Prof. Mwamfupe apongeza wadau wa elimu


Na. John Masanja, MIYUJI

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe awapongeza wadau wa elimu kwa jitihada zao kwenye kukuza sekta ya elimu na kuchangia ufaulu wa wanafunzi.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe


Pongezi hizo alizitoa kwa walimu, wazazi na wadau mbalimbali wa elimu kwa ushirikiano mzuri katika kukuza na kuinua sekta ya elimu ndani ya Jiji la Dodoma kwenye kikao cha wadau wa elimu na utoaji tuzo za kitaaluma kilichofanyika katika ukumbi wa Shule ya Msingi St. Gasper jijini Dodoma.

“Natambua sana kuna changamoto nyingi ambazo mnakutana nazo wakati wa utendaji kazi wenu lakini hamjawahi kutuangusha na haya mafanikio tunayoyaona sasa hivi katika elimu ni matunda ya uwekezaji wa pamoja” alisema Prof. Mwamfupe.

Vilevile, alipendekeza kufanyika kwa vikao vya wadau wa elimu kuanzia ngazi za chini ambako watu wengi hufikiwa katika kutoa ushauri na kuona namna gani mawazo yao yatakuwa na manufaa katika kuleta mabadiliko ya elimu kiujumla ndani ya Jiji la Dodoma.

Kwa upande wake mlezi wa taaluma kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Justine Machela, ambaye pia ni Afisa Taaluma wa Mkoa wa Dodoma alisema kuwa uwajibikaji ni moja ya nguzo ya kuinua ubora wa elimu na ufaulu Dodoma. Akinukuu kutoka kwenye wimbo ulioimbwa na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Dodoma wakati wa kikao hicho na hivyo, kuwataka kila mmoja kwenda kuwajibika ipasavyo kwa matokeo chanya ya kielimu ndani ya Jiji la Dodoma. “Jiji la Dodoma na vitu vyake vyote, vinatakiwa kuendana na hadhi ya makao makuu ya nchi, chama na serikali” alisema Machela.

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma