Uwanja wa Maonesho wa Nanenane wafurika

Na. Flora Nadoo, NANENANE

Uwanja wa maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati Dodoma, wafurika watu kutoka sehemu mbalimbali kwa ajili ya kushuhudia ufunguzi huo.




Mbali na ufunguzi huo wa maonesho ya Nanenane, wananchi washuhudia uzinduzi wa Tukutuku (Pikipiki za miguu mitatu) takribani 100 ambazo zitagawiwa kwa vijana. Kupitia pikipiki hizo vijana watapata faida kubwa sana kwasababu ni pikipiki zilizotengenezwa kisasa zaidi na hivyo zitakuwa zinatoa kahawa ya viwango vya juu sana.

Kwa upande wa burudani, wananchi walifurahia sana wagogo wakicheza ngoma zao za asili kwa umahili mkubwa wakiongozwa na mwalimu wao aliyefahamika kwa jina la Malima.  

Kutokana na kufurika kwa watu hao, watu wenye vyombo vya moto kama bajaji, pikipiki na magari wajipatia faida kubwa tofauti na siku zote kufuatia kutoa huduma ya usafiri.

Habari hii imehaririwa na Janeth Gerald

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma