Maadhimisho ya Wiki ya Lishe kupitia Dodoma FM jijini DOdoma

 Maafisa Lishe Jiji la Dodoma wamefanya shughuli mbalimbali katika Wiki ya Lishe ikiwemo utoaji wa elimu ya lishe kupitia vyombo vya habari na kwa kutembelea vituo vya kulelea watoto kwaajili ya kupima afya.



‎Maadhimisho ya Siku ya Lishe Kitaifa ambayo yalianza tarehe 17 Novemba 2025 yanatarajiwa kuhitimishwa leo tarehe 21 Novemba, 2025.

‎Akizungumza katika kipindi cha Dodoma Live kinachorushwa na Kituo cha Redio Dodoma Fm, Afisa Lishe Kituo cha Afya Makole, Frida Mollel alisema kuwa kila mmoja anatakiwa kuzingatia makundi sita ya chakula. "Katika maisha ya kawaida ya binadamu makundi sita ya chakula yanapatikana kiurahisi mfano mboga za majani, matunda, dagaa hata mafuta ya kupikia. Jambo la kuzingatia ni kwamba kuna baadhi ya vyakula havitakiwa kuliwa kwa pamoja kwasababu vinafanya kazi moja" alisema.

‎Mollel alisisitiza kwa mifano juu ya aina ya vyakula vinavyopaswa kuepukwa kuliwa kwa pamoja na vyenye kazi moja kwenye mwili wa binadanu. "Mfano viazi, ndizi, wali na ugali ni vyakula ambavyo ni aina ya wanga na vinafanya kazi moja ya kuupa mwili nguvu hivyo mtu anashauriwa kuchagua kimojawapo" alisisitiza

‎Alimalizia kwa kuelezea namna mtoto mchanga anapaswa kupatiwa lishe bora kutoka kwa Mama. "Pia mtoto mchanga anatakiwa kunyonya kwa muda wa miezi sita bila kupewa chakula kingine baada ya hapo atatumia uji wenye virutubisho vya lishe ili kumjenga kiafya" alimalizia Mollel.

‎MWISHO

Comments

Popular Posts

Agenda ya Lishe yaongeza Ari ya usomaji S/M Dodoma Makulu

Miaka minne ya Dkt. Samia, Kizota yanufaika mikopo ya asilimia 10

Halmashauri ya Jiji la Dodoma Kuhudumia Majimbo Mawili ya Uchaguzi