Shule shikizi Ipala, mkombozi kwa wanafunzi wanaotembea umbali mrefu

Na. John Masanja, IPALA

Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa, aishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu ya elimu msingi katika kata hiyo kwa kujenga shule shikizi ili kutengeneza mazingira rafiki kwa wanafunzi wenye umri mdogo kupata elimu bora.


Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa

Aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ‘media tour’ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika Kata ya Ipala kuanzia mwaka 2021 hadi 2025.

Diwani Magawa alisema kuwa katika miaka minne ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita, elimu katika Kata ya Ipala imekuwa kwa kasi. “Serikali yetu tukufu imetuletea elimu hadi kwenye kata yetu. Tuna shule shiziki mbili zimeanzishwa kwa lengo la kusaidia wanafunzi wadogo wanaotembea umbali mrefu karibu kilomita tano kufuata elimu. Sasa hivi uwepo wa madarasa haya matatu nafuu imekuwa kubwa sana kwa kuwapunguzia watoto wadogo kutembea umbari mrefu” alisema Magawa.




Pia, aliongeza kuwa anaishukuru serikali kwa maboresho hayo kwasababu wanafunzi wanapata elimu ipasavyo na anaamini kwa siku zijazo maboresho makubwa zaidi yatafanyika. “Tunaishukuru serikali kuanzia rais wetu Dkt. Samia, Mbunge Mavunde, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Sagamiko na watendaji wengine wote kwa kuona umuhimu mkubwa wa Kata ya Ipala kupata shule hizi. Kama mlivyojionea ndugu waandishi, jiji hili ni kubwa kwahiyo, hata sasa tunafurahi kufikiwa na maendeleo haya” alishukuru Magawa.



Kwa upande mwingine, mkazi wa Kata ya Ipala, Elisha Nghambi alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada nyingi anazofanya kuboresha maendeleo ya wananchi ikiwemo sekta ya elimu. “Shule hii shikizi ya Mwinyi imekuwa na faida kubwa hasa kwa kuinua viwango vya elimu hapa kwetu, hapo nyuma vijana wengi hawakusoma kutokana na umbali uliokuwepo. Ujenzi wa shule hii umeleta mwamko wa elimu zaidi, wazazi wanapeleka watoto shule, watoto wengi wa mtaa huu wanasoma na kufurahia sasa, tunashukuru sana. Mradi huu ni chachu ya wananchi kuwahimiza watoto kupata elimu ili kutenegeneza maisha yao ya sasa na ya baadae” alishukuru Nghambi.




MWISHO

 

 

Comments

Popular Posts

Agenda ya Lishe yaongeza Ari ya usomaji S/M Dodoma Makulu

Shule shikizi Ipala, mkombozi kwa wanafunzi wanaotembea umbali mrefu

Waziri Mavunde asisitiza miradi mikubwa ya madini iliyopewa leseni kuanza kazi haraka