PM azindua Pikipiki za miguu mitatu kuwawezesha vijana

Na. Flora Nadoo, NANENANE

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amezindua zoezi la usambazaji wa pikipiki za miguu mitatu 100 kwa ajili ya vijana katika viwanja vya Nanenane jijini Dodoma.




Alisema kuwa pikipiki hizo zitatolewa kwa mkopo nafuu sana na marejesho hayatakuwa na riba yoyote. Pikipiki hizi zinamashine ya kusagia kahawa, sehemu za kukaa watu kwa ajili ya kusambaza kahawa” alisema Waziri Bashe.

Alisema kuwa Shirika la kuhudumia viwanda vidogo SIDO wanatengeneza tera la miguu mitatu. “Ndani yake zitakuwa na friji dogo, brenda na sehemu za kuonesha mazao. Mtu ataweza akaihamisha au akakaa sehemu moja ya kudumu. Pia tela hizo zitakuwa na solar panel kwa ajili ya kuifanya kazi hiyo. Tunaanza kugawa kwa ajili ya viwanda” alisema Waziri Bashe.

 

Aidha, serikali ilitoa rai kwa vijana wajitokeze kwa wingi kuchukua pikipiki hizo kwasababu ni chachu ya maendeleo katika jamii na taifa kiujumla. Kupitia pikipiki hizo zitawasaidia kujikwamua kimaendeleo kutoka hali ya chini kimaisha hali hali ya juu. Kwa sababu kutokana na teknolojia waliyoitumia kutengeneza pikipiki hizi ni ya kisasa zaidi hivyo basi, hata kahawa itakayotengenezwa itakuwa ya kisasa zaidi na utapendwa na watu wengi sana.

 

Habari hii imehaririwa na Moureen JohN

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma