Wadau wa Elimu kukutana ngazi ya chini

 Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MSTAHIKI Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe amewashauri wadau wa elimu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuwa vikao hivyo viwe vinaanzia ngazi ya mitaa na kata ili wananchi wengi waweze kushiriki katika maendeleo ya sekta ya elimu.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe akisisitiza jambo


Ushauri huo aliutoa katika kikao cha wadau wa elimu Halmashauri ya Jiji la Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa Shule ya Msingi St. Gasper iliyopo jijini Dodoma.

Prof. Mwamfupe alisema “nilidhani kwamba siku kama leo tutambue kwamba changamoto zinazotukabili katika sekta ya elimu ni za kienyeji zaidi (localized) ziko zaidi katika maeneo husika. Kama ndivyo, ili vikao vya wadau wa elimu viwe endelevu tuvishushe kutoka ngazi hii hadi katika maeneo yetu tukawape watu uhuru wa kuongea ili siku kama ya leo watu waje na mifano ya vikao katika maeneo mengi zaidi. Mchakato huu ni muhimu kuanzia ngazi za chini zaidi ambapo tunawafahamu watu hata wachangiaji kwa majina na tunawafahamu watoro kwa majina”.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma