Mikopo ya 10% yawanufaisha vijana wa Kata ya Ipala

Na. John Masanja, IPALA

Halmashauri ya Jiji la Dodoma yakipatia kikundi cha Kazi iendelee Ipala mkopo usio na riba wa shilingi 17,000,000 kwa ajili ya kuongeza mtaji kwa shughuli ya bodaboda na kutengeneza ajira kwa vijana ili waweze kujitegemea kimaisha.


Hayo yalielezwa na Mhasibu wa Kikundi cha Kazi iendelee, Peter Mhaka mbele ya waandishi wa habari waliofanya ‘media tour’ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika kata hiyo kuanzia mwaka 2021 hadi 2025.

“Kikundi kilipata mkopo huu ili kujikwamua kiuchumi. Mwaka 2023 tulichukua mkopo wa shilingi 17,000,000 tukiwa watano, tukanunua bodaboda tano ambazo zimetunufaisha kwa kusomesha watoto, tumejiingiza kwenye kilimo na tumepunguza utegemezi yote hii ili kujikwamua zaidi kiuchumi” alisema Mhaka.

Aidha, aliiomba serikali kuendelea kuhamasisha vijana ili wafahamu umuhimu wa mikopo hiyo. “Nawashauri vijana wenzangu wachangamkie fursa ya mikopo hii isiyoumiza, watembelee ofisi za kata ili kupata elimu ya mikopo hii” alisema Mhaka.



Nae Afisa Mtendaji wa Kata ya Ipala, Herman Malindila alikipongeza Kikundi cha Kazi iendelee na kuwasihi kuendelea kuchangamkia fursa zinazotolewa kwa vijana na serikali ya awamu ya sita. “Nawapongeza vijana kwa kazi nzuri, muendelee kuwa mfano kwa wengine ili nao waje waone umuhimu wa mikopo hii. Serikali yetu inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan inajali vijana wa rika zote hivyo, changamkieni fursa ili kujikwamua kiuchumi” alipongeza Malindila.



MWISHO

 

 

Comments

Popular Posts

Agenda ya Lishe yaongeza Ari ya usomaji S/M Dodoma Makulu

RC Senyamule azipongeza Club za Jogging Dodoma

Osterbay Dodoma wajitokeza usafi wa mazingira