Maeneo ya Shule kupimwa Dodoma

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri ameagiza maeneo yote ya shule yapimwe na kupatiwa hati miliki ili kuepuka migogoro ya Ardhi inayotokana na uvamizi wa mipaka ya shule.


Alhaj Shekimweri aliagiza maeneo ya shule yaliyopo sasa yapimwe na kutengenezewa hati miliki. Alisema kuwa utekelezaji huo utasaidia kuepusha migogoro ya Ardhi inayosababishwa na wananchi kuvamia maeneo ya shule.

Aidha, alishauri ujenzi wa shule katikati ya mji ujielekeze kwenye majengo ya maghorofa ili katika eneo dogo litumike vizuri. “Nichukue nafasi hii kuwashukuru wenzetu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) wameanza kutuunga mkono. Lakini pia mapato ya ndani ya halmashauri wameanza kufanya hivyo” alisema Alhaj Shekimweri.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma