Posts

Showing posts from January, 2024

DC Shekimweri awataka wazazi kuwa karibu na watoto wao

Image
Na. Arafa Waziri, DODOMA MAKULU Mkuu wa Wilaya wa Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri aliwataka wazazi kuwa karibu na watoto wao ili kuwaepusha   na vitendo vya kikatili ili wawe katika mazingira salama.   Mkuu wa Wilaya wa Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri akiongea na walimu na wazazi  Aliyasema hayo wakati alipotembelea Shule ya Msingi Kisasa na kuongea na walimu na wazazi shuleni juu ya masuala ya kupinga ukatili wa kijinsia na uelimu kwa ujumla. Alhaj Shekimweri alisema kuwa ukatili wa kijinsia hutokea katika familia kutokana na kuaminiana sana baina ya wanafamilia. “Upo ukatili wa kijinsia, tafiti zinaonesha ukatili wa kijinsia kwa watoto asilimia kubwa wanafanyiwa na ndugu wa karibu Dunia imebadilika sana hivyo, nawasisitiza hatuna budi kuchukua tahadhari katika kuwaangalia watoto kwa karibu’’ alisema Shekimweri. Alisema kuwa ni vema wazazi kufuatilia mienendo ya watoto wao kwa kuangalia watu wanaokutana na kuhusiana nao ili kubaini kama wanafaa kumjenga mtoto h...

Wazazi watakiwa kutowafisha wanafunzi wenye ulemavu Dodoma

Image
Na. Leah Mabalwe, DODOMA MAKULU   Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri amewataka wazazi kutowaficha watoto wenye uhitaji maalum na badala yake kuwapeleka shule kwa sababu nao wanatakiwa kupata elimu iliyo bora.   Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri akikagua kazi za watoto wenye mahitaji maalum Kauli hiyo aliitoa alipokuwa akiongea na Jumuiya ya Shule ya Msingi Dodoma Viziwi alipofanya ziara ya kawaida kutembelea shule hiyo iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   Alhaji Shekimweri alisema kuwa kila mzazi anatakiwa kumpeleka mtoto wake shule hata kama anaulemavu kwasababu ni haki yake ya msingi. “Nitoe kauli hii kwa wazazi wote, kila mtoto asiachwe nyuma, kila mtoto ananafasi ya kupata elimu na sio elimu tu na baadae kuweza kuitumikia nchi katika nafasi mbalimbali. Wazazi wote wasifiche watotot wao wenye changamoto wakakosa nafasi ya kusoma, sio tu mnakuwa hamuwatendei haki watoto bali hamjitendei haki nyie kama wazazi. Wapo waz...

MABARAZA YA ARDHI YANAMCHANGO KATIKA KUSULUHISHA MIGOGORO YA ARDHI

Na. Eleuteri Mangi, WANMM   Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia Mabaraza ya Ardhi na Nyumba imeshiriki uzinduzi wa Wiki ya Sheria jijini Dodoma yakiongozwa na Mhe. Dkt. Tulia Ackson Spika wa Bunge la Tanzania.   Uzinduzi huo umefanyika Januari 27, 2024 katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma ukitanguliwa na matembezi ya uzinduzi wa Wiki ya Sheria ambao umehusisha viongozi mbalimbali wa mahama, watumishi wa umma na wananchi kutoka jiji la Dodoma.   Akizungumzia ushiriki wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba, Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi Dodoma Bw. Jackson Kanyerinyeri amesema kuwa moja ya jukumu lao ni kutoa elimu kwa wananchi wanaotembelea banda hilo katika masuala ya ardhi, migogoro ya ardhi namna inavyotatuliwa katika mabaraza hayo hadi kutolewa hukumu.   Bw. Kanyerinyeri ameongeza kuwa wamepata wasaa mujarabu wa kuwaeleza wananchi juu ya mabadiliko ya Sheria Na 3 ya 2021 ambayo imeondoa mamlaka ya mabaraza ya Kata kusikiliza ...

MABARAZA YA ARDHI YANAMCHANGO KATIKA KUSULUHISHA MIGOGORO YA ARDHI

  Na. Eleuteri Mangi, WANMM   Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia Mabaraza ya Ardhi na Nyumba imeshiriki uzinduzi wa Wiki ya Sheria jijini Dodoma yakiongozwa na Mhe. Dkt. Tulia Ackson Spika wa Bunge la Tanzania.   Uzinduzi huo umefanyika Januari 27, 2024 katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma ukitanguliwa na matembezi ya uzinduzi wa Wiki ya Sheria ambao umehusisha viongozi mbalimbali wa mahama, watumishi wa umma na wananchi kutoka jiji la Dodoma.   Akizungumzia ushiriki wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba, Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi Dodoma Bw. Jackson Kanyerinyeri amesema kuwa moja ya jukumu lao ni kutoa elimu kwa wananchi wanaotembelea banda hilo katika masuala ya ardhi, migogoro ya ardhi namna inavyotatuliwa katika mabaraza hayo hadi kutolewa hukumu.   Bw. Kanyerinyeri ameongeza kuwa wamepata wasaa mujarabu wa kuwaeleza wananchi juu ya mabadiliko ya Sheria Na 3 ya 2021 ambayo imeondoa mamlaka ya mabaraza ya Kata kusiki...

Mkoa wa Dodoma wamtakia heri ya kuzaliwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan

Image
Na. Dennis Gondwe, KIKOMBO MKOA wa Dodoma umempongeza na kumtakia heri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa siku yake ya kuzaliwa na kumtakia maisha marefu ili aendelee kuwaongoza watanzania. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule  Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule katika halfa ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyofanyika katika makao ya taifa ya kulelea watoto- Kikombo, Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Senyamule alisema “sisi Mkoa wa Dodoma tunatoa pongeza kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza umri akiwa na nguvu na afya njema na maono ya kuliongoza taifa. Chini ya uongozi wake tunafuraha na amani”. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma alimtaja Rais kuwa ni mtu mwenye hekima sana na mchapa kazi. “Mheshimiwa Rais ametujengea uhusiano mzuri ndani na nje ya nchi. Hakika uongozi wake umeifanya Tanzania kuwa nchi pendwa duniani. Ameonesha ku...

LTIP Yatambua Vipande vya Ardhi 11,000 Nzega

Image
Na Magreth Lyimo, WANMM Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP) unaotekelezwa chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi umetambua vipande vya ardhi takribani 11,000 katika Halmashauri ya Mji wa Nzega ikiwa lengo ni kutambua takribani vipande 20,000. Kiongozi wa Timu inayotekeleza  M radi  wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi   Bw. Nolasko Matsuva  akielezea namna mradi huo unavyotekelezwa katika Halmashauri ya Mji wa Nzega Mkoani Tabora Hayo yalisemwa Nolasko Matsuva, Kiongozi wa Timu inayotekeleza mradi huo katika halmashauri ya mji wa Nzega Mkoani Tabora wakati akielezea mafanikio yaliyopatikana wakati wa utekelezaji wa Mradi huo. ‘‘Katika Halmashauri ya Mji wa Nzega utekelezaji wa Mradi ulianza na shughuli za uwandani Desemba 5, 2023 katika Mtaa wa Maporomoko, Uwanja wa ndege, Upiriri, Ushirika, mpaka sasa tuko mtaa wa Nyasa ambapo tumetambua vipande vya ardhi takribani 11,000’’ alisema Matsuva. Katika mwitikio wa wa...

