Walimu Dodoma waaswa uzalendo

 Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WALIMU wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kutanguliza uzalendo katika kazi zao ili kuwafundisha wanafunzi na kuwasaidia katika kujenga taifa lao.

Mchumi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Christian Mauya alipochangia katika kikao cha wadau wa elimu


Kauli hiyo ilitolewa na Mchumi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Christian Mauya alipochangia katika kikao cha wadau wa elimu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Shule ya St. Gasper jijini Dodoma.

Mauya alisema “mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, mimi binafsi Ndugu zangu walimu nataka kuzungumzia kipengele cha pili, kipengele cha uzalendo. Sisi, walimu tunakubaliana kabisa tunakutana na changamoto nyingi sana, lakini nilikuwa naomba sana tuishi katika uzalendo wetu, uzalendo Tanzania. Hautakaa sehemu yeyote katika maisha yako yawe yamenyooka, uzalendo kwanza, hebu pigania Tazania yako”.

Aliwakumbusha kuwa wapo makao makuu Dodoma kwa ajili ya kuwafundisha wanafunzi. “Niwakumbushe kuwa mmeletwa makao makuu kuhakikisha wanafunzi wa Dodoma wanapata elimu na wanafaulu, hebu kaa katika eneo hilo ili kuacha alama kwa kazi unayofanya. Serikali inatuhangaikia sana na inatujali sana, hebu na sisi tuangalie nafasi yetu ni nini kwenye ile dhamana tuliyopewa” alisema Mauya.

Akiongelea changamoto ya miundombinu katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema kuwa yatapungua kwa kiwango kikubwa. “Nikupongeze wewe mheshimiwa mkuu wa wilaya, raia namba moja katika Wilaya ya Dodoma. Wakati watu wanawasilisha kulikuwa na hoja ya miundombinu ya madarasa, madawati, vyoo, ofisi za walimu, nyumba za walimu na hosteli, walimu oyee!, walimu safii!. Mheshimiwa mkuu wa wilaya kwetu haya ni maelekezo. Sisi kama Divisheni ya Mipango na Uratibu na mimi kama Mchuni ni kuhakikisha matatizo hayo tunayapunguza kwa kiwango kikubwa” alisema Mauya kwa kujiamini.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma