BenPaul achangia Elimu Dola 300
Na.
John Masanja, MIYUJI
Dola
300 za BenPaul kwenda kuunga mkono jitihada za elimu katika Halmashauri ya Jiji
la Dodoma kabla ya kuteuliwa kuwa balozi wa Mfuko la Lishe.
Msanii
wa muziki wa kizazi kipya Bernard Paul alimaarufu BenPol amechangia kiasi cha dola
300 za kimarekani ikiwa ni ushiriki wake katika kuunga mkono jitihada za elimu
ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
Msanii
BenPol alichangia kiasi hicho wakati wa kikao cha wadau wa Elimu na utoaji wa tuzo
za kitaaluma kilichoandaliwa na Ofisi ya Halmashauri Jiji la Dodoma na
kufanyika katika ukumbi wa Shule ya Msingi St. Gasper jijini Dodoma.
“Nitoe
wito na ombi kwa wazazi, walimu na wadau wote, tuendelee kuwaunga mkono vijana
wetu kwenye elimu lakini pia tusiwakataze wanapopenda kufanya sanaa kwasababu
vyote viwili vinalipa. Elimu inalipa na sanaa ni ajira” alihitimisha BenPol.
Sanjari
na hayo msanii BenPol aliteuliwa na wajumbe wa kikao hicho kuwa Balozi wa Mfuko
wa Lishe ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kuahidi kufanya kazi kwa weledi
ili kufikia malengo yaliyowekwa.
Comments
Post a Comment