TANESCO Ddodoma kuendelea kuboresha miundombinu ya umeme Jiji la Dodoma

Image
Na. Mwandishi Wetu-DODOMA SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Dodoma limetoa semina kwa madiwani wa kata zote 41 za Jiji la Dodoma lengo likiwa ni kueleza mikakati ya shirika hilo pamoja na miradi inayotekelezwa katika Mkoa wa Dodoma. Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma, Charles Mamba,akizungumza wakati akifungua Mkutano wa Madiwani, kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ulioandaliwa na Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma Akitoa elimu jijini Dodoma, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Donasiano Shamba alisema kikao hicho kimejumuisha Madiwani, Kamati ya Usalama Wilaya na Polisi kata wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Kikao hiki kimehusisha madiwani kutoka kata zote 41 za Jiji la Dodoma pamoja na Polisi kata lengo ni kueleza mikakati yetu lakini pia kueleza changamoto zinazotukabili sisi kama shirika hasa suala la uharibifu wa miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme” alisema Mhandisi Shamba...

Jiji la Dodoma lakemea utapishaji maji taka

Image
Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imekemea tabia ya baadhi ya wakazi kutapisha vyoo kipindi cha mvua na kusababisha kinyesi kwenda kwenye maji yanayotumiwa na wananchi. Maji taka Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti wa taka ngumu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alipokuwa akiongea na mamia ya wakazi wa Kata ya Chamwino waliojitokeza kufanya usafi wa pamoja siku ya Jumamosi. Kimaro alisema “kuna tabia imeibika kwa baadhi ya wakazi wa Kata ya Chamwino kutapisha vyoo. Ndugu zangu tabia hiyo halikubaliki kutapisha vyoo kwa sababu mvua inaponyesha inasomba kile kinyesi na kupeleka kwenye vyanzo vya maji. Maji hayo tunayatumia sisi wenyewe kwa matumizi ya kawaida. Nitumie nafasi hii kuwataka wenye tabia hiyo waache mara moja na tukikukamata tutakuchukulia hatua kwa mujibu wa sheria”. Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti wa taka ngumu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro akitoa karipio Alisema kuwa eneo la Kat...

Kata ya Chamwino yatakiwa kuchukua tahadhari ya Kipindupindu

Image
Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imefurahishwa na muitikio wa wakazi wa Kata ya Chamwino kushiriki katika mazoezi ya usafi wa mazingira na kuwataka kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu. Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti taka ngumu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro akiongea na mamia ya wakazi wa Kata ya Chamwino Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti taka ngumu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alipokuwa akiongea na mamia ya wakazi wa Kata ya Chamwino waliojitokeza kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya kata hiyo. Kimaro alisema “nichukue nafasi hii kuwashukuru sana wakazi wa Kata ya Chamwino kwa jinsi mlivyojitokeza kwa wingi kufanya usafi katika eneo la makaburi ya Hijra na maeneo mengine ya kata. Tulichokifanya hapa ni ibada tosha kwa sababu tumesafisha eneo tulipowalaza ndugu zetu. Lakini niwapongeze kwasababu mmekuwa mkijitokeza kwa wingi kufanya usafi katika makazi n...

Bazara la Madiwani Jiji la Dodoma lapitisha rasimu ya Mpango na Bajeti shilingi 146,287,642,299 kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma limepitisha rasimu ya mapendekezo ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 jumla ya shilingi 146,287,642,299.70 ikitajwa kuwa ni bajeti ya wananchi. Mkuu wa Divisheni ya Mipango na Uratibu, Francis Kaunda akiwasilisha rasimu ya Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Akiwasilisha kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/2025 katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma Mkuu wa Divisheni ya Mipango na Uratibu, Francis Kaunda alisema kuwa bajeti hiyo imelenga kutatua changamoto za wananchi. “Mheshimiwa Mwenyekiti, mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti ya Halmasahuri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka wa fedha 2024/2025 ni jumla ya shilingi 146,287,642,299.70. Kati ya fedha hizo, shilingi 58,521,926,299.70 ni mapato ya ndani, shilingi 73,852,812,000 ni ruzuku ya mishahara, shilingi 1,168,778,000 ruzuku ya matumi...