekta ya elimu na kazi kubwa bado zinaendelea kufanyika. Nimeamua kufanya ziara hii ya ugawaji wa kompyuta katika shule zote za Dodoma mjini ili kuwaongezea maarifa pamoja na kukua kwa utandawazi kwasababu tunarahisisha upataji wa maarifa kwa ninyi wanafunzi wote. Kompyuta hizi zina ...

Shule ya Sekondari Viwandani yamshukuru Mbunge Mavunde kuboresha miundombinu ya Elimu

Image
Na. Faraja Mbise, VIWANDANI Uongozi wa Shule ya Sekondari Viwandani wamshukuru Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde kwa kuboresha miundombinu ya shule hiyo sambamba na ujenzi wa maabara mpya ya kompyuta na ugawaji wa kompyuta 20, viti 20 na printa moja. Shukrani hizo zilitolewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari Viwandani, Mwl. Ester Simchimba, alipokuwa akitoa taarifa ya shule hiyo katika hafla ya ugawaji Kompyuta na Printa kwa shule za sekondari jijini Dodoma, iliyofanyika tarehe 10 Machi, 2025 katika Shule ya Sekondari Viwandani, Kata ya Viwandani, jijini Dodoma. Akisoma risala hiyo, Mwl. Simchimba alimshukuru mgeni rasmi kwa kuwa mdau mkubwa katika kusimamia taaluma na kuboresha miundombinu ya shule hiyo, sambamba na kutoa nafasi ya kipekee ya kuichagua shule hiyo kuwa sehemu maalum kwa kufanyia tukio hilo la kihistoria katika shule hiyo. “Tunashukuru kwa kuchagua shule yetu kuwa mahali pa kufanyia hafla hii fupi na tukio la kihistoria katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ikiwaki...