Jiji la Dodoma lakemea utapishaji maji taka
Na.
Dennis Gondwe, CHAMWINO
HALMASHAURI
ya Jiji la Dodoma imekemea tabia ya baadhi ya wakazi kutapisha vyoo kipindi cha
mvua na kusababisha kinyesi kwenda kwenye maji yanayotumiwa na wananchi.
![]() |
Maji taka |
Kauli
hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti wa taka ngumu, Halmashauri
ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alipokuwa akiongea na mamia ya wakazi wa Kata
ya Chamwino waliojitokeza kufanya usafi wa pamoja siku ya Jumamosi.
Kimaro
alisema “kuna tabia imeibika kwa baadhi ya wakazi wa Kata ya Chamwino kutapisha
vyoo. Ndugu zangu tabia hiyo halikubaliki kutapisha vyoo kwa sababu mvua
inaponyesha inasomba kile kinyesi na kupeleka kwenye vyanzo vya maji. Maji hayo
tunayatumia sisi wenyewe kwa matumizi ya kawaida. Nitumie nafasi hii kuwataka
wenye tabia hiyo waache mara moja na tukikukamata tutakuchukulia hatua kwa
mujibu wa sheria”.
![]() |
Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti wa taka ngumu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro akitoa karipio |
Alisema
kuwa eneo la Kata ya Chamwino kuna mtandao wa maji taka wa Malmaka ya Majisafi
na Usafi wa Mazingira Dodoma mjini (DUWASA). “Naomba pale mtakapoona kuna
tatizo la mfumo wa maji taka mtoe taarifa mapema ili wenzetu waweze kulifanyia
kazi. Maana tukiacha hivyo, itakuwa chanzo cha ugonjwa wa kipindupindu. Aidha,
tunapokula chakula tule cha moto, tunawe mikono kwa maji na sabuni na hiyo
ndiyo iwe tabia yetu. Tunafahamu usafi ni ustaarabu na unaanza na mimi” alisema
Kimaro.
Wakati
huohuo, alivitaka vikundi vya kuzoa taka katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri
ya Jiji la Dodoma kutimiza wajibu wao wa kuzoa taka kwenye makazi kwa wakati.
“Nitoe wito kwa vikundi vya uondoshaji taka kwenye makazi ya watu kutimiza
wajibu wao. Mimi sitasita kushauri kata kuondoa kikundi ambacho hakifanyi
vizuru katika uondoshaji taka. Vikundi vyote tulivyovipa dhamana ya kuondoa
taka kwenye makazi ya watu viondoshe taka na visiwe sababu ya kutusababishia
ugonjwa wa kipindupindu kwenye makazi ya watu. Hatuwezi kukubali kipindupindu
kutokea makao makuu ya nchi” alisisitiza Kimaro.
Kwa
upande wake Mkazi wa Kata ya Chamwino, Mwanaidi Juma alisema kuwa Halmashauri
ya Jiji la Dodoma imejitahidi kutoa elimu juu ya usafi wa mazingira. “Niseme
ukweli, suala la usafi na umuhimu wake tumeelezwa sana halmashauri. Ni jukumu
letu kufanya usafi wa mazingira. Natamani ifike wakati suala la usafi wa
mazingira liwe ni utamaduni wetu na siyo kusubiri serikali kutuhamasisha
kufanya usafi. Mfano bwana Kimaro kaongelea suala la kipindupindi, mtu akipata
kipindupindu inayoathirika ya kwanza ni familia yake na mtu akifa hawezi
kurudu. Maana yake ni bora kuchukua tahadhari ya usafi ili tuendelee kuwa
salama” alisema Juma.
Usafi
wa pamoja siku ya Jumamisi umefanyika katika Kata ya Chamwino ukihusisha
maafisa waandamizi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, mamia ya wakazi wa kata
hiyo na Mbunge wa Jimbo la Urambo alikuwa sehemu ya washiriki.
MWISHO
Comments
Post a Comment