Wananchi 2,700 Kunufaika, Mradi wa Ukarabati Maji Taka
Na. Faraja Mbise, KIWANJA CHA NDEGE
Takribani wakazi 2,700 wanatariwa
kunufaika na mradi wa ukarabati wa mtandao wa maji taka unaotekelezwa na
Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) katika Mtaa wa Area
C na D, Kata ya Kiwanja cha Ndege, jijini Dodoma.
Hayo yalisemwa na Mhandisi wa Maji taka
DUWASA, Mhandisi Yohana Koroso alipokuwa anawasilisha taarifa ya mradi wa
ukarabati wa mtandao wa Maji taka katika eneo la Area C na D wakati wa ziara ya
Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma.
Mhandisi Koroso alisema “mradi
unagharimu jumla ya shilingi bilioni 4.9 ambao utawezesha jumla ya watu 2,700
kunufaika na mradi huo katika uondoaji wa Maji taka”.
Akizungumza wakati
wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma, alisema
ukarabati wa miundombinu ya Maji taka una urefu wa Kilomita 19 za mabomba ya
plastiki (PVC). Mhandisi Koroso alisema “ukarabati wa miundombinu ya maji taka
maeneo ya Area C na D wenye urefu wa Kilomita 19 za mabomba ya plastiki (PVC)
kuanzia kipenyo cha 160mm hadi 315mm”.
Sambamba na hilo, alisema utekelezaji
wa kazi za mradi na hatua zilizofikiwa kwa kiwango cha ukamilifu wa mradi huo
ni jumla ya asilimia 96. “Kazi za mradi na hatua zilizofikiwa kwa sasa ni
ulazaji wa mabomba mapya ya plastiki daraja B na viungio vyake, yenye kipenyo
kuanzia 160mm mpaka 315mm ambao umefikia jumla ya mita 19,159 za mabomba kati
ya mita 20,274 zimelazwa na ukamilifu wake ni asilimia 94.5. Ujenzi wa jumla ya
chemba 936 kati ya 962 zimejengwa na kazi inaendelea ambapo imekamilika kwa
asilimia 97.3” alisema Mhandisi Koroso.
Hata hivyo, alisema kuwa kutokana na
changamoto kadha wa kadha hasa kuchelewa kwa malipo ya hati mbalimbali za madai
ya Mkandarasi, imepelekea mradi kutokukamiliaka ndani ya muda uliopangwa.
Mradi huo wa Maji taka uliandaliwa na
DUWASA kwa kushirikiana na Wizara ya Maji, utekelezaji wake unafanywa na Mkandarasi
Shanxi Constructions Engineering Corporation and Mineral Company chini ya
usimamizi wa DUWASA.
MWISHO
Comments
Post a Comment