Mradi wa ukamilishaji Bweni Mbalawala Sekondari

Na. Nancy Kivuyo, MBALAWALA

Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma imefanya ziara katika Shule ya Sekondari Mbalawala kwa dhumuni la kukagua mradi wa ukamilishaji bweni ya wanafunzi kama moja ya miradi inayopaswa kukamilika na kutumika na wanafunzi wanaotoka maeneo ya mbali.




Akisoma taarifa ya mradi wa ukamilishaji wa bweni la wasichana Shule ya Sekondari Mbalawala, Kaimu Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Fredrick Mwakisambwe alisema kuwa mradi ulianza kutekelezwa tarehe 14 Mei, 2009 chini ya usimamizi wa ofisi ya kata hadi hatua na upigaji plasta.

“Ilipofika mwaka 2017 shule ilipokea kiasi cha shilingi 20,000,000 kutoka mapato ya ndani ya halmashauri kwa ajili shughuli za ukamilishaji wa kuondoa paa la zamani, kuongeza kozi moja ya tofali, kuweka dari (gypsum board) na kuweka mifumo ya umeme. Kujenga chumba cha matroni, kuskimu na kupaka rangi nje na ndani, kuchimba shimo la choo kwa ajili ya matundu manne na kujenga boma la choo hadi kufikia hatua ya lenta. Mwaka 2023 Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilitoa kiasi shilingi 10,000,000 kwa ajili ya kazi zifuatazo za kukamilisha ujenzi wa choo chenye matundu manne na mifumo yake na kuweka mfumo wa umeme katika bweni na choo” alisema Mwl. Mwakisambwe.

Jengo la bweni la wasichana katika Shule ya Sekondari Mbalawala lina uwezo wa kuchukua wanafunzi 44 na matroni mmoja na ilianzishwa mwaka 2008 ikiwa na jumla ya wanafunzi 45 ambapo wavulana walikuwa 27 na wasichana walikuwa 18, kwa sasa shule ina jumla ya wanafunzi 557, kati yao wavulana 251 na wasichana 306.





MWISHO

Comments

Popular Posts

Mbunge Mavunde akabidhi Kompyuta kwa Kata 41 za Jiji la Dodoma

Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo Dodoma watarajia makubwa Mradi wa TACTIC

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma