Wafanyabiashara wanufaika na ufunguzi wa Nanenane na uzinduzi wa SGR


Na. Rahma Abdallah, NANENANE NA KIKUYU KUISNI

Wafanyabiashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamenufaika kutokana na ufunguzi wa maonesho ya siku ya Nanenane yaliyofanyika katika viwanja vya Nanenane Nzuguni jijini Dodoma pamoja na ufunguzi wa treni ya kisasa ya mwendo kasi inayotumia umeme (SGR), ufunguzi huo uliofanyika Kata ya Kikuyu Kusini jijini Dodoma.

Hayo yamezungumzwa na wafanyabiashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma mapema jana katika ufunguzi wa maonesho ya Nanenane pamoja ufunguzi wa Treni ya kisasa inayotumia umeme (SGR).

“Nashukuru Mungu mimi nikiwa kama mfanyabiashara wa chakula nimenufaika sana kwa sababu watu ni mengi sana hatuna budi kumenya viazi vingi ili wateja wetu wanapokuja kukuta kila kitu kiko vizuri pia kupitia ufunguzi huu sisi kama wafanyabiashara tumepata fursa kwasababu kabla ya uzinduzi huu biashara haikuwa nzuri kabisa kwa sababu ya ukosefu wa watu (wateja) lakini kwa kupitia uzinduzi huu tumechangamkia na kufanya biashara’’ alisema mfanyabiashara Emmanuel Edward.

Nae, mfanyabiashara wa chombo cha moto (dereva wa bajaji) anaefahamika kwa jina la Noel Yonah alisema “siku ya leo ni siku nzuri sana hasa kwetu sisi wafanyabiashara wa vyombo vya moto kwasababu watu ni wengi sana inafikiwa wakati mpaka mimi mwenyewe kama mfanyabiashara nachoka kubeba au kupakia wateja. Yaani wateja wananifata lakini mimi nawaambia mimi siendi kwahiyo, leo tumenufaika sana tunatamani kila siku biashara iwe kama ya leo’’ alisema Yonah.

Kwa upande wa mkazi wa Dodoma, Mariam Alex alisema kuwa biashara ni nzuri. “Leo ni siku ya pesa kama unavyo ona watu ni wengi tena wananchi wa hapa hapa Tanzania. Mimi nikiwa kama mfanyabiashara ninae uza hizi bendera ndogo za Taifa letu la Tanzania nimepata pesa nyingi kwasababu kila mtu ananunua bendera ili aonekane ni mwananchi halali wa Tanzania. Kwahiyo, biashara yangu imeenda vizuri kwasababu watanzania wenzangu wameniunga mkono namshukuru Mungu, lakini pia nisiwe mchoyo wa fadhila kuwashukuru na watanzania wenzangu’’ alisema Alex.

Aliongeza kwa kusema kuwa uzinduzi na ufunguzi ni chanzo cha fursa. Sisi tukiwa kama wananchi kwasababu, unaweza kubuni na kuanza biashara yako kidogo kidogo na mwisho kuwa mfanyabiashara mkubwa. “Kwahiyo, sisi kama wananchi hasa vijana tuache tabia ya uvivu na tujaribu kujishughulisha ili tuweze kukidhi mahitaji yetu” alisema Alex.

Habari hii imehaririwa na Fadiga James

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma