Agenda ya Lishe yaongeza Ari ya usomaji S/M Dodoma Makulu

Na. Abdul Iddi, DODOMA MAKULU

Shule ya Msingi Dodoma Makulu imeshukuru agenda ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya lishe shuleni kwa sababu inawaongezea ari ya kusoma na kupata matokeo yanayokusudiwa.



Shukrani hiyo ilitolewa na Mwalimu wa Lishe, Rehema Kalinga alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari waliotembelea shule ya msingi Dodoma makulu kujionea hali ya lishe kwa wanafunzi shuleni hapo.

Alisema kuwa shule yake inazingatia ajenda ya Lishe kwa kuwapa wanafunzi wote kuanzi awali mpaka darasa la Saba uji. Darasa la Nne na la Saba kupata chakula cha mchana. “Toka ajenda hii kuanza kutekelezwa, tumeanza kuona matokeo Chanya. Kwanza kwakupunguza utoro, pia watoto darasani wanafundishika” alisema Mwl. Kalinga.

Aidha, alitoa pongezi kwa wazazi kwa kusikiliza ajenda ya Lishe na kuitekeleza bila kusuasua kwasababu waliweza kutoa mchango kwa kiasi walicho kubaliana na kamati ya wazazi wa shule hiyo. “Muitikio ni mkubwa kwasababu watoto wote katika Shule ya Dodoma Makulu wanapata uji na wengine pia chakula cha mchana, kwasababu wazazi hawakukaa nyuma kutoa mchango kwaajili ya watoto wao kupata chakula shuleni” alisema Kalinga.

Nae Mwalimu wa Taaluma wa shule hiyo, Mwl. Mwanahamisi Goma alieleza namna serikali ya awamu ya sita inavyotoa kipaumbele kwa agenda ya lishe na kusema kuwa inasaidi kukuza taaluma. “Suala la lishe limenisaidia sana katika utendaji kazi wangu wa uratibu wa taaluma hapa shuleni, kwasababu kupitia chakula shuleni wanafunzi wa shule wameonekana kuongeza ufahulu kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na wakati ambao walikuwa hawapati chakula. Ufaulu wetu umepanda kuanzia ngazi ya kata mpaka kitaifa” alisema Mwl. Goma.

Nae mwanafunzi wa darasa la Sita, Jonathan Mwasambuli alieleza jinsi agenda ya lishe ilivyowasaidia katika masomo. “Chakula shuleni kinasaidia kupata nguvu pia kuimarika kiubongo pia inanifanya nishindwe kulala darasani. Hivyo, chakula kinanipa nguvu ya kusoma kwa bidi” alisema Mwasambuli.

MWISHO

Comments

Popular Posts

RC Senyamule azipongeza Club za Jogging Dodoma

Osterbay Dodoma wajitokeza usafi wa mazingira