Posts

Showing posts from July, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kuzindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kuzindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akionesha nakala za vitabu vya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 mara baada ya uzinduzi

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akionesha nakala za vitabu vya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 mara baada ya uzinduzi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC

Mkoa wa Dodoma kuja na Mpango Mkakati wa kukuza na kutangaza Utalii wa Ndani

Image
Na. Hellen Minja, DODOMA RS Utalii unatajwa kuwa na athari chanya za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na Mkoa kwa ujumla pale unapotumika kimkakati. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amebainisha hayo alipokua akifungua kikao Maalumu cha Maandalizi ya uzinduzi wa Kitabu cha Mpango Mkakati wa Kukuza na Kutangaza Utalii wa Mkoa huu. Kikao hicho kimewahusisha wadau wa utalii kutoka sekta mbalimbali waliokutana kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma jijini hapa lengo likiwa ni kupitia Mpango Mkakati ulioandaliwa sambamba na kuunda Kamati itakayoshughulikia kwa karibu ufanikishaji wa shughuli hiyo. “Utalii una athari nyingi za kiuchumi kama ukiwa nao maana utakuza uchumi wa mtu mmoja mmoja lakini pia wa Mkoa. Dodoma tunatamani tuwe ‘hub’ ya utalii kwa sababu tunafikika kila upande wa nchi ya Tanzania hata kama vivutio vya utalii havipo Dodoma tunataka iwe active kwenye suala la utalii” Senyamule. Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Tawala Msaidizi Sekta za Viwanda, Bi...

Watanzania waaswa kutunza tunu ya Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Image
Na. Sofia Remmi, Dodoma RS Watanzania wametakiwa kuendelea kuitunza Tunu ya amani wakati nchi ikielekea kwenye zoezi la Kitaifa la uchaguzi mkuu huku wanasiasa wakitakiwa kufanya kampeni za kistaarabu ambazo hazichochei hasira na vurugu zisizo na tija. Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Taifa, Askofu Dkt. Venance Chande, aliyasema hayo wakati wa mkutano wa kutoa taarifa ya kongamano lililoandaliwa na Idara ya Elimu ya Mahakama ya Kadhi na Baraza la Waislam Tanzania (BAKWATA) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. Askofu huyo alisema kuwa amani ndio msingi wa maendeleo ya Taifa lolote Duniani. “Sisi watanzania hatujazoea kugombana, tumezoea kuishi pamoja kwa umoja na upendo, hatujazoea kubaguana kwa misingi ya makabila au dini zetu, hayo ndiyo maisha tuliyoyazoea kuishi” alisema Dkt. Chande. Aidha, amewataka Wanasiasa kufanya siasa za kistaarabu. “Wanasiasa, huu ni mwaka wa uchaguzi, kampeni zifanyike kistaarabu zisiwe za kuchochea hasira, washawishi kwa Ser...

Kituo cha Dharura cha Serikali chawa kivutio Afrika kwa kukinga Maafa

Image
Na Mwandishi Wetu – Dodoma Uwekezaji wa Serikali ya Tanzania katika kuimarisha mifumo ya kukabiliana na majanga kupitia Kituo cha Ufuatiliaji wa Majanga na Tahadhari ya Mapema (Situation Room) umeanza kuzaa matunda, baada ya nchi mbalimbali za Afrika kuonesha kuvutiwa na namna kituo hicho kinavyofanya kazi. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu kwa wataalamu kutoka Ghana, Togo na Burkina Faso yanayofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, Jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Menejimenti ya Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Brigedia Jenerali Hosea Ndagala, alisema kituo hicho kimeongeza uwezo wa nchi kuchakata taarifa za viashiria vya majanga na kutoa taarifa za viashiria vya majanga na kutoa tahadhari mapema kwa wananchi. “Uendeshaji wa kituo hiki unahusisha wataalamu kutoka taasisi mbalimbali za Serikali wanaoshirikiana kuchakata taarifa kwa pamoja, jambo linalosaidia kutoa tahadhari kwa wakati,” alisema Brigedia Jenerali Ndagala. Mkurugenzi Msaidizi wa kituo hicho, Bi....

Picha ya Pamoja ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan na Baraza la Mawaziri

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Dkt. Moses Kusiluka kwenye picha ya pamoja  na Mawaziri  mara baada ya Kikao cha mwisho cha Baraza la Mawaziri cha Serikali ya Awamu ya Sita kilichofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 14 Julai, 2025

Rais, Dkt. Samia aongoza kikao cha mwisho cha Baraza la Mawaziri

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 14 Julai, 2025. Kikao hicho cha Baraza la Mawaziri ni cha mwisho cha Serikali ya Awamu ya Sita kabla ya kufanyika Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba 2025.  

Waganga Wakuu wamemtunukia Rais Tuzo, Dkt. Mpango awapongeza, atoa maelekezo mahususi

Image
Na. John Mapepele Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa tuzo maalum ya kutambua mchango wake kwenye Sekta ya Afya na Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri hii leo. Tuzo hiyo aliitoa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa kwa niaba ya Waganga hao na kumkabidhi Makamo wa Rais, Mhe. Dkt. Philipo Mpango aliyekuwa mgeni rasmi katika Mkutano huo wa Mwaka wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri jijini Dodoma. Mbali na tuzo hiyo pia Waganga Wakuu wamemtunukia Makamo wa Rais tuzo hiyo pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa na Waziri wa Afya, Jenista Mhagama. Dkt. Mpango amewapongeza Waganga Wakuu nchini kwa kazi wanayofanya ya kuwahudumia wananchi huku akiwataka waendelee kuimarisha huduma na sekta ya afya kwa ujumla na kuzingatia maadili ya taaluma yao. Alisisitiza kuwa Serikali itatekeleza mara moja maombi ya kuboresha stahili za wataalam hao kulingana hali halisi ya uchumi. “Nawaelekeza Mawaziri ...

Kongamano la Rushwa latoa matumaini ya kuendelea kutokomeza Rushwa nchini

Image
Na. Nnacy Kivuyo, DODOMA   Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amesema Tanzania inaendelea kufanya vizuri katika mapambano dhidi ya rushwa kila mwaka kutokana na utawala bora uliopo nchini.   Aliyasema hayo wakati akifungua Kongamano la Maadhimisho ya siku ya Mapambano dhidi ya Rushwa Barani Afrika yaliyofanyika jijini Dodoma. Alisema kuwa kuanzishwa kwa Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi ndani ya Mahakama Kuu pamoja na Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2023 ni hatua nyingine muhimu katika kuhakikisha vitendo vya rushwa vinadhibitiwa ipasavyo nchini.  “Ndugu washiriki, Tanzania imepiga hatua kubwa katika jitihada za kutokomeza rushwa, ikiwa ni pamoja na kutunga na kufanya maboresho ya sheria mbalimbali zinazolenga kupambana na vitendo hivyo. Tuendelee kuzitumia sheria hizi sambamba na kutoa elimu ili kuhakikisha wananchi wanafahamu nafasi na wajibu wa kila mmoja katika kuitoko...

Baraza la Biashara kuvutia sekta binafsi kuwekeza Dodoma

Image
Na. Nancy Kivuyo, MTUMBA Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri ameeleza kuwa Jiji la Dodoma linakua kwa kasi kutokana na uwezeshaji mkubwa unaofanywa na serikali katika miundombinu mbalimbali. Aliyasema hayo katika kikao cha Baraza la Biashara la Wilaya ya Dodoma kilichofanyika katika ukumbi mkubwa wa mikutano wa halmashauri katika Mji wa Mtumba. Alisema kuwa anapongeza mwitikio wa sekta binafsi katika uwekezaji Dodoma. “Ninyi watu wa sekta binafsi nawapongeza sana kwa kufanya uwekezaji wenye tija ikiwemo hoteli kubwa za kisasa zipo hapa Dodoma, kumbi za mikutano na maduka makubwa” alisema Shekimweri ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma. Aliongeza kuwa analipongeza Baraza la Biashara la Wilaya kwa kuweka sera za kuvutia wawekezaji. “Nalipongeza baraza hili kwa kuweka sera Madhubuti zinazofanya wawekezaji kuzikimbilia fursa zilizopo ndani ya Jiji letu la Dodoma. Tuendelee kufanya vizuri kwasababu hapa ndipo kitovu cha makao makuu ya nchi k...

JIJI LA DODOMA LATOA HERI YA SABASABA

Image
 

TANZANIA YAENDELEA KUTANGAZA NA KUKUZA KISWAHILI NA UTAMADUNI WAKE KIMATAIFA

Image
  Lugha ya kiswahili na utamaduni wa mtanzania vimeendelea kuwa kivutio kikubwa kwa wageni mbalimbali wa kimataifa waliotembelea banda la Tanzania katika Wiki ya utamaduni na Kiswahili inayoendelea kwenye maonesho ya biashara ya dunia (Expo 2025) yanayofanyika Osaka, Japan. Kuelekea maadhimisho ya siku ya Kiswahili duniani yanayofanyika kila ifikapo tarehe 7 Julai lugha ya Kiswahili inaendelea kuwafikia watu wengi duniani na mwaka huu 2025 maadhimisho hayo yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Kiswahili kwa amani na mshikamano”. Viongozi waandamizi wa mataifa mbalimbali, wametembelea banda hilo ikiwemo Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi la Japani, Bw. Koichiro Gemba, Mfalme wa Lesotho, Mhe. Letsie III na Mhe. Prudence Sebahizi, Waziri wa Biashara na Viwanda wa Rwanda. Viongozi hao wameonesha kuvutiwa kwa kiasi kikubwa na lugha ya Kiswahili na Utamaduni kupata nafasi katika Maonesho hayo ya Dunia yenye hadhi kubwa. Akizungumza wakati alipotembelea banda hilo Mhe. Sebahizi alie...

MAGEUZI YA ELIMU TANZANIA YAVUTIA NCHI NYINGINE KUJIFUNZA

Image
Mageuzi makubwa yaliyofanyika katika sekta ya elimu nchini, hususan mafunzo ya Amali yameanza kuvutia mataifa mengine barani Afrika kuja kujifunza namna yalivyofanyika na utekelezaji wake. Hayo yalibainishwa jijini Dodoma kufuatia ziara ya Waziri wa Elimu ya Juu, Utafiti, Sayansi na Teknolojia kutoka Jamhuri ya Gambia, Prof. Pierre Gomez ambaye alisema kuwa lengo la kufika Tanzania ni kujifunza mbinu zilizotumika katika kufanya maboresho na maugezi makubwa katika sekta ya elimu. Waziri huyo alisema kuwa Benki ya Dunia iliishauri nchi hiyo kuja Tanzania ili kujionea namna utekelezaji wa Sera, mikakati na miradi mbalimbali katika sekta ya elimu ili kuwawezesha kutekeleza miradi yao kwa ufanisi na tija. “Tumeshuhudia ujenzi wa miundombinu na mifumo ya mafunzo ya vitendo yenye tija katika vyuo mbalimbali ikiwemo DIT, VETA na Taasisi, tunaamini kunufaika zaidi kupitia ushikiano katika nyanja mbalimbali za mafunzo” alisema Prof. Gomez. Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia wa Tanzan...

DKT. BITEKO ASEMA TANZANIA INA USALAMA WA CHAKULA, AWAPONGEZA WAKULIMA

Image
* Asema Serikali inatambua Vyama vya Ushirika ni muhimu kuunganisha nguvu za wananchi na kujiendeleza kiuchumi * Mauzo ya nje ya kahawa na tumbaku 2023/2024 yaongezeka hadi Dola za Marekani 19,300,000 * Maono ya Rais Samia yaanza kuonekana sekta ya kilimo yachangia GDP asilimia 26 * Aziagiza Wizara za Fedha na Kilimo kupata ufumbuzi wa bei za mazao   Na. Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amewapongeza wakulima nchini kwa jitihada zao za kuzalisha mazao kwa wingi na hivyo kusaidia nchi kuwa na usalama wa chakula ikiwa ni pamoja na kuwezesha sekta ya kilimo kuwa na mchango mkubwa katika Pato la Taifa.  Dkt. Biteko alitoa pongezi hizo jijini Dodoma wakati akifunga Kongamano la Siku ya Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani. “Leo sekta ya kilimo ina mchango mkubwa kwenye uchumi wa nchi yetu, tunazungumza mchango wa GDP wa asilimia 26, tunazungumza mazao ambayo yanatupa usalama wa ch...