DUWASA yamshukuru Rais, Dkt. Samia kutoa kipaumbele huduma za Maji
Na. Faraja Mbise, DODOMA MAKULU
Mamlaka ya
Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) yamshukuru Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuipa kipaumbele katika
kutatua changamoto za upatikanaji wa Maji mjini Dodoma.
Akiwasilisha
taarifa ya utekelezaji wa mradi wa kutoa Maji Njedengwa kupeleka mpaka UDOM,
Mhandisi wa Usambazaji Maji, Peter Shemwelekwa kutoka DUWASA,
alisema kuwa mamlaka inaendelea
kuboresha hali ya upatikanaji wa Maji katika maeneo mbalimbali mjini Dodoma na
pembezoni. “DUWASA ilipewa maelekezo na Wizara ya Maji kuongeza Maji katika
busta ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ili kusaidia kuongeza kiwango cha Maji
katika matanki yaliyopo (UDOM). Kutokana na Changamoto ya Maji kuwa kubwa
katika Chuo Kikuu cha Dodoma. DUWASA iliamua kutoa Maji kutoka bomba kubwa la
inchi sita linalotoka katika Tenki la Njedengwa na kupeleka Maji katika Tenki
la kukusanyia Maji kabla ya kusukumwa kwenda maeneo mbalimbali ya UDOM. Mradi
huu pia unalo tawi linalohudumia nyumba za NHC Iyumbu, pale itakapolazimu.
Mpaka sasa mradi huu umekamilika na tayari umeshaanza kuhudumia Chuo cha UDOM”
alisema Mhandishi Shemwelekwa.
Akiongelea hatua ya utekelezaji, alisema kuwa mradi ulianza kutekelezwa tarehe 24, Januari 2024 na
kukamilika tarehe 2 Machi, 2024, ukihusisha ulazaji wa mtandao wa mabomba
pamoja na viungio vyake wenye urefu wa kilomita 4.564. Mradi huo umepunguza
kero ya upatikanaji wa Maji safi na salama katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
baada ya kukamilika kwake, aliongeza.
MWISHO
Comments
Post a Comment