Viongozi wamshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kukuza sekta za Mifugo na Uvuvi
Na. Flora Nadoo, NANENANE
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Alexander Mnyeti amshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo ameendelea kuzipa kipaumbele sekta za mifugo na uvuvi ili zichangie katika uchumi wa taifa.
Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan (picha na maktaba)
Shukrani hizo alizitoa wakati akitoa salamu za Wizara ya Mifugo na Uvuvi
katika uzinduzi wa maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika viwanja vya Nanenane
Nzuguni Dodoma.
Mnyeti alisema "Mheshimiwa Rais ameongeza bajeti ya wizara yangu yangu kutoka shilingi bilioni 295.9 mwaka 2023/2024 hadi shilingi bilioni 460.3 kwa mwaka 2024/2025 sawa na nyongeza ya 50.5%. Fedha hizi zitatumika katika kuimarisha
sekta ya mifugo na uvuvi na kuongeza mchango wake katika pato la Taifa.
Pia Waziri wa Kilimo
Mh.Husein Bashe alianza kwa kumshukuru mgeni rasmi Waziri mkuu Mh.Kasim
Majaliwa Kasim kwa kutenga muda wake na kuifanya kazi hiyo.Awashukuru kwa
mchango wao mkubwa sana kwenye kilimo.
Hivyo basi, Husein Bashe alimshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza bajeti ya kilimo kutoka
shilingi bilioni 294.97 mwaka 2021/2022 hadi kufikia bajeti
iliyopitishwa tarehe 7/6/2024 shilingi
trilioni 1.2. Fedha
hizo zilizoongezeka
zitatumika kwenye kilimo. Pia
aliishukuru serikali
kutenga fedha
kwenye kilimo cha umwagiliaji.
Kutokana na mchango wa
serikali kwenye kilimo, imepelekea
uzalishaji mkubwa sana wa mazao. Aidha,
mchango huo umewezesha kufanikisha kupeleka mahindi nchini Zambia kama ilivyokuwa
imesainiwa. Mahindi hayo ni jumla ya tani 600,000. Pia kwa mara ya kwanza NFRA imeuza
mahindi kwa dola ambayo ni historia ya nchi yetu. NFRA imefungua vituo vya
kununua mahindi. Vivyo hivyo, serikali inatoa ruzuku kwenye pembejeo
na kwenye bei ya kununua mazao, ili kuwasaidia wakulima na kuwawekea mazingira
bora, aliongeza.
Alimalizia kwa kusema kuwa serikari yaahidi kwamba hakuna mkulima
yeyote wa mahindi ambaye atakosa sehemu
ya kuuza mahindi yake. Serikali
itanunua mahindi yote yaliyo mikononi mwa wakulima.
Habari hii imehaririwa na Emmanuel Lucas kwa
kushirikiana na Janeth Gerald
Comments
Post a Comment