CCDO Sichona apongeza Azimio Mfuko wa Lishe Dodoma
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
MKUU wa Divisheni ya
Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Charity Sichona amepongeza
azimio la kuanzisha Mfuko wa Lishe wa halmashauri na kusema kuwa utakwenda
kutatua changamoto za lishe.
Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Charity Sichona akipongeza Azimio la Mfuko wa Lishe |
Pongezi hizo alizitoa
alipokuwa akichangia katika kikao cha wadau wa elimu wa Halmashauri ya Jiji la
Dodoma kilichofanyika katika Shule ya Msingi St. Gasper iliyopo jijini hapa.
Sichona alisema
“nikupongeze na kikao chako kwa kuja na azimio la kuanzisha mfuko wa lishe wa
halmashauri. Mfuko huo utaenda kutatua matatizo ya lishe na hata ukatili kwa watoto.
Mimi kazi yangu kubwa ni kuongea na makundi maalum na huwa tunaongea na watoto
wa kike na unakuta wengi wanadanganyika kutokana na kuwa na njaa shuleni.
Watoto wa kike wanadanganywa na vijana waendesha bodadoba, wanadanganywa na
makondakta wa daladala na mafundi wa gereji”.
Akiongelea ushirikishaji
jamii katika kutatua changamoto za sekta ya elimu alisema kuwa ni jambo la
muhimu. “Ushauri wa pili ni kushirikisha jamii katika changamoto za shule.
Jamii inaposhirikishwa changamoto katika eneo husika ile changamoto inaweza
kupungua na kumalizika kabisa kwa sababu inakuwa sehemu ya utatuzi. Huwa
tunashirikisha wazazi na jamii katika masuala ya ujenzi. Ila kwenye masuala ya
utoro na lishe unakuta jamii haishirikishwi sana kutoa utatuzi. Nashauri kwa
walimu wakuu na maafisa elimu kuweza kushirikisha jamii husika na kwenye
mikutano kupata nafasi ya kuongea na jamii ili kuwa na uelewa na makubaliano ya
pamoja” alishauri Sichona.
MWISHO
Comments
Post a Comment