Dodoma Queens yawakalisha Dodoma Jiji

Na. Mussa Richard, DODOMA

Klabu ya mpira wa kikapu ya wanawake ya Dodoma Queens imeibuka kidedea kwa kushinda vikapu 44 kwa 33 vya Dodoma jiji katika bonanza la kuelekea kilele cha Siku ya Wanawake Duniani Machi 8, mchezo uliopigwa katika viwanja vya Shule ya Sekondari Dodoma.





Akizungumza baada ya mchezo huo, nahodha wa timu ya Dodoma Queens Respicia Mkulas alisema “mchezo ulikuwa mzuri,na tumeweza kupata ushindi  wa tofauti ya seti 10, nitoe rai kwa wanawake wenzangu  kujitokeza kwa wingi kushiriki katika michezo mbalimbali kwasababu michezo ni afya, michezo ni burudani na pia michezo ni dawa inakukinga dhidi ya magonjwa”.

Nae, Jeni Kutawe, Nahodha wa timu ya kikapu ya Dodoma Jiji baada ya mchezo kutamatika akawaita wanawake kote nchini kushiriki kwenye mazoezi ili kuimarisha afya na kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa.

“Mchezo ulikuwa mzuri tumefurahi japo tumepoteza, mchezo huu ulikuwa siyo wa kushindana ulikuwa ni mchezo wa burudani kuhakikisha wote tunafurahi na bonanza linaenda vizuri, ushauri wangu kwa wanawake wote wajitokeze kufanya mazoezi kwa wingi kwani mazoezi yanasaidia kulinda afya ya mwili” alisema Kutawa.




Wakati akifungua Bonanza hilo Mgeni David Msasa, kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma akatoa wito kwa wanawake kujitokeza ipasavyo kushiriki kwenye michezo ili kutengeneza usawa katika michezo na jamii.

“Nitoe shime kwa wanawake waliofika hapa na ambao hawajafika hapa wajitokeze kwa wingi kufanya mazoezi kwasababu michezo ni afya lakini pia kupitia michezo tunatengeneza mawasiliano mazuri baina yetu na wengine, niwapongeze sana wale ambao mmejitokeza kushiriki bonanza hili ikiwa ni maandalizi kuelekea kilele cha Siku ya Wanawake Duniani, kwahiyo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma na Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma zinawatakia kila la kheri” alisema Msasa.

Siku hii ya wanawake duniani rasmi ilianzishwa tarehe 8 Machi 1975 baada ya Umoja wa Mataifa kuridhia siku hii kutumika kuikumbusha dunia juu ya haki za wanawake kwa lengo la kuongeza chachu katika harakati za mapambano katika usawa kwa mwanamke na mwanamke katika jamii, maadhimisho ya siku ya wanawake duniani mwaka huu kitaifa yatafanyika mkoani Arusha yakiwa na kaulimbiu “Wanawake na wasichana 2025: tuimarishe haki, usawa na uwezeshaji”.

 



MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Mbunge Mavunde akabidhi Kompyuta kwa Kata 41 za Jiji la Dodoma

Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo Dodoma watarajia makubwa Mradi wa TACTIC

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